Ali Menza Mbogo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 161 to 170 of 295.

  • 19 Apr 2023 in National Assembly: Mhe. Spika wa Muda, sitazungumza mengi zaidi. Nakushukuru kwa kunipatia nafasi. Imebaki siku moja au mbili kufikia sikukuu yetu na nawatakia Waislamu wote sikukuu njema. Mungu awabariki, Insha Allah . view
  • 16 Mar 2023 in National Assembly: Asante sana Mhe. Spika wa Muda kwa kunipa fursa ili nipenyeze sauti yangu. Ningependa kuchukua nafasi kumpongeza Mwenyekiti wa Hazina ya Maeneo Bunge kwa kuleta majina ya maeneo Bunge matatu ili yaweze kupitishwa. Ni vizuri sana yapitishwe kwa sabau kuna shida kubwa sana mashinani. Watoto wengi hawaendi shule kwa sababu hawana karo. Shida zimekuwa nyingi. Kwa hivyo haya maeneo Bunge matatu ambayo majina yao hayajakuja yako katika shida kubwa sana. Naomba sisi sote tushirikiane kuhakikisha kwamba haya majina yamekuwa Gazzeted mapema sana kwa sababu hali ni nzito. Pia, ningependa nichukue fursa hii kumweleza mwenyekiti wa hazina hiyo kwamba ni muhimu ... view
  • 16 Mar 2023 in National Assembly: . Shida ni kubwa ndugu yangu mwenyekiti. Naomba uwasukume kwa sababu katika ahadi walizotoa tukiwa Pride Inn ni kwamba kila wiki mbili watatoa shilingi bilioni nne. Baada ya hapo hakuna kitu tumeona, hata ndururu! Hali ni ngumu sana. Watoto wa university hawaendi shule kwa sababu ya hali ngumu ya kimaisha. Pia nikutahabarishe Mwenyekiti kwamba Board ya NG-CDF ndiyo inaotoa maamuzi ni kitu gani kifanywe katika maeneo Bunge. Wananchi wamekuwa wakikusanyika wakitoa maamuzi. Kama eneo langu kuna uzoroto wa usalama. Sasa watu wanataka securitylights. Tumekubali tuweke security lights. Ikifikia hapo kwa bodi, wanasema haiwezekani ilhali watu wanaumia. Sio wao wako kule ... view
  • 1 Mar 2023 in National Assembly: Ahsante sana Mhe. Spika wa Muda, kwa kuniruhusu niweze kupenyeza sauti yangu kwa suala hili. Nitafanya haraka kwa sababu ya muda ili wengine wapate nafasi ya kuchangia. Kwa kweli, inasikitisha sana Mahakama Kuu kuidhinisha kusajiliwa kwa vyama hivi vya usagaji na ushoga ama uhanithi. Mimi nitawasihi majaji hao wamche Mwenyezi Mungu. Hapa duniani tumekuja kulima shamba ambalo matunda yake tutayapata mbeleni. Kwa hivyo, lolote wanalolifanya na maamuzi yote wanayoyatoa hivi sasa watakutana nayo mbele akhera, ambapo wote wataondoka katika ulimwengu huu. Hakuna mtu atabaki. Pia wajue kwamba wataweka kumbukumbu za vizazi vilivyoko na vitakavyokuja kulingana na maamuzi ambayo wanayafanya sasa. ... view
  • 21 Feb 2023 in National Assembly: Ninakushukuru kwa taratibu. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 21 Feb 2023 in National Assembly: Kuhusu swala la CBC, kwa kweli taifa halijakuwa tayari kwa haya mageuzi ya elimu. Shule zilizochaguliwa kuwa na junior secondary school ni chache ukilinganisha na wanafunzi walio wengi zaidi. Walimu waliochaguliwa ni wachache ukilinganisha na shule na wanafunzi. Fedha, pia, za kuwezesha mchakato huu kuendelea kikamilifu. Shule zote hazina mahabara na CBC haiwezikukamilika bila mahabara. Wazazi wanaumia kifedha kupeleka watoto wao junior secondary schools. Wanaambiwa wabadili sare za shule na pia waende na madawati. Kila siku kuna mambo mapya mpaka inakuwa vigumu kutekeleza swala hili. Kwa hivyo, ninasimama na wengi wa Wajumbe Bungeni ambao wamezungumzia kuwa swala hilo bado; Serikali ... view
  • 16 Nov 2022 in National Assembly: Asante, Mhe. Spika wa Muda. Hata mimi nilibonyeza kidude kitambo ili nizungumzie swala la NG-CDF, lakini sikupata nafasi. Labda uniruhusu dakika moja niseme ni vyema waachilie hizo pesa kwa sababu zinasaidia wengi sana kule mashinani. Umaskini ulioko kule mashinani ni mkubwa sana. Hata watu wakiambiwa wapeleke mia mbili ya chakula shuleni inawashinda. Ni vyema sana Serikali iachilie hizi fedha ambazo zinasaidia watu maskini. Hali ni ngumu na kazi hakuna. Watu wanategemea hiyo pesa. Kwa hivyo, sioni sababu ya Katibu wa Baraza la Mawaziri wa Hazina ya Taifa kusema kwamba ataenda kutafuta ushauri kwa Mkuu wa Sheria. Hii ni kwa sababu ... view
  • 16 Nov 2022 in National Assembly: Mhe. Spika wa Muda, kupanda miti kando ya barabara ni muhimu sana. Miti inasaidia kunyonya hewa chafu kutoka kwa mazingira na kuachilia hewa safi ambayo tunatumia. Miti husaidia sana kuboresha mazingira. Afya za watu wengi mahali kuna miti ziko imara kuliko mahali hakuna miti. Miti ikipandwa kando ya barabarani ama mitaani itazuia mmomonyoko wa udongo. Ukipanda miti, hata wakati wa mvua hakutakuwa na mafuriko. Katika sehemu ambako hakuna miti, mafuriko yanakuwa makubwa na athari zake zinakuwa kubwa zaidi. view
  • 16 Nov 2022 in National Assembly: Uzuri wa kupanda miti ni kwamba kunafanya mahali panapendeza. Wakati wa ukame, kunakuwa na maua aina fulani yanayotoka. Wakati wa mvua pia kunatokea maua ya aina fulani ambayo hutupatia vivuli katika sehemu zile. Miti pia ni muhimu sana kwa sababu kuna viumbe wanaolala hapo, kama vile ndege ambao wanakwenda pale usiku. Hapo ndipo nyumba zao. Kwa hivyo, ni muhimu kwa mkandarasi yeyote anayejenga barabara alazimishwe apande miti. Miti husaidia watu wengi na hata viumbe vingine ambavyo vinaishi katika miti hiyo. view
  • 16 Nov 2022 in National Assembly: Kwa hayo mengi, ninaunga mkono Hoja hii. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus