22 May 2013 in National Assembly:
Ni maskitiko makubwa kwamba ndugu zetu wavuvi wana ujuzi kamili wa kuwawezesha kuifanya kazi hiyo lakini hawajapata usaidizi kikamilifu kutoka kwa Serikali yetu kama walivyosaidiwa Wakenya kwenye sekta ya kilimo na sekta nyinginezo. Hivi sasa, samaki wanatoka sehemu ya Lamu na kupelekwa kuuzwa Mombasa. Kuna sehemu inayoitwa Majengo. Huko ndiko wanakouzwa samaki hao â
view
15 May 2013 in National Assembly:
Ahsante Mhe. Spika wa Muda. Kwanza, ninataka kumshukuru ndugu yangu, Mheshimiwa aliyeleta Hoja hii hapa. Tunafahamu vyema kwamba wazee wetu ni watu ambao wanahitaji kuzingatiwa sana. Hii ni kwa sababu hatungefika hapa leo au hatungefikisha umri huu bila wazee wetu. Hata sisi tutakuwa wazee.
view
15 May 2013 in National Assembly:
Ahsante Mhe. Spika wa Muda. Kwanza, ninataka kumshukuru ndugu yangu, Mheshimiwa aliyeleta Hoja hii hapa. Tunafahamu vyema kwamba wazee wetu ni watu ambao wanahitaji kuzingatiwa sana. Hii ni kwa sababu hatungefika hapa leo au hatungefikisha umri huu bila wazee wetu. Hata sisi tutakuwa wazee.
view
15 May 2013 in National Assembly:
Hoja hii inafuatana na Katiba yetu ambayo tuliipitisha kwa kusema kwamba tutawasimamia na kuwasaidia wazee. Jambo hili liko katika Kipengee cha 57 cha Katiba ya Kenya. Kipengee hiki kinasema: âThe State shall take measures to ensure the rights of older persons.â Kipengee cha 57(d) kinasema: âto receive reasonable care and assistance from their family and the State.â
view
15 May 2013 in National Assembly:
Hoja hii inafuatana na Katiba yetu ambayo tuliipitisha kwa kusema kwamba tutawasimamia na kuwasaidia wazee. Jambo hili liko katika Kipengee cha 57 cha Katiba ya Kenya. Kipengee hiki kinasema: âThe State shall take measures to ensure the rights of older persons.â Kipengee cha 57(d) kinasema: âto receive reasonable care and assistance from their family and the State.â
view
15 May 2013 in National Assembly:
Mheshimiwa ameelezea usaidizi ambao wazee wetu wanaweza kupata. Moja ni kuwa wazee wa umri wa miaka 60 na zaidi wahudumiwe katika hospitali zetu bila malipo yoyote. Hii ni kwa sababu mzee ataenda hospitalini, aambiwe alipe shilingi mia mbili na hajui atoe hizo pesa wapi. Ningeomba tulizingatie suala hili sana.
view
15 May 2013 in National Assembly:
Mheshimiwa ameelezea usaidizi ambao wazee wetu wanaweza kupata. Moja ni kuwa wazee wa umri wa miaka 60 na zaidi wahudumiwe katika hospitali zetu bila malipo yoyote. Hii ni kwa sababu mzee ataenda hospitalini, aambiwe alipe shilingi mia mbili na hajui atoe hizo pesa wapi. Ningeomba tulizingatie suala hili sana.
view
15 May 2013 in National Assembly:
Vile vile, zile Kshs.4,000 ambazo Serikali inawapatia wazee, itakuwa vyema kama tutahakikisha kwamba zinamfikia kila mzee popote alipo. Hii ni kwa sababu
view
15 May 2013 in National Assembly:
Vile vile, zile Kshs.4,000 ambazo Serikali inawapatia wazee, itakuwa vyema kama tutahakikisha kwamba zinamfikia kila mzee popote alipo. Hii ni kwa sababu
view
9 May 2013 in National Assembly:
.: Asante, mhe. Mwenyekiti. Nataka niseme kwamba kuunga mkono
view
24 Apr 2013 in National Assembly:
Asante Naibu Spika. Ninaitwa Shariff Athman Ali. Ningependa kuchukua fursa hii kukupongeza wewe pamoja na Spika kwa kuchaguliwa katika nafasi zenu. Vile vile, ninataka kuchukua fursa hii kuwashukuru watu wa Lamu Mashariki kwa kunichagua kuwawakilisha katika Bunge hili la kumi na moja. Kulingana na Hotuba ya Rais iliyotolewa hapa wiki iliyopita, kwa kweli, ni Hotuba ya kupendeza. Kama unavyosikia Wabunge wenzangu--- Kila anayeinuka anaipendekeza Hotuba hii. Lakini ajabu kubwa iliyoko ni kwamba mpaka dakika hii yote yaliyozungumziwa--- Bali na kwamba Rais mstaafu Mwai Kibaki alianzisha CDF bado malalamiko mashinani yako. Vijana wanasoma chini ya miti. Hayo ni masikitiko makubwa na ...
view
24 Apr 2013 in National Assembly:
Ukiangalia maswala ya ardhi, mpaka hivi sasa hili ni tatizo kubwa, na limezungumziwa na wapwani wenzangu. Swala hili linaihusu Lamu pia. Ningependa jambo hili lichukuliwe kwa uzito sana ili tusionekana kama ni nyimbo twaimba, ama ni hadithi tunatoa. Ni lazima tuonyeshe uzito wa maswala haya. Ni masikitiko na aibu kubwa katika nchi hii kuwa baada ya miaka 50 ya Uhuru, ama utawala wetu, bado kuna Wakenya ambao hawana maji, na kuna vijana ambao wanasomea chini ya miti kwa sababu hawana madarasa. Haya ni maswala ambayo ni lazima tuyape kipaumbele na kuyazingatia vilivyo. Kinachostahili hapa ni kuhakisha kwamba haya mambo yametekelezwa ...
view