Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 11 to 20 of 512.

  • 8 Apr 2025 in National Assembly: Asante bwana Spika. Kwa niaba yangu, familia yangu, na watu wangu wa Lamu Mashariki ninaowakilisha, natoa rambirambi zangu kwa familia ya Mhe. Teiyaa. Tulikuwa naye katika Bunga la Kumi na Mbili. Tulikuwa kwa kamati moja. Alikuwa mtu mzuri. Natoa pole kwa familia. Mungu aiwezeshe kujaza pengo aliloacha. Asante bwana Spika. view
  • 2 Apr 2025 in National Assembly: Mhe. Spika. Mwanzo nakupongeza kwa kuwatambua wavuvi wa samaki. Ahsante. Wizara iko na mikakati gani ya kuwasaidia wavuvi kuboresha usalama wao? Wavuvi hawajazingatiwa inchini Kenya. Siku tatu zilizopita kule Lamu, boti ilipata shida mbele ya Mkokoni, na wavuvi wakapiga simu na kuomba wasaidiwe. Hawakusaidiwa, na ikabidi waogolee wenyewe wakafika. Chombo kilikuwa kimebeba mizigo mingi na mawimbi yakaja yakakizamisha. Ingekuwa rahisi wangefikiwa kwa haraka kwa maana si mbali na kambi nyingi za forces zilizoko katika eneo lile. Ni mikakati tuu haijapangwa. Tafadhali Waziri, hao wavuvi ni Wakenya, na wanachangia pakubwa uchumi wa nchi hii. The electronic version of the Official Hansard ... view
  • 2 Apr 2025 in National Assembly: Hon. Spika, utanisaidia. Sijui niseme suala hili ni la kitengo cha usalama, ama kile cha utumishi au Blue Economy . Lakini hawa ni Wakenya, na inafaa watafutiwe njia wasaidike. view
  • 2 Apr 2025 in National Assembly: ziwekwe. Ahsante. view
  • 2 Apr 2025 in National Assembly: Mhe. Spika, Lamu inajulikana kwa kutegemea sana utalii. Tunauza samaki sana katika eneo Bunge langu la Lamu Mashariki. Kwa hivyo, watalii wakiathirika kidogo tu, sisi pia tunaathirika. Nataka Waziri aliambie Bunge hili ni kitu gani kilitokea Mangai, ambapo Chifu alitafutwa na Al-Shabaab. Kuna Gavana aliyesema kwa jambo la vitambulisho kuwa ni vibaya watu wa Lamu wasifanyiwe vetting kwa sababu Al-Shabaab wanaingia nchini. Kwa hivyo mimi na watu wangu tuna wasiwasi hao watu wasifanye kusudi to justify their point . Kwa hivyo, Waziri atuambie ni nani alihusika kumtafuta Chifu Mangai. Kama ni Al-Shabaab utuambie, maanake walikuja kwa njia tofauti kabisa. Eti ... view
  • 2 Apr 2025 in National Assembly: Ahsante, Mhe. Spika wa Muda, kwa kunipatia nafasi hii ya kuzungumzia Hoja hii ya kutengeneza mbolea hapa nchini kwetu. Ninataka kumpongeza Mhe. Atandi kwa kuleta Hoja hii. Hoja hii itawasaidia wakulima kuhakikikisha kuwa mbolea inapatikana kwa wingi na kwa urahisi. Mazao pia yatapatikana kwa wingi ikiwa mbolea itatengenezwa hapa Kenya. Vijana wetu watapata kazi kwa sababu kampuni hizo au viwanda hivyo vikiwa hapa, vitaajiri watu. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 2 Apr 2025 in National Assembly: Tuseme ukweli. Tusiwe wezi wa fadhila. Kitu kizuri kikifanywa, tuseme kimefanywa vizuri au kiboreshwe. Tusikatae kusema kuwa mtu amefanya jambo nzuri kwa sababu ya siasa. Rais wetu na Naibu wake wamejaribu. Ruzuku ama subsidy inayowekwa kwenye mbolea ili isiwe ghali haikuanza na Rais huyu wala Serikali hii. Ilianza na Serikali iliyopita. Hawa nao wamejaribu kuhakikisha kuwa mbolea inapatikana kwa bei nzuri lakini kuna haja ya kuzidisha bidii ili mbolea ipatikane kwa urahisi zaidi. view
  • 2 Apr 2025 in National Assembly: My Question has not been answered. It is about the ETA. It affects tourism. The issue of Al-Shabaab in Mangai affects tourism not only in Lamu but also in Kenya. We are really affected. We want to know the root cause of this. Who is involved? Is it Al-Shabaab, or who is it? view
  • 19 Feb 2025 in National Assembly: Ahsante, Mhe. Naibu wa Spika, kwa kunipatia nafasi hii ya kuchangia Mswada huu. Mswada huu wa mfuko wa kusawazisha utahakikisha kuwa yale maeneo bunge yaliyokuwa chini yatainuliwa yawe sawa na mengine. Sheria hii inavyopangiwa itasaidia sana. Hapo awali, mfuko huo ulikuwa na pesa lakini hapakuwa na sheria, kwa hivyo pesa zilifujwa. Sheria hii itatusaidia ili mambo yafunguke na maeneo yetu yawe kama maeneo bunge mengine. Usimamizi wa pesa hizo ni muhimu. Ninaweza toa mifano. Mara ya kwanza pesa zilipotoka, Eneo bunge langu lilipata Ksh120,000,000 zilizotumika kutengeneza barabara ya kokoto inayoitwa Mtangawanda-Kizingitini. Kulikuwa na kampuni inayoitwa Zarara Oil and Gas Company ... view
  • 19 Feb 2025 in National Assembly: . Lakini ukweli wa mambo ni kuwa pesa hizo zilifujwa. Cha kusikitisha ni kuwa kwa sababu barabara ni ya kokoto, haikufuatiliwa kwa sababu wangesema kuwa mvua ilinyesha na kwa hivyo pesa zilitumika. Ningependa kutoa pendekezo kuwa pesa hizo zisitumike kujenga barabara za udongo. Zitumike kujenga barabara ya lami, hata kama ni kilomita moja, kuliko kutumika kwa njia ambazo mtu anaweza jificha nazo azimalize. Pesa hizi ni za maskini. Watu wanasahau kuwa pesa za maskini zikiliwa, humrudia mtu. Kama pesa hizi zingetumika kwetu, tungekuwa mbele sana na tungekuwa tunatumia hizi pesa zingine kusonga mbele zaidi. Kwa mfano, watu wa Mangai walio ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus