20 Mar 2025 in Senate:
Thank you, Hon. Speaker, Sir. I rise pursuant to Standing Order No.53(1), to seek a Statement from the Standing Committee on Education regarding the operations of Bandari Maritime Academy in Mombasa County. The Bandari Maritime Academy in Mombasa County is a regional center of excellence for maritime skills development in the blue economy. However, in recent times, the institution has faced several challenges, including delayed salary payments for the lecturers, irregular fee payment structures and the absence of a clear framework for placing students in industrial attachment. These challenges, if not resolved, impact the Academy's operations and daily status as ...
view
19 Mar 2025 in Senate:
Asante, Bw. Spika kwa kunipa fursa hii kuchangia kwenye Kauli iliyoletwa Bungeni na Sen. Abass, Seneta wa Wajir. Amezungumzia masuala ya ugonjwa wa Kala-azar . Ugonjwa huu umeingia katika Kaunti za kaskazini. Wiki iliyopita tulizungumzia Kaunti ya Marsabit, hivi sasa tunazungumzia Kaunti ya Wajir. Zamani, afya haikuwa imegatuliwa. Ilikuwa ni shida kupata wataalamu wa kupambana na majanga kama haya kwa muda mfupi. Kaunti zetu hazijafanya mipango yoyote kuhusiana na magonjwa kama haya. Inakuaje ugonjwa unaingia, wananchi wanafariki, sio mmoja bali wawili watatu. Ripoti ya magazeti ilisema kuwa watu kadhaa wamepoteza maisha yao kwa sababu ya ugonjwa huu. Ni ugonjwa ambao ...
view
19 Mar 2025 in Senate:
Hakuna mandalizi kwenye kaunti ya kupambana na majanga kama haya ambayo yanatokea mara kwa mara na kupoteza Maisha ambayo tungeokoa. Tulipopambana na janga la COVID-19, kaunti nyingi zilijitayarisha na kujenga vyumba vya wagonjwa mahututi. Hivi sasa tunashikwa na magonjwa madogo madogo kama haya ambayo yanaweza kutibiwa na kuepukwa iwapo kaunti zetu zitakuwa imara katika kuangalia afya ya umma katika maeneo yao. Pia ningependa kutoa maoni yangu kuhusiana na Kauli ya Sen. Githuku, Seneta wa Lamu. Kauli ni kuhusiana na ulipaji wa ridhaa kwa watu wanaoadhiriwa na masuala ya kushambuliwa na wanyama pori katika maeneo yetu. Hili limekuwa ni donda sugu. ...
view
19 Mar 2025 in Senate:
Asante Bw. Spika. Kisha tujue ni vipi wanafanya malipo haya. Kuna wengine ambao wamepeleka madai gushi, wamelipwa wakati wale ambao wanastahili kulipwa bado wanangojea na hawajulikani watalipwa lini.
view
19 Mar 2025 in Senate:
Asante Bw. Spika kwa kunipa fursa hii kuchangia Mjadala wa Ripoti ya Kamati ya Fedha na Bugeti ya Bunge hili kuhusiana na mipango ya kuthibiti madeni katika mwaka 2025/2026. Hatuna habari nzuri kuhusiana na deni katika nchi yetu kwa sababu, deni limepanda kutoka trilioni kumi nukta mbili tokea Juni mwaka jana mpaka trilioni kumi na moja kufikia Januari thelathini na moja mwaka huu. Deni hili limeongezeka likiwa ni pamoja na deni la nyumbani la karibu trilioni tano nukta sita na deni la kimataifa la kutoka nchi za inje ambalo ni trilioni tano nukta nne. Katika mipango kama hii iliyoletwa mwaka ...
view
19 Mar 2025 in Senate:
Vile vile, kuna madeni ambayo yamechukuliwa lakini miradi haijaanza. Asubuhi ya leo Waziri wa Maji, Usafi wa Mazingira na Unyunyuziaji alisema hakuna pesa za kulipa ridhaa kwa wale ambao ardhi zao zinachukuliwa kwa hizo miradi za maji. Ukiangalia katika Wizara ya Barabara na Uchukuzi, kuna miradi mingi ambayo imeanzishwa kupitia kwa ufadhili wa wahisani wetu lakini Serikali haijalipa ridhaa wale ambao ardhi zao zinachukuliwa ili barabara hizo zijengwe. Takriban Shilingi bilioni mia mbili zinahitajika kulipa ridhaa kwa wale ambao ardhi zao zinachukuliwa ili miradi hiyo iweze kufanywa. Kwa hivyo, utapata kuwa pesa zimekopwa na zimekaa katika account lakini hakuna kitu ...
view
19 Mar 2025 in Senate:
sababu ya ukosefu wa kulipa madeni ambayo wanachukuwa. Kwa hivyo, hakuna haja ya kujenga nyumba hizi halafu zibaki mahame, na mwishowe popo na wanyama wengine wahamie ndani na kuishi katika nyumba hizi ilhali Wakenya hawawezi kumiliki hizo nyumba. Mhe. Spika, Serikali Kuu inaingilia kazi za kaunti. Unaskia kunajengwa soko na serikali kuu Mjini Mombasa, ilhali soko ile inapaswa kujengwa na Kaunti ya Mombasa. Kilifi wanajengewa masoko na ardhi za kaunti zinachukuliwa na Serikali Kuu kujengwa miradi ambayo serikali za kaunti zinaweza kufanya. Tulipata experience kama hii wakati Serikali Kuu ilipokuja kujenga Mama Ngina Water Front. Walisema sisi tutajenga halafu tutaipeana ...
view
13 Mar 2025 in Senate:
Asante, Mhe. Spika, kwa kunipa fursa hii ili nichangie Taarifa kuhusu milipuko ya mitungi ya gesi katika miji tofauti. Nampongeza Sen. Ojienda kwa kuleta taarifa hii ambayo imekuja wakati mwafaka. Katika Kaunti ya Mombasa, kila siku kuna mioto isiyopungua miwili au mitatu, na mingi inasababishwa na milipuko ya gesi. Mara nyingi, ijapokuwa kuna ongezeko ya matumizi ya gesi kwa matumizi ya kinyumbani hakujakuwa na mfumo wote wa kuwasaidia wale ambao wanatumia gesi hizi kupata elimu kuhusiana na matumizi haya. Kwa mfano, Mhe. Spika, mpira unaoconnect The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version ...
view
13 Mar 2025 in Senate:
mtungi wa gesi na kichwa ambacho kinawaka moto unafaa kubadilishwa baada ya miaka miwili. Lakini, utapata wengine wanatumia ile ile tangu waliponunua mtungi huo. Mara nyingi, hiyo pipe huwa inalika ndani na ikilika inasababisha gesi kuvuja. Ikivuja, inasababisha mlipuko ama moto kwa urahisi. Kwa hivyo, jukumu hili la kupambana na moto pamoja na dharura nyingine ni jukumu la kaunti zetu. Ni lazima kaunti zetu zikishirikiane na Energy and Petroleum Regulatory Authority (EPRA) na wahudumu wa wazima moto waanzishe mikakati ya kuwaelimisha wananchi juu ya matumizi ya gesi kwa sababu mara nyingi wengi wanatumia gesi hizo bila elimu yoyote na inawafanya ...
view
12 Mar 2025 in Senate:
Asante, Bw. Spika. Nimesimama kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu No.51(1) ya Kanuni za Bunge la Seneti kuomba kauli kutoka kwa Kamati ya Kawi kuhusu kupotea kwa nguvu za umeme katika Kaunti ya Mombasa na viunga vyake, hususani mwezi huu mtukufu wa Ramadhan. Kutoka mwanzo wa Mwezi huu wa tatu ambao unaenda sawia na mwezi mtukufu wa Ramadhan, jiji la Mombasa na viunga vyake limeshuhudia kupotea mara kwa mara nguvu za umeme. Hii imeadhiri pakubwa mipango ya ibada na biashara kwa wakazi ikizingatiwa kwamba mwezi huu waumini wengi wa dini ya Kiislamu wanahusika na ibada ya sala ya usiku inayojulikana ...
view