Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 11 to 20 of 2263.

  • 3 Apr 2025 in Senate: Kitu ambacho ningependa kusisitiza ni kuwa tunataka kama Wakenya tupate kazi safi. Ni matumaini yetu kuwa wale watu watakaochaguliwa watatimiza wajibu wao na kufanya kazi vilivyo. Vile vile, tunajua watu ambao wanakuwa interviewed wanatoka sehemu mbalimbali za Kenya. Hii sio kazi ambayo unaweza kuketi na kuchagua watu. Tunataka kuona katika muda wanaouhitaji ili kumaliza kazi hii, watachukua watu kutoka upande zote za Kenya. Ni jambo kubwa ama jambo lililo na mzigo mkubwa katika muda huu ambao wameuliza. Kwa hivyo, mimi nataka kuunga mkono ya kuwa ni sawa wakiongezewa siku hizi 14 ambazo wameuliza. Ikiwa wamemaliza zile siku zao 90 kulingana ... view
  • 3 Apr 2025 in Senate: Sio haki kijana kama Cherarkey kuongea ninapoongea. Bila kuchukua wakati zaidi, naunga mkono Hoja hii kwa dhati. view
  • 1 Apr 2025 in Senate: Asante, Bi. Spika wa Muda. Ninataka kuchangia hii Kauli ambayo imeletwa na ndugu yangu, Sen. Omogeni. Hili ni jambo ya kusikitisha sana. Katika Kaunti ya Nyamira, kuna watu ambao wamesoma; kuna watu ambao wanaelewa kunaendelea namna gani. Kwa hivi sasa, tunaona aibu tupu ambayo huyu Gavana Amos Nyaribo ameleta ndani ya Kaunti ya Nyamira. Haiwezekani kuwe na County Assembly mbili ikiwa wewe ni gavana mmoja pale. Ni matusi kwa watu wa Kaunti ya Nyamira kufanyiwa namna hii. Juzi, alituambia ya kwamba yeye hajui ni county assembly gani ambayo iko na mamlaka zaidi ya nyingine. Lakini ikifika wakati wa kutambua pale ... view
  • 1 Apr 2025 in Senate: Tafadhali, nipe dakika mbili kwa sababu ninataka kumaliza. view
  • 1 Apr 2025 in Senate: Ninasema hivi; tafadhali gavana afanye heshima na watu wa Nyamira ili aweze kuleta mwelekeo vile county assembly itaendelea. Hatuwezi kukubali kuwa na Spika wawili, clerks wawili na hata kila mahali watu wawili wawili. Je, hao watu wanalipwa aje? Ninakubaliana na Kiongozi wa Walio Wengi, Sen. Cheruiyot, akisema kwamba makosa haya yanaletwa na mtu mmoja ambaye yuko na interest hapo, ambaye anapaswa kutuambia. Huyo mtu ambaye ni Controller of Budget, ikiwezekana, pia yeye tumuite aje katika Seneti ili tumhoji. Asante. view
  • 1 Apr 2025 in Senate: Asante, Bi. Spika wa Muda, kwa kunipa nafasi hii. Kwanza, naunga mkono yote ambayo ndugu yangu ambaye ni Kiongozi wa Wengi amesema kuhusu Mswada Huu. Hii ni sheria ambayo itatupa nafasi ya kufungua ukurusa mwingine ili watu wasaidike wakati kuna janga. Hii ni mojawapo ya Miswada ambayo si ya kawaida lakini inaweza kutupatia mamlaka. Wahenga walisema kuwa fimbo ya karibu ndio huua nyoka. Hii inamaanisha kuwa kitu ulichonacho ndicho hukusaidia wakati una shida fulani. Sisi tulikuwa katika shida kubwa na ilikuwa lazima tuepukane na shida hiyo. Kwa hivyo, ni lazima tuwe na sheria ambayo itatusaidia kutoka katika janga hilo. Ndio ... view
  • 1 Apr 2025 in Senate: The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate. view
  • 1 Apr 2025 in Senate: Huu ulikuwa mojawapo ya misemo iliyotumika katika NADCO. Watu walikuja pamoja na kupendekeza sheria hiyo. Tukiwa katika shida ama janga lolote la kisiasa, ni lazima watu wakae ili tupate suluhisho. Hii ni mojawapo ya sheria ambazo zilipendekezwa. Naunga mkono Mswada huu kwa sababu unaweza kupeana uhai kwa jopo ili sheria ambayo inaweza kutumika wakati wa dharura itengenezwe. Majukumu kama hayo ni muhimu sana. Ikiwa watu wanaopatikana katika hali hiyo wanaweza kutafakari na kutoa majukumu kabla ya janga kutokea, hiyo itakuwa njia nzuri. Sheria endelevu kama hii ambayo inapendekezwa inafaa kuwa. Ikiwa itaweza kutekelezwa, basi, kutakuwa na adhabu ikiwa mtu hatafanya ... view
  • 19 Mar 2025 in Senate: Asante, Bw. Spika. Naomba uweze kunitetea kutokana na watu ambao wananiingilia wakati nimesimama. view
  • 19 Mar 2025 in Senate: Bw. Spika, nataka kuunga mkono Taarifa iliyotolewa hapa na ndugu yetu Sen. (Prof.) Tom Ojienda wa Kisumu. Ni kweli kwamba hapa Kenya, hususan pande za Kisumu na maeneo ya Nyando, hutatizwa sana na mafuriko. Zaidi sana wananchi hupoteza maisha yao. Bw. Spika, tukizingatia vile vile hali ya mafuriko, wakati wa mvua ukifika hakuna hata siku moja tumeweza kuona Serikali yetu ya Kenya Kwanza ikiweka kipaumbele mambo ya mafuriko. Kitu tunaona tu ni kwamba wananchi wengi wanasombwa na maji wakati wa mafuriko, wengine wanafariki na hata wengine kutolewa katika maeneo ambayo yako chini kule walikoweza kujisitiri kiamaisha kama nyumbani The electronic ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus