Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 11 to 20 of 1944.

  • 19 Sep 2023 in Senate: Badala ya kutetea watu katika maeneo kama yale, sasa hivi Serikali inagongana wenyewe kwa wenyewe. Mawaziri wanaongea tofauti. Pia, yule Economic Advisor naye anaongea vile. Sasa unashindwa, je, watachukuwa wakati gani kuangalia zile sehemu zinaendelea namna gani kwa usalama. Wakiwa kitu kimoja, wataona ya kwamba maisha ya watu wa Lamu yameweza kutetewa vilivyo. Hivi sasa, tuko katika hali ya kupigana na hali ya uchumi. Kule kwingine watu wanakufa. Watu hawana chakula na inafaa wapelekewe chakula katika maeneo ambayo yako na shida zaidi kama vile Lamu. Ni sehemu ambayo iko n a shida nyingi na inatakiwa msaada upelekwe kule. Lakini, hivi ... view
  • 31 Aug 2023 in Senate: Asante, Bw. Spika. Kitu cha kwanza ni, naunga mkono Mswada huu wa mabadiliko ya hali ya hewa, au kwa Kiswahili sanifu, mabadiliko ya tabianchi. Kwa mara ya kwanza nimejipata nikiona tabianchi au climate change kwa Kamusi lakini, hali ya hewa ni mojawapo. Bw. Spika, cha muhimu ni kuona ya kwamba tumezingatia swali hili katika nchi yetu. Hii tabia ya nchi inaweza kuangaliwa vizuri ikiwa sisi sote tutajumuika kama Wakenya na kuona tumepanda miti ambayo itaweza kulinda mazingira. Ninatoka sehemu za Kaunti ya Kilifi. Mara nyingi ukienda pande za ufuoni wa bahari, utapata sio kukata miti pekee yake katika ardhi lakini ... view
  • 31 Aug 2023 in Senate: Tukiwa katika mazungumzo hayo wiki ijayo, ni muhimu kuonyesha ya kwamba Kenya iko katika kipao mbele. La muhimu katika hii mabadiliko ya tabia ya nchi ni kwamba sisi pia lazima tuone baada ya kupanda hii miti, tutailinda. Huwezi kupanda miti pekee yake bila kuilinda. Tuko na makabila mengi kama alivyotaja ndugu yangu. Kule ninakotoka, kuna kabila la Warta. Hilo ni kabila ambalo limeishi na linalinda misitu. Watu kama hawa ni lazima ikiwa kutatoka pesa zozote, wapewe nafasi hiyo. Bw. Spika, nikimalizia, dakika moja tu. Kunao umuhimu kuona ya kwamba watu wanaoishi katika hiyo miti ndio watapewa--- view
  • 31 Aug 2023 in Senate: I second. Thank you. view
  • 31 Aug 2023 in Senate: Madam Temporary Speaker, I second. view
  • 29 Aug 2023 in Senate: Asante, Bw. Spika--- view
  • 29 Aug 2023 in Senate: Bw. Spika, kwanza ninaunga mkono Hoja hii iliyoletwa na Kiongozi wa Walio Wengi. Katiba inatueleza kabisa kuwa mamlaka yote ya taifa hili yako katika mikono ya Wakenya. Kwa hivyo wao ndio wenye mamlaka. Sisi tuko hapa kama Bunge kutekeleza yote ambayo Wakenya wanahitaji yatekelezwe katika Bunge hili la Seneti. Mengi yamesemwa. Hata hivyo, Kipengele cha 94 cha Katiba kinasema wazi kwamba Wakenya watawakilishwa Bungeni na wale waliochagua. Tukiwa hapa, tunayo majukumu tofauti. Jukumu letu la kwanza ni kuona--- view
  • 29 Aug 2023 in Senate: Bw. Spika ningependa kusikizwa lakini kuna sauti nyingi zinazotoka upande huo mwingine. view
  • 29 Aug 2023 in Senate: Bw. Spika, tunajua kuna mazungumzo yanayoendelea. Ni lazima yapitishwe katika hili Bunge. Ni muhimu hayo mazungumzo yafaulu ili amani ipatikane nchini. Kulingana na pande zote mbili; Upande wa Walio Wengi na wa Walio Wachache, tunajua wananchi wasio Wabunge walichaguliwa ili wasaidie ile timu ya Bunge. Timu ambayo tulichagua hapa inaongozwa na Wabunge wetu kutoka pande zote mbili. Hawa Wabunge wako na ujuzi na taaluma ya hali ya juu ya kuendesha mazungumzo haya. Vile vile, kuna technical experts ambao wanasaidia hilo kundi. Wao pia wako na taaluma ya juu. Jambo tunalohitaji katika nchi hii ni amani. Bila amani hakuna nchi inayoweza ... view
  • 29 Aug 2023 in Senate: Bw. Spika, nia yetu ni kwamba mazungumzo haya yaweze kufaulu. Tuna imani na timu ambazo tumeziweka hapa mbele. Bibilia inatuambia ya kwamba, pale watu wawili au watatu wako pamoja kuzungumza, ni lazima pawe na amani. Kwa hivyo, sisi tuko na imani na mazungumzo haya na vinara wote kutoka upande huu na ule tuliowachagua. Kuna Viongozi wa Walio Wengi wakiongozwa na mhe. Ichung’wa, na Viongozi wa Walio Wachache wakiongozwa na Mhe. Kalonzo Musyoka. Kwa hivyo, mazungumzo haya yataleta matunda na hatimaye Kenya itaendelea mbele na kupata faida kubwa. Bw. Spika, naunga mkono Mswada huu ili uweze kufaulu. Asante sana. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus