Mohamed Faki Mwinyihaji

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 871 to 880 of 2123.

  • 26 Oct 2022 in Senate: The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate. view
  • 26 Oct 2022 in Senate: Harambee Stars. Kwa bahati mbaya, umri ukawa haumruhusu. Hivyo basi, hakuweza kuingia katika Harambee Stars. Sen. Murkomen ni mtu ambaye anachukulia watu wote kwa usawa na ana heshima kwa binadamu. Kwa hivyo, twamtakia kila la heri katika nyadhifa yake mpya ya Uwaziri. Bw. Naibu Spika, Serikali iliyoondoka imefanya miradi mingi katika Kaunti ya Mombasa. Na sisi tunataka ile imebakia, Sen. Murkomen, ambaye ni Waziri wa Barabara aimalize, ili Mombasa iweze kuwa shwari kama hapo awali. view
  • 25 Oct 2022 in Senate: Asante, Bw. Naibu wa Spika, kwa kunipa fursa hii. Nimesimama kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu Nambari 51(1), kuomba Taarifa kutoka kwa Kamati ya Kudumu ya Usalama wa Taifa, Ulinzi na Uhusiano wa Kimataifa kuhusu kuvunjiliwa mbali kwa Kitengo cha Upelelezi wa Jinai. Katika taarifa hiyo, Kamati iangazie yafuatayo- (1)Sababu zilizopelekea kuvunjwa kwa Kitengo hicho kwa ghafla; (2)Idadi ya watu waliouliwa au kukamatwa na kitengo hicho, na iwapo kuna wananchi wowote ambao walikamatwa na kuwekwa kizuizini bila kupelekwa Mahakamani; (3)Iwapo Serikali itawalipa ridhaa wale wote walioshikwa bila ya makosa ama bila kupelekwa Mahakamani, na; (5)Hatua zitakazochukuliwa kwa maafisa waliohusika na ... view
  • 25 Oct 2022 in Senate: The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate. view
  • 25 Oct 2022 in Senate: Bw. Naibu wa Spika, kwa kuongezea ni kwamba, hivi majuzi kulikuwa na taarifa kwamba mhe. Rais amevunjilia mbali kile kitengo cha Upelelezi wa Jinai kinachoitwa Special Service Unit (SSU). Tukiangalia kutoka Mwaka wa 2013 hadi 2022, Zaidi ya watu 2,000 wameweza kupotezwa na wengine kuweza kuuawa kinyama na vitengo vya usalama. Hawa wote wameuawa bila kupelekwa mahakamani. Hivyo basi, hawakupewa nafasi ya kujitetea kwa yale makosa ambayo walituhumiwa kufanya. Nikizungumzia Mombasa, waliuliwa Sheikh Abud Rogo, marehemu makaburi na wengine wengi. Wote waliouliwa kinyama na polisi bila sababu zote za kisheria. view
  • 25 Oct 2022 in Senate: Kuvunjiliwa mbali kwa kitengo hicho hakutatatua maswala haya. Hii ni kwa sababu, Serikali ambayo ilikuwa mamlakani ilikuwa ni “nusu mkate” kuanzia mwaka wa 2013 mpaka 2022. Kwa hivyo, walihusika kwa kiwango fulani kwa vitendo hivi vya maafisa wa usalama. view
  • 25 Oct 2022 in Senate: Tunaomba kwamba Kamati hii iangalie kwa undani zaidi. Na ikiwezekana hata kama ni mapendekezo, yawe na Tume Huru ya kuchunguza maswala haya kama vile Goldenberg na mengineyo. Hii itafanya siku za usoni tusiwe na shida kama hizo. Hii ni kwa sababu Katiba yetu inamlinda mtu yeyote katika nchi yetu ya Kenya. view
  • 18 Oct 2022 in Senate: On a point of information. Madam Temporary Speaker. view
  • 18 Oct 2022 in Senate: Madam Temporary Speaker, I would like to inform my brother, Sen. (Dr.) Khalwale, who resided in Mombasa for a long time. Firstly, we are grateful for his services to Port Reitz District Hospital then. However, at the moment, there are about seven ferries which operate across the Likoni Channel. Even in Mtongwe, they have started the service. Unfortunately, after the incident, which occurred in the year 2020, where the lady, Mariam, drowned with her daughter, the Kenya Ferry Services was transferred to Kenya Ports Authority. So, there is no longer Kenya Ferry Services. It is now a department of Kenya ... view
  • 18 Oct 2022 in Senate: Bi. Spika wa Muda, asante kwa kunipa fursa hii kuchangia ardhihali ambayo imeletwa Bungeni na Seneta wa Homa Bay, Sen. M. Kajwang’. Jambo ambalo Sen. M. Kajwang’ amezungumzia katika ardhihali hii ni muhimu sana kwa sababu usafiri wa majini hutumika hususan katika Jiji la Mombasa na Mji wa Lamu ambako kuna visiwa vingi. Tangu huduma za ferry zianzishwe kule Mombasa, hazijawahi kupanuliwa kwa njia yoyote. Ijapokuwa ferry zimeongezeka, hakujakuwa na upanuzi wowote wa huduma za ferry katika Kaunti ya Mombasa. Labda kina Sen. M. Kajwang’ wanalia ngoa kwamba hawana ferry . Kwetu sisi, huduma zinazotolewa pale ni duni sana kwa ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus