Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 21 to 30 of 512.

  • 19 Feb 2025 in National Assembly: Tukizungumzia kuhusu pesa hizi, kila mtu anafikiria ubinafsi. Ukweli ni kuwa wale wanaoishi kule kwingine ni ndugu zenyu. Kama vile pesa zinawekwa katika miradi ya chai au kahawa, msikasirike zikiwekwa huko kwingine. Sisi hatukasiriki kwa sababu hatuna chai kwa hivyo hatuwezi lilia pesa hizo. Pesa za marginalisation ni za kurekebisha makosa yaliyotokea katika serikali zote zilizopita. Hiyo sio pendeleo tunafanyiwa. Ninamshukuru Rais kwa sababu tangu aingie mamlakani miaka miwili iliyopita, amefanya zaidi ya pesa zilizowekwa. Ukihesabu faida ya pesa hizi, hazilingani na alichofanya. Kwa mfano, Rais anaweka lami kilomita 15 katika barabara ambayo pesa za Equalisation Fund zilifanyiwa ubadhirifu. Mbona ... view
  • 19 Feb 2025 in National Assembly: na anafanya kazi. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 19 Feb 2025 in National Assembly: Watu katika maeneo bunge yetu wanataka tumaini. Roho zao zilikuwa zimekata tamaa na hawakuwa na tumaini katika Kenya. Rais wetu ametupa tumaini. Watoto wetu wana tumaini kuwa barabara zitajengwa. Leo tumetia sahihi katika mkataba wa kihistoria. Kutoka mwanzo wa dunia, kati ya vijiji vyangu ishirini na tatu, vijiji kumi na mbili pekee vina stima. Saa hii, tumetia sahihi mkataba katika vijiji vitatu, yaani, Ndau, Kiwayu na Mkokoni ili ziwekwe mini grid za solar . Jambo hilo limenifanya niwe very emotional. Karibu nilie katika mkutano huo. Watu wangu na watoto wao hawajawahi ona stima kwa miaka hii yote ilhali tumekuwa tukifanya ... view
  • 19 Feb 2025 in National Assembly: Ninasisitiza tena na tena kuwa pesa za Equalisation Fund zikipelekwa kule, magavana walio na mifuko mikubwa ya kufanya kazi wanachukua hizo pesa chache na kuziweka katika ugatuzi ili Serikali kuu ionekane ni kama haifanyi kazi. Hizo ni pesa chache sana. Kwa mfano, nimebaki na million ishirini na nne ninazopaswa kugawanya katika eneo bunge langu lote. Kwa hivyo, sheria iwekwe, tugawane majukumu, na ijulikane kuwa kaunti inafanya nini na Serikali kuu inafanya nini ili watu wote wasaidike na kusiwe na mizozo. view
  • 11 Feb 2025 in National Assembly: Ahsante Mhe. Spika. Tunaheshimu uamuzi wa korti lakini hatukubaliani nao. Mwanzo, sisi kama Jubilee Party, tulikuwa tushaenda. Hatuko kwa Azimio la Umoja-One Kenya Coalition Party. Ukiangalia Mawaziri wale tuko nao saa hii, ambao walipeleka haya mambo kortini, Mhe. Wandayi na Mhe. Mbadi, saa hii wako kwenye hii Serikali. Kwani hao mahakimu hawaoni mambo yamepita na yameendelea? Kwani wanaishi Kenya gani? Sasa huku ni kuleta taharuki. Sisi hatuna haja nayo. Serikali hii imepitia changamoto kubwa na nyingi. Kwa hivyo, tafadhali, tunaomba watupatie nafasi tuendelee. Kuna jambo kuhusu ofisi ya Mhe. Spika. Katiba haijasema Jambo kulihusu na imenyamaza. Hii yamaanisha inaruhusiwa. Haina ... view
  • 16 Jan 2025 in National Assembly: Asante Mhe. Spika kwa kunipatia nafasi nipate kuchangia. Moja kwa moja, ninaunga mkono. Ninataka niwaambie kwamba na iwe vile ambavyo wamesema kwenye Kamati; siyo kusema tu kwa mdomo, bali waseme kwa vitendo. Kuna wakati Ministry ya Information, Communication and Digital Economy ilitoa nafasi kwa vijana wawili katika kila kaunti, lakini kaunti zingine hazikupewa hizo nafasi. Utaona hata zile zetu mbili zinapewa watu wengine. Kwa hivyo, Waziri akifika hapo, aangalie Kenya yote. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 16 Jan 2025 in National Assembly: Asiache Mkenya yeyote nje. Sisi ni Wakenya pia. Kule kwetu Lamu ni mbali na kidogo tunasahaulika. Kwa hivyo, atuzingatie na atumie ile affirmative action kufikiria na kusaidia watu walio sehemu mbali mbali. Si lazima Lamu pekee, lakini Wakenya wote kwa jumla. Ningependa pia kumwambia Waziri wa Kilimo na Mifugo kwamba masuala ya samaki yako kwenye kilimo pia. Asiangalie tu upande wa kulima mimea pekee, bali pia aangalie mifugo na samaki. Aje na mbinu za kisasa zile ambazo zitatusaidia. Tusibaki kwenye hali ya babu zetu ambao walienda kuvua samaki na kupata pengine kilo ishirini tu. Saa hii, watu wanapoenda kuvua wanapata ... view
  • 16 Jan 2025 in National Assembly: Mbali na hayo, eneo ninaloliwakilisha, Lamu Mashariki, lina pande nyingi zenye manufaa. Kuna upande wa samaki, na upande mwingine ni wakulima wa simsim na view
  • 16 Jan 2025 in National Assembly: . Kuna mfadhili mmoja alisaidia hivi karibuni kwa kutoa laki tano akakipa kikundi cha youth . Hizo laki tano zilitoa watermelon mpaka tukashindwa kuuza. Watermelon zilikuwa nyingi sana. Kuna haja ya Waziri kuingia kule na kuangalia maeneo gani yatatoa mazao gani ili tuweze kusaidia watu wetu. Itakuwa ni kuinua uchumi wa Kenya. view
  • 16 Jan 2025 in National Assembly: Pia, kuna ukulima wa ndimu na mihogo, lakini bado tunategemea mbinu za zamani. Hawatusaidii. Ningependa kumwambia Waziri kwamba sisi ndio tunatoa simsim nzuri. Ajue kwamba akiingia, kazi inamngojea pale mezani. Ajue kwamba kule Lamu Mashariki, simsim iko nyingi, lakini haiuziki kwa sababu ya makosa ya watu wengine. Wao walitumia dawa inaitwa kausha, wakakausha mimea na sasa simsim yetu haiwezi kuuzwa kule uzunguni. Haiwezi kwenda. Kwa hivyo, aje afanye tofauti na hivyo. Wale wanaotumia madawa wasipeleke bidhaa zao, lakini wale ambao hawatumii madawa bidhaa zao ziweze kupelekwa. Simtarajii aseme kwamba nizungumze na kaunti… view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus