Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 31 to 40 of 133.

  • 9 Jul 2024 in Senate: ile ya kilimo, tunasema jambo la haki. Linafaa lisikizwe na tuone kwamba tumewekewa kiongozi ambaye atapeleka Kenya mbele katika masuala ya kilimo. Nikiendelea kujadilia mambo ya corruption, katika serikali zetu za kaunti, kuna nafasi nyingi sana ambazo zilikuwa zimetolewa za kazi. Tumeona corruption ikiwa na magavana wetu katika kaunti zote 47. Magavana wengine wanaandika vijana kazi kupitia discrimination . Hilo ni jambo ambalo tunafaa kulilaani katika Bunge hili na tuseme kwamba kijana yeyote ambaye ana view
  • 9 Jul 2024 in Senate: ya kuajiriwa kazi katika kaunti yake aweze kupata kazi. Tusiandike wananchi wetu kazi kwa kujuana, kuwa alinifanyia campaign au alisimama nami katika mambo tofauti. Tupatie watu competent wafanye kazi na vijana ambao wamehitimu na kusoma ili Kenya yetu isonge mbele. Bw. Spika wa Muda, ningependa nitoe pendekezo kwamba ili Kenya lsonge mbele, jambo la kwanza ni kwamba Serikali hii lazima ipigane na ufisadi kabisa. Itakapopigana na ufisadi, hizi pesa ambazo zinapotea kila uchao zitakosa mashimo ya kuingia na zitafanyia wananchi kazi. The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can ... view
  • 9 Jul 2024 in Senate: Nikisema ufisadi naanza na county Government hadi national Government. Ufisadi upigwe marufuku, kila mtu atosheke na mshahara wake na afanye kazi ambayo anafaa kuifanya na inavyostahili ili Kenya isonge mbele. Jambo lingine ambalo ni muhimu sana ni kwamba ni lazima tuweze kuhusisha vijana katika mambo ya kuendeleza nchi hii. Namaanisha kwamba lazima tuangalie kwamba wakati tunapofanya public participation, vijana wetu wapewe nafasi na kipaombele, waweze kutoa maoni yao na matatizo ambayo wanapitia kila uchao. Jana, nimeona kijana mmoja akiongea katika runinga. Alikuwa anatoa mawazo yake kama kijana akisema kwamba viongozi wasishinde wakiuliza ni nani anaongoza hawa Gen Zs. Hawana kiongozi ... view
  • 11 Jun 2024 in Senate: Asante Bw. Spika, kwa kunipatia hii fursa. Naomba niweze kuungana na wenzangu katika kupongeza Bunge hili la Seneti kwa sababu ya kazi nzuri ambayo imefanyika mwaka huu. Magatuzi zetu hazina vikwazo kwa sababu tumeshawapatia pesa ambazo zitawezesha magavana kufanya kazi wanayostahili kufanya ili wananchi wa kaunti tofauti tofauti waweze kupata manufaa. Katika Kaunti ya Lamu, tumepata mgao wa zaidi ya Shilingi 300 milioni ambazo zitawezesha Kaunti ya Lamu kupata maendeleo. Tunapoongea sasa, Gavana wa Kaunti ya Lamu hana sababu ya kutoweza ku-equip hospitali zetu na madawa ya kutosha. Ukienda katika ECDE classes ambazo kwa muda mrefu katika Kaunti ya Lamu ... view
  • 11 Jun 2024 in Senate: Asante Bw. Spika, kwa kunipatia hii fursa. Naomba niweze kuungana na wenzangu katika kupongeza Bunge hili la Seneti kwa sababu ya kazi nzuri ambayo imefanyika mwaka huu. Magatuzi zetu hazina vikwazo kwa sababu tumeshawapatia pesa ambazo zitawezesha magavana kufanya kazi wanayostahili kufanya ili wananchi wa kaunti tofauti tofauti waweze kupata manufaa. Katika Kaunti ya Lamu, tumepata mgao wa zaidi ya Shilingi 300 milioni ambazo zitawezesha Kaunti ya Lamu kupata maendeleo. Tunapoongea sasa, Gavana wa Kaunti ya Lamu hana sababu ya kutoweza ku-equip hospitali zetu na madawa ya kutosha. Ukienda katika ECDE classes ambazo kwa muda mrefu katika Kaunti ya Lamu ... view
  • 11 Jun 2024 in Senate: hali tata. Tukiingia katika maswala ya kilimo ambayo ni kitega uchumi cha wakaazi wengi wa Kaunti ya Lamu, kama Seneta wa sehemu hiyo, ningependa kuona ya kwamba kilimo kimeimarishwa kwa sababu pesa za kutosha zimeenda katika gatuzi hili la Lamu na sasa tunatarajia kuona mambo makubwa, manufaa na maendeleo ya watu wa Kaunti ya Lamu. Naunga mkono Mswada huu na kusema kuwa umekuja kwa wakati unaofaa na sasa ni wakati wa kuwafanyia wananchi wetu kazi. Asante. view
  • 11 Jun 2024 in Senate: hali tata. Tukiingia katika maswala ya kilimo ambayo ni kitega uchumi cha wakaazi wengi wa Kaunti ya Lamu, kama Seneta wa sehemu hiyo, ningependa kuona ya kwamba kilimo kimeimarishwa kwa sababu pesa za kutosha zimeenda katika gatuzi hili la Lamu na sasa tunatarajia kuona mambo makubwa, manufaa na maendeleo ya watu wa Kaunti ya Lamu. Naunga mkono Mswada huu na kusema kuwa umekuja kwa wakati unaofaa na sasa ni wakati wa kuwafanyia wananchi wetu kazi. Asante. view
  • 22 May 2024 in Senate: Asante, Bw. Spika wa Muda, kwa fursa hii ili niweze kuchangia Mswada huu muhimu ambao unahusisha ukuzaji wa korosho na nazi. Nashukuru Sen. Kibwana kwa kuleta Mswada huu kwa wakati unaofaa. Tulikuwa tunahitaji Mswada huu sisi kama wakaazi wa Pwani. Nazi na korosho ni vitega uchumi katika kanda yote ya Pwani. Mswada huu utasaidia kufanikisha wakulima wetu ili wapate kitega uchumi ambacho kinazingatiwa kisheria. Wakulima wa Pwani waweze kuuza mali yao. Ili kusaidia wakulima wetu, Serikali, kupitia Wizara ya Kilimo na Mifugo, lazima ifanye utafiti mwafaka kuhakikisha wanapata mbegu nzuri za uzalishaji wa korosho na nazi. Hiyo ikizingatiwa vizuri, tutaweza ... view
  • 22 May 2024 in Senate: Ni vyema Wizara ya Kilimo na Mifugo ifanye utafiti. Wanafaa kutoa dawa mwafaka ambazo zitasaidia. Dawa hizo zisiwe na madharau ya moja kwa moja kwa mkulima na mazingira. Hilo likifanyika, bila shaka mazao yatapatikana kwa wingi na kusaidia wakazi wa sehemu mbalimbali. Pia naunga mkono kwamba tutafute masoko katika nchi za nje ili wakulima wetu watie bidii kwa sababu mazao hayo yanahitajika. Serikali ikiwahakikishia kwamba wanapokuza mazao hayo watapata masoko katika nchi za nje. Ikifanya hivyo, bila shaka itasaidia sana wananchi wetu na Kenya nzima. Bw. Spika wa Muda, kuna jambo ambalo limekuwa likiendelea. Watu kutoka nchi za nje wamekuwa ... view
  • 8 May 2024 in Senate: Mr. Temporary Speaker, Sir, I wish to take this opportunity to congratulate Waziri for the good job he is doing. Lamu has been in the limelight for a long time for the obvious bad reasons. Now it is a peaceful county. We had many security problems since 2014, but as of now, things are okay. I wanted to ask Waziri two questions. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus