Ali Menza Mbogo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 171 to 180 of 292.

  • 8 Nov 2022 in National Assembly: CDF, mambo ya usafiri yangekuwa katika shule za kibinafsi pekee. Naomba kuwa NG-CDF ibakie ili isaidie. Ihalalishwe kwenye Katiba ili iendelee. Si vibaya hata hawa ndugu zetu Maseneta wakipewa fedha, bora zimfaidi mwananchi. Wakati mwingine unasikia Serikali ikisema kuwa uchumi umeimarika. Uchumi hauwezi kuimarika kama mwananchi hana kitu mfukoni mwake! Lazima uchumi uhusiane na mwananchi. Kwa hivyo, hata wale Maseneta wakitaka fedha za kuwasaidia wananchi, wapewe. Ikiwa zile fedha Wawakilishi wa Akina Mama watapewa zitasaidia, itakuwa vizuri zaidi. Ikiwa Wawakilishi wa Akina Mama, Wajumbe na Maseneta watasaidia, wananchi ndio watafaidika. Hili ni taifa letu sote. Kwa hivyo, ni lazima tushirikiane ... view
  • 2 Nov 2022 in National Assembly: Ahsante Mhe. Spika wa Muda. Nachukua fursa hii kumshukuru Mhe. Yusuf Hassan kwa kunipa hii fursa ili niweze kupenyeza sauti yangu katika Hoja hii ya kubuniwa kwa Baraza la Kiswahili. Naunga mkono kwa sababu wakati Baraza hili litakapobuniwa, nina imani kwamba Kiswahili kitashamiri na kitakuwa lugha muhimu katika Taifa letu. Mataifa mengi yaliyondelea yalitumia lugha za mama. Ukiangalia Uingereza, Urusi na Bara la Arabu, wanatumia lugha zao na nchi hizo zimeendelea zaidi. Ukiangalia Taifa Jirani letu la Tanzania, limeweza kuwa na maendeleo mengi kwa sababu ya kutumia lugha zao. Ningeomba kwamba almashauri zote za kiserikali ziweze kuweka maandishi katika milango ... view
  • 12 Oct 2022 in National Assembly: Asante sana, Mhe. Naibu Spika kwa kunipatia fursa ya kupenyeza sauti yangu katika janga hili la ukame. Lakini, kabla ya hayo, nachukua nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kuwa katika Bunge la Kumi na Tatu. Kama sio uwezo wake, singekuwa hapa. Nina imani nitafanya mema wakati huu wa kipindi hiki cha miaka mitano. view
  • 12 Oct 2022 in National Assembly: Pili, nachukua fursa hii kukupongeza kwa kuchaguliwa kama Naibu Spika wa Bunge hili la Kumi na Tatu. Tuna imani utafanya haki pamoja na Spika Moses Wetangula katika The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 12 Oct 2022 in National Assembly: Bunge hili, ili wote wapate fursa ya kuzungumza. Nachukua nafasi hii pia kushukuru familia yangu kwa kunipa moyo na nguvu wakati wa kampeni, ili nisirudi nyuma mpaka nikapata ushindi. Nawashukuru sana. Pia, nichukua fursa hii kuwashukuru wangwana wa Kisauni kwa kunichagua kuwa Mjumbe wao na kwa kuniamini ili niweze kuwaakilisha katika Bunge hili la Kumi na Tatu. Nina imani kwamba wako katika mikono salama na nitakaa na wao. Tutasaidiana kwa hali na mali kuhakikisha kwamba Eneo Bunge letu la Kisauni linasonga mbele. Baada ya kunipumzisha katika Bunge la Kumi na Mbili, nashukuru kwa sababu waliniamini na wakaona kwamba wamekosa huduma ... view
  • 12 Oct 2022 in National Assembly: Namshukuru Mhe. Rais kwa kurudisha huduma za utendakazi wa bandari kwa Wapwani. Tunawaomba wawekezaji warudi ili watumie fursa hiyo ili vijana wetu wapate ajira. Pia, bandari irudishe ile mfumo wa zamani wa ‘white card’ ili watoto wetu waendelee kupata ajira. Watoto wetu wamekaa mabarazani. Tuna imani kwamba ikiwa watarudisha hiyo ‘whitecard’ itatusaidia zaidi ili watoto wengi waajiriwe. Kutakuwa na moyo na hata wao watakuwa na ufahamu kwamba baada ya muda fulani, watarudi kufanya kazi na wengine watabadilishana baada ya miezi mitatu. view
  • 12 Oct 2022 in National Assembly: Suala la maskwota ni tatizo kubwa Pwani, hasa Kisauni. Nina imani Serikali hii ya awamu ya tano itashughulikia suala hili. Moja katika ahadi walizozitoa ni kwamba wataumaliza uskwota na tunasubiri kuona hilo jambo likitekelezwa. view
  • 12 Oct 2022 in National Assembly: Upande wa Kisauni, amri za kufukuzwa nyingi zimetoka. Hatuingilii mahakama lakini tunaomba wawe na utaratibu wa fikra kwamba unapotoa amri ya kufukuza nyumba zaidi ya elfu moja, unaleta matatizo makubwa. Wanaoteseka ni akina mama na watoto wakati nyumba hizo zinabomolewa. Wale ambao wanadai kuwa zile ardhi ni zao walikuwa wapi wakati ambapo watu walikuwa wanajenga msingi, wakajenga hadi wakaweka paa na stima? Mbona watu hawa wakuje wakati mtu amelala kusema ni kwao? Kwa hivyo, naomba mahakama iwe inaangalia sana swala hilo. Katika upande wa ukame, ningeomba kwamba ukame uwe janga la kitaifa kwa sababu kuna watu wanapata dhiki kubwa wanapoenda ... view
  • 31 May 2022 in National Assembly: Asante Mhe. Spika kwa kunipa fursa hii kama Mbunge wa Kisauni. Kwa niaba ya watu wa Kisauni, ninataka kuchukua fursa hii kutoa pole zangu na kupeana mkono wa buriani kwa mwenzetu aliyetuacha jana kutokana na ajali ya barabarani. Mhe. Kamoti hakuwa Mjumbe tu bali aliishi eneo bunge langu. Eneo Bunge za Kisauni na Rabai zimeshikana. Kwa hivyo, ni mtu aliyekuwa karibu sana na mimi kwa sababu mahitaji yake kama mwananchi anayeishi katika eneo langu, yalinipitia ili niweze kuyatatua. Hivi majuzi, niliweza kutengeza barabara iliyopitia pale alipoishi marehemu Mhe. Kamoti, lakini Mwenyezi Mungu alikuwa na mipango mengine. Tumekuwa naye juzi alipokuwa ... view
  • 6 Apr 2022 in National Assembly: Thank you, Hon. Temporary Deputy Speaker, for giving me this opportunity to contribute to this important Bill that has been brought to the Floor of the House by the able Member, Hon. Gikaria, the former Chairperson of the Departmental Committee on Energy. I wish he was still the Chair of that Committee, because what we have experienced recently would not have happened. It has never happened during his tenure. This demonstrates that he is a capable Member of this House. Hon. Temporary Deputy Speaker, this is a timely Bill. It is extremely important to the marginalized groups and interested groups ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus