5 Jul 2023 in National Assembly:
Mhe. Spika wa Muda, Waziri hakujibu swali la mikakati walionayo kama Wizara ya kuyakomboa mashamba katika Eneo Bunge la Kisauni. Hakujibu swali hilo, ingawa halikuwa limeandikwa. Akiomba muda ni sawa. Bora nipate jawabu.
view
4 Jul 2023 in National Assembly:
Ahsante sana, Mhe. Spika wa Muda kwa kunipa fursa hii ili niweze kupenyeza sauti yangu.
view
4 Jul 2023 in National Assembly:
Nimesimama kuunga mkono Ripoti hii. Taifa bora ni lile linalolinda mazingira yake. Mazingira ndio chanzo cha matatizo mengi. Mataifa mengi yanarudi nyuma wakati mazingira yanakuwa mabaya. Mazingira yanapokuwa mabaya, maradhi yanagubika taifa hilo. Na badala ya kwenda mbele, linarudi nyuma. Siyo vyema watu katika mataifa mengine ambayo ni ya kitajiri kutupa takataka zao sehemu zetu. Au hata mabaki ambayo wanaona hayawafai na kusema sasa yanakuja kama msaada na kumbe yana madhara.
view
4 Jul 2023 in National Assembly:
Bahari yetu imechafuliwa sana na mataifa yanayojiita ya kitajiri. Licha ya kuwa tuna umaskini, hao ndio wametusababishia umaskini huo kwa njia kama hii ya kutuletea uchafu ambao ni sumu. Tabia hiyo yao inaturudisha nyuma na wao wanatuambia kuwa wanakuja kutupa misaada. Maradhi ya saratani hayakuwa hapa Afrika hapo zamani. Sasa yamezidi mpaka mtoto mdogo anazaliwa na hayo maradhi kwa sababu ya ule uchafu wanaotubwagia. Kule kwao, wanajifanya wanasafisha bahari zao, lakini kwetu ndio wanatumia kama dumping grounds na kusema ni msaada. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can ...
view
4 Jul 2023 in National Assembly:
Taifa linaloheshimika ni lile ambalo linahakikisha kwamba watu wake wanaishi salama. Kuishi salama ni kutokubali kabisa kumwagiwa vitu usivyovijua. Wanatuletea vifaa, kama wanavyosema, vinakuja kama msaada lakini baada ya wiki mbili vinaharibika na tayari vilishatoa miale fulani kwa wale watoto kama ni vya shule. Ni vyema twende na hali yetu wenyewe. Tusijaribu kuomba misaada ambayo itakuja kutudhuru. Hata sisi katika taifa letu, ikiwa ni takataka ambazo ziko katika sehemu ya mji mwingine, zisihamishwe kupelekwa mji mwingine. Zikae pale pale na kama zina madhara, basi zikabiliwe pale na zisiambukize sehemu nyingine.
view
4 Jul 2023 in National Assembly:
Nimesimama kuunga mkono Ripoti hili. Tusikubali hilo licha ya umaskini wetu. Mungu ndiye atakuwa ametupa sisi na ana njia ya kutuhifadhi. Tusikubali kuletewa uchafu kutoka mataifa ya ulaya ama ya kitajiri. Kwa hayo machache, nashukuru na kuipongeza Kamati iliyounda Ripoti hii.
view
6 Jun 2023 in National Assembly:
Asante sana, Mhe. Spika wa Muda, kwa kunipa fursa hii ili niweze kupenyeza sauti yangu. Kwanza, naunga mkono Ripoti hii ya Mhandisi wa Fedha. Pia, naitilia mkazo kwamba…
view
6 Jun 2023 in National Assembly:
Asante, Mhe. Spika wa Muda. Ningependa kutia sauti yangu haswa kwa miradi ya NG-CDF. Ile miradi inayopatikana na inayoonekana katika maeneo yetu sana ni ya NG-CDF. La kusikitisha zaidi ni kwamba hivi sasa, tunakaribia mwaka mwingine na hatujapata hata robo ya pesa. Ni hatari sana kwa sababu hizi ndizo fedha ambazo zilikuwa zinasaidia maskini asiyejiweza. Lakini sasa hana la kufanya kwa sababu ofisi zetu hazina fedha. Hata sisi tumepeana bursaries lakini mpaka sasa, hatujamaliza kupeana za sekondari na vyuo vikuu kwa sababu hakuna fedha.
view
6 Jun 2023 in National Assembly:
Mhe. Spika wa Muda, mijengo mingi ya shule imeanguka. Vyoo vimefurika. Kila siku, ukiuliza unaambiwa shida ni hazina. Tunaenda mwaka mwingine. Sasa tutakua tena kwa
view