16 Jan 2025 in National Assembly:
Mbali na hayo, eneo ninaloliwakilisha, Lamu Mashariki, lina pande nyingi zenye manufaa. Kuna upande wa samaki, na upande mwingine ni wakulima wa simsim na
view
16 Jan 2025 in National Assembly:
. Kuna mfadhili mmoja alisaidia hivi karibuni kwa kutoa laki tano akakipa kikundi cha youth . Hizo laki tano zilitoa watermelon mpaka tukashindwa kuuza. Watermelon zilikuwa nyingi sana. Kuna haja ya Waziri kuingia kule na kuangalia maeneo gani yatatoa mazao gani ili tuweze kusaidia watu wetu. Itakuwa ni kuinua uchumi wa Kenya.
view
16 Jan 2025 in National Assembly:
Pia, kuna ukulima wa ndimu na mihogo, lakini bado tunategemea mbinu za zamani. Hawatusaidii. Ningependa kumwambia Waziri kwamba sisi ndio tunatoa simsim nzuri. Ajue kwamba akiingia, kazi inamngojea pale mezani. Ajue kwamba kule Lamu Mashariki, simsim iko nyingi, lakini haiuziki kwa sababu ya makosa ya watu wengine. Wao walitumia dawa inaitwa kausha, wakakausha mimea na sasa simsim yetu haiwezi kuuzwa kule uzunguni. Haiwezi kwenda. Kwa hivyo, aje afanye tofauti na hivyo. Wale wanaotumia madawa wasipeleke bidhaa zao, lakini wale ambao hawatumii madawa bidhaa zao ziweze kupelekwa. Simtarajii aseme kwamba nizungumze na kaunti…
view
27 Nov 2024 in National Assembly:
Ahsante, Mhe. Spika wa Muda. Nataka niafikiane na wenzangu katika Hoja hii. Nawaunga mkono wale waliochaguliwa. Kusema kweli, Mhe. Jaldesa atakuwa katika mstari wa mbele kwa sababu tunamjua. Alipokuwa WomanRepresentative, alifanya bidii sana katika kuzingatia mambo ya wanawake. Kwa hivyo, anajua kile kinachotakikana. Nataka kuwaomba wale waliochaguliwa wasikae tu kwa ma -boardroom . Watembee. Watuonyeshe kuwa watahakikisha wanawake wamechaguliwa zaidi kama
view
27 Nov 2024 in National Assembly:
, Members of Parliament na Members of County Assemblies (MCAs).
view
27 Nov 2024 in National Assembly:
The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor.
view
27 Nov 2024 in National Assembly:
Nimemsikia mmoja wa Wabunge wanaume wenzangu akisema kuwa wanaume pia wapewe kipaumbele, hususan boy-child . Sikatai lakini kwa sasa, kulingana na mambo ya
view
27 Nov 2024 in National Assembly:
, yule ambaye ni mnyonge kidogo ni mwanamke. Kuna maneno tuliyoyasikia kwenye mtandao, na nimemsikia Leader of the Majority
view
27 Nov 2024 in National Assembly:
akiwatetea wanawake. Imesemekana kuwa ni uongo na mtu huyo hakusema matusi hayo. Basi mtu huyo angejitokeza na kusema kuwa maneno hayo hayakuwa yake na ni propaganda tu . Lakini propaganda hiyo inayowalenga wanawake ikiendelea, mtatufanya tuzungumze ilhali hatutaki kuzungumza. Kila mtu ana maumbile yake. Ikiwa mwanamke anaweza kuyatumia, hata mwanaume anaweza kuyatumia. Nikisema kile ninachotaka kusema, mtasema ninaongea vibaya. Lakini ni kwa nini mwanamke haambiwi maneno hayo mpaka aamue kusimama kuwa kiongozi? Akiwa daktari, hamna shida.
view
27 Nov 2024 in National Assembly:
Sijataja jina la mtu hapa. Kama mtu anaona kofia inamtosha na akaivaa, hiyo ni stori yake. Sijataja jina la mtu.
view