All parliamentary appearances
Entries 241 to 250 of 993.
-
7 Mar 2024 in Senate:
The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard Services,Senate.
view
-
7 Mar 2024 in Senate:
We pay taxes, like other Kenyans, understand the political affiliation of Homa Bay, Migori, and Kisumu. However, as we build for them, let them allow us also to enjoy the same infrastructure that they are enjoying. I want Sen. Osotsi to inform our people at home, not me here on the Floor of the House. I, therefore, support it.
view
-
6 Mar 2024 in Senate:
Asante, Bw. Spika kwa nafasi hii. Ni jambo la kutamausha sana sisi kama Maseneta kurauka asubuhi na mapema, wengine kupuuzilia mbali staftahi ili tuje tujadili mambo muhimu ya Serikali na nchi ya Kenya. Bw. Spika, baadhi ya Mawaziri ambao wamealikwa hapa ni lazima wajue kwamba kuja kwao hapa kutatoa mwelekeo na suluhisho ama kupea matumaini kwa Wakenya. Mhe. Rais amekuwa akizuru pembe mbalimbali za nchi ya Kenya akiahidi na kupea mwelekeo kwa miradi ya maendeleo kwa Wakenya. Miradi hii ambayo yeye hupea mwelekeo, wale ambao lazima watekeleze ni Mawaziri ambao wachache wao wamealikwa hapa na wamefeli kufika. Waziri wa Barabara ...
view
-
6 Mar 2024 in Senate:
Naomba kuondoa hoja hiyo na kushinikiza kwamba, iwapo mfanyikazi ama Waziri analipwa mshahara, anaendeshwa kwa magari ya kifahari na anatibiwa kwa pesa za mtozwa ushuru, ilhali anayelipa ushuru hamuoni mtumishi wa umma popote katika Kaunti hiyo, na mtumishi huyo hajalalamika kwamba analishwa, kuvishwa na kuendeshwa vizuri, bila shaka anafurahia jasho la Wakenya. Bw. Spika, niliuliza Waziri wa Mausala ya Jinsia Maswali kuhusiana na mimba za mapema katika Kaunti ya Bungoma, kwa sababu ya upungufu wa sodo na pesa za The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposes only. A certified version of this Report can be ...
view
-
6 Mar 2024 in Senate:
kuimarisha biashara za akina mama na wajane. Waziri huyu mpaka leo ameweka nta kwenye maskio na kinywa chake amekifunga kabisa. Tunajiuliza haya maswali kwa sababu alichaguliwa kwa mrengo wa Kenya Kwanza. Ni lazima adhihirishe uwezo wake wa kuchapa kazi kwa kutembea katika pembe zote na kujadili masuala haya na wananchi wa Kenya. Bw. Spika, haya maswali, yeye na Waziri wa Elimu lazima watembee pamoja kusuluhisha masuala ya mimba za mapema na masuala ya wanawake na watoto katika taasisi za elimu katika nchi ya Kenya. Sasa kile tunasema sio kwamba tunaomba ati tafadhali waje, lazima waje. Mimi niko tayari kujiunga na ...
view
-
6 Mar 2024 in Senate:
Nitadai haki kwa niaba ya watu wa Bungoma na Wakenya, ili Serikali niliyoipigania na ninayoipigania ipate sifa na ishukuriwe kwa jasho na kwa kazi wanayofanya. Bw. Spika, Mawaziri hawa lazima wakuje. Asante, Bw. Spika.
view
-
6 Mar 2024 in Senate:
Asante, Bw. Naibu Spika, kwa kunipa nafasi hii. Mchango ni kwamba matarajio ya Wakenya yataweza kuafikiwa kutokana na pesa ambazo tunagatua kwenda mashinani. Juzi, magavana walidai kwamba pesa zimechelewa na miradi mingi ya maendeleo haijatimilika Wengine wamekuwa wakikenua vichwa wakidai tumepunguza mgao wao. Leo, mbele ya Wakenya wote, wamejionea wazi msimamo wa Bunge la Seneti. Tunataka waongezewe pesa ili ziambatane na majukumu yaliyogatuliwa katika Katiba Zile pesa ambazo kaunti zinawatozwa watu ni kama sadaka au kafara kule mashinani. Naomba hili Bunge la Seneti lifuate hizi pesa ili tuhakikishe zote zinazotozwa watu wa kaunti zetu, zinaweza kuhesabika na kuajibikiwa kwa miradi ...
view
-
5 Mar 2024 in Senate:
Asante, Bw. Spika, kwa fursa hii ili niweze kuwakaribisha wandani wangu na rafiki zangu wa kisiasa na vilevile wapiga kura wangu wa Kaunti ya Bungoma. Seneti lina wanaume na wanawake wa tajriba na heshima kuu. Kule Kaunti ya Bungoma, unapowatazama, kuna mabinti ambao walipambana kisiasa kuwabwaga wanaume na wanawake kwa njia ya kidemokrasia. Bungoma ni Kaunti ambayo inajulikana kwa kutoa viongozi wanawake ambao wanajua kazi wanayopaswa kufanya na kwamba kura wanayopata sio kwa sababu ya urafiki wa mahaba ama wa kidini au wa kibiashara. Langu ni kuwakaribisha wanawake ninyi shupavu na wanaume wenzangu kwamba hapa ndimo Seneta wenu huchapa kazi. ...
view
-
21 Feb 2024 in Senate:
Thank you, Mr. Speaker, Sir. I rise, pursuant to Standing Order No.53(1), to seek a Statement from the Standing Committee on Trade, Industrialization, and Tourism regarding cooperative societies in Bungoma County. In the Statement, the Committee should- (1) List of all cooperative societies operating within Bungoma County, detailing their specific areas of operation. (2) List the cooperative societies funded by the Bungoma County Government for the financial years 2022/2023 and 2023/2024, detailing the projects implemented with this support. (3) State the criteria used by the county government to select cooperatives for funding, furnishing financial and audit reports of the cooperative ...
view
-
21 Feb 2024 in Senate:
Thank you, Mr. Temporary Speaker, Sir. I fully second.
view