Ali Menza Mbogo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 131 to 140 of 292.

  • 15 Aug 2023 in National Assembly: Sasa, miraa na muguka zinapigwa dawa na kuletwa sokoni. Vijana wetu wengi sasa ni wenda wazimu kwa sababu ya dawa za sumu ambazo wanatumia kila siku. view
  • 15 Aug 2023 in National Assembly: Mheshimiwa Spika wa muda, ninakomea hapo ili nitoe nafasi kwa wenzangu kuchangia Mswada huu. view
  • 15 Aug 2023 in National Assembly: Ninaunga mkono. view
  • 9 Aug 2023 in National Assembly: Asante sana, Mhe. Spika. view
  • 9 Aug 2023 in National Assembly: Ahsante sana, Mhe. Spika, kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la ziada. Waziri wa Masuala ya Ndani na Utawala wa Taifa, tunayo imani na wewe. Tunayo imani utaleta mabadiliko. Umesema usajili wa wanajeshi uko huru, lakini kuna Wakenya ambao wanakatazwa kujiunga na jeshi kwa sababu ya kimo chao na siyo eti ni wagonjwa. Wanavaa viatu na suruali, na wana afya njema lakini wanakataliwa kwa sababu ni wafupi. Ni Mungu amewaumba hivyo. Kwa nini mnawanyima fursa ya kujiunga na jeshi? Kama mnawaona ni wafupi, wanaweza kumfikia adui bila kuonekana. view
  • 9 Aug 2023 in National Assembly: Wachina ni wafupi Zaidi, lakini ni wanajeshi. Kwa nini tunawanyima Wakenya fursa ya kulinda taifa lao? Mhe. Waziri, hili jambo tunafaa tuliangalie kwa makini sana na tusiseme usajili ni huru kama hao tumewaweka nje. Ahsante sana. view
  • 5 Jul 2023 in National Assembly: Asante sana, Mhe. Spika wa Muda. view
  • 5 Jul 2023 in National Assembly: Nashukuru, Mhe. Spika wa Muda, kwa kunipatia nafasi kuuliza swali la ziada. Masuala ya ardhi katika Kisauni ni tatizo sugu. Je, Wizara ina mikakati gani kuyakomboa mashamba ili wananchi waishi kwa amani? Kuna tatizo katika shamba la Ugatuzi, shamba la Kashani na mashamba yaliyoko Junda. Je, mna mikakati gani ya kukomboa ardhi hizo? view
  • 5 Jul 2023 in National Assembly: Mhe. Spika wa Muda, nilikuwa nikieleza swali langu lakini ikawa unazungumza na Mhe. Junet. Sijui kama Waziri alipata swali langu. Waziri, masuala ya ardhi ni sugu Kisauni. Je, Wizara ina mikakati gani ya kukomboa mashamba ili wananchi waishi kwa amani? Shamba la Ugatuzi, shamba la Kashani na mashamba yaliyoko Junda yako na tatizo. view
  • 5 Jul 2023 in National Assembly: On a point of order, Hon. Temporary Speaker. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus