Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 21 to 30 of 515.

  • 2 Apr 2025 in National Assembly: My Question has not been answered. It is about the ETA. It affects tourism. The issue of Al-Shabaab in Mangai affects tourism not only in Lamu but also in Kenya. We are really affected. We want to know the root cause of this. Who is involved? Is it Al-Shabaab, or who is it? view
  • 19 Feb 2025 in National Assembly: Ahsante, Mhe. Naibu wa Spika, kwa kunipatia nafasi hii ya kuchangia Mswada huu. Mswada huu wa mfuko wa kusawazisha utahakikisha kuwa yale maeneo bunge yaliyokuwa chini yatainuliwa yawe sawa na mengine. Sheria hii inavyopangiwa itasaidia sana. Hapo awali, mfuko huo ulikuwa na pesa lakini hapakuwa na sheria, kwa hivyo pesa zilifujwa. Sheria hii itatusaidia ili mambo yafunguke na maeneo yetu yawe kama maeneo bunge mengine. Usimamizi wa pesa hizo ni muhimu. Ninaweza toa mifano. Mara ya kwanza pesa zilipotoka, Eneo bunge langu lilipata Ksh120,000,000 zilizotumika kutengeneza barabara ya kokoto inayoitwa Mtangawanda-Kizingitini. Kulikuwa na kampuni inayoitwa Zarara Oil and Gas Company ... view
  • 19 Feb 2025 in National Assembly: . Lakini ukweli wa mambo ni kuwa pesa hizo zilifujwa. Cha kusikitisha ni kuwa kwa sababu barabara ni ya kokoto, haikufuatiliwa kwa sababu wangesema kuwa mvua ilinyesha na kwa hivyo pesa zilitumika. Ningependa kutoa pendekezo kuwa pesa hizo zisitumike kujenga barabara za udongo. Zitumike kujenga barabara ya lami, hata kama ni kilomita moja, kuliko kutumika kwa njia ambazo mtu anaweza jificha nazo azimalize. Pesa hizi ni za maskini. Watu wanasahau kuwa pesa za maskini zikiliwa, humrudia mtu. Kama pesa hizi zingetumika kwetu, tungekuwa mbele sana na tungekuwa tunatumia hizi pesa zingine kusonga mbele zaidi. Kwa mfano, watu wa Mangai walio ... view
  • 19 Feb 2025 in National Assembly: Tukizungumzia kuhusu pesa hizi, kila mtu anafikiria ubinafsi. Ukweli ni kuwa wale wanaoishi kule kwingine ni ndugu zenyu. Kama vile pesa zinawekwa katika miradi ya chai au kahawa, msikasirike zikiwekwa huko kwingine. Sisi hatukasiriki kwa sababu hatuna chai kwa hivyo hatuwezi lilia pesa hizo. Pesa za marginalisation ni za kurekebisha makosa yaliyotokea katika serikali zote zilizopita. Hiyo sio pendeleo tunafanyiwa. Ninamshukuru Rais kwa sababu tangu aingie mamlakani miaka miwili iliyopita, amefanya zaidi ya pesa zilizowekwa. Ukihesabu faida ya pesa hizi, hazilingani na alichofanya. Kwa mfano, Rais anaweka lami kilomita 15 katika barabara ambayo pesa za Equalisation Fund zilifanyiwa ubadhirifu. Mbona ... view
  • 19 Feb 2025 in National Assembly: na anafanya kazi. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 19 Feb 2025 in National Assembly: Watu katika maeneo bunge yetu wanataka tumaini. Roho zao zilikuwa zimekata tamaa na hawakuwa na tumaini katika Kenya. Rais wetu ametupa tumaini. Watoto wetu wana tumaini kuwa barabara zitajengwa. Leo tumetia sahihi katika mkataba wa kihistoria. Kutoka mwanzo wa dunia, kati ya vijiji vyangu ishirini na tatu, vijiji kumi na mbili pekee vina stima. Saa hii, tumetia sahihi mkataba katika vijiji vitatu, yaani, Ndau, Kiwayu na Mkokoni ili ziwekwe mini grid za solar . Jambo hilo limenifanya niwe very emotional. Karibu nilie katika mkutano huo. Watu wangu na watoto wao hawajawahi ona stima kwa miaka hii yote ilhali tumekuwa tukifanya ... view
  • 19 Feb 2025 in National Assembly: Ninasisitiza tena na tena kuwa pesa za Equalisation Fund zikipelekwa kule, magavana walio na mifuko mikubwa ya kufanya kazi wanachukua hizo pesa chache na kuziweka katika ugatuzi ili Serikali kuu ionekane ni kama haifanyi kazi. Hizo ni pesa chache sana. Kwa mfano, nimebaki na million ishirini na nne ninazopaswa kugawanya katika eneo bunge langu lote. Kwa hivyo, sheria iwekwe, tugawane majukumu, na ijulikane kuwa kaunti inafanya nini na Serikali kuu inafanya nini ili watu wote wasaidike na kusiwe na mizozo. view
  • 11 Feb 2025 in National Assembly: Ahsante Mhe. Spika. Tunaheshimu uamuzi wa korti lakini hatukubaliani nao. Mwanzo, sisi kama Jubilee Party, tulikuwa tushaenda. Hatuko kwa Azimio la Umoja-One Kenya Coalition Party. Ukiangalia Mawaziri wale tuko nao saa hii, ambao walipeleka haya mambo kortini, Mhe. Wandayi na Mhe. Mbadi, saa hii wako kwenye hii Serikali. Kwani hao mahakimu hawaoni mambo yamepita na yameendelea? Kwani wanaishi Kenya gani? Sasa huku ni kuleta taharuki. Sisi hatuna haja nayo. Serikali hii imepitia changamoto kubwa na nyingi. Kwa hivyo, tafadhali, tunaomba watupatie nafasi tuendelee. Kuna jambo kuhusu ofisi ya Mhe. Spika. Katiba haijasema Jambo kulihusu na imenyamaza. Hii yamaanisha inaruhusiwa. Haina ... view
  • 16 Jan 2025 in National Assembly: Asante Mhe. Spika kwa kunipatia nafasi nipate kuchangia. Moja kwa moja, ninaunga mkono. Ninataka niwaambie kwamba na iwe vile ambavyo wamesema kwenye Kamati; siyo kusema tu kwa mdomo, bali waseme kwa vitendo. Kuna wakati Ministry ya Information, Communication and Digital Economy ilitoa nafasi kwa vijana wawili katika kila kaunti, lakini kaunti zingine hazikupewa hizo nafasi. Utaona hata zile zetu mbili zinapewa watu wengine. Kwa hivyo, Waziri akifika hapo, aangalie Kenya yote. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 16 Jan 2025 in National Assembly: Asiache Mkenya yeyote nje. Sisi ni Wakenya pia. Kule kwetu Lamu ni mbali na kidogo tunasahaulika. Kwa hivyo, atuzingatie na atumie ile affirmative action kufikiria na kusaidia watu walio sehemu mbali mbali. Si lazima Lamu pekee, lakini Wakenya wote kwa jumla. Ningependa pia kumwambia Waziri wa Kilimo na Mifugo kwamba masuala ya samaki yako kwenye kilimo pia. Asiangalie tu upande wa kulima mimea pekee, bali pia aangalie mifugo na samaki. Aje na mbinu za kisasa zile ambazo zitatusaidia. Tusibaki kwenye hali ya babu zetu ambao walienda kuvua samaki na kupata pengine kilo ishirini tu. Saa hii, watu wanapoenda kuvua wanapata ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus