Mohamed Faki Mwinyihaji

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 1131 to 1140 of 2123.

  • 1 Dec 2021 in Senate: Kwa mfano, kudhibiti vyombo vya kuhifadhi samaki wanapovuliwa kwa wingi, barabara katika sehemu ambazo wanavuvi wanavua na zile bandari zinapokea samaki wale, hazijapewa kipaumbele katika maendeleo ya uchumi samawati. view
  • 1 Dec 2021 in Senate: Bi. Spika wa Muda, sisi watu wa Pwani tuna tumbojoto kuhusiana na ripoti zilizotolewa kuwa sehemu ya bandari ya Kenya itabinafsishwa kupitia shirika la Kenya National Shipping Line ambalo limeingia mazungumzo na shirika la Mediterranean Shipping Company (MSC). view
  • 1 Dec 2021 in Senate: Mwaka jana kulitolewa Executive Order ambapo mashirika ya Kenya Ports Authority (KPA), Kenya Railways Corporation (KRC) na Kenya Pipeline Company (KPC) yaliletwa pamoja na Industrial and Commercial Development Corporation (ICDC) ambalo ni taasisi ya Serikali ili kuwa na usimamizi moja, kupitia kwa Wizara ya Fedha. view
  • 1 Dec 2021 in Senate: Mhe. Rais hakuzungumzia suala hili ili kutoa mwongozo. Je, suala hili limeleta natija ama la? Ni mambo gani yamezuia kupatikana kwa maendeleo kwa usafirishaji wa mizigo na kudhibiti mambo ya reli, kama ilivyokuwa imekusudiwa na mpaka sasa haijakamilishwa. view
  • 1 Dec 2021 in Senate: Swala hili la kubinafsishwa kwa bandari limetia sana tumbojoto wakazi wa Pwani kwa sababu bandari ndio mtaji mwenyezi Mungu amewajalia nalo. Kwa hivyo, hatutakuwa tayari wakati wowote kuwacha mtaji huu uweze kuharibika. view
  • 1 Dec 2021 in Senate: Bi. Spika wa Muda, masuala ya usafirishaji wa mizigo kutoka bandari ya Mombasa yalistahili kuzungumziwa kwa sababu Serikali inalazimisha mizigo yote ibebwe na shirika la Standard Gauge Railways (SGR), shirika la reli la Kenya. Hata hivyo, kuna uhuru wa biashara nchini. Kuna wale wanaofanya biashara za malori na za kibinafsi wanastahili kupewa nafasi kufanya hivyo. The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate. view
  • 1 Dec 2021 in Senate: Bi. Spika wa Muda, kwa kumalizia pia ni kwamba, tumeona kuwa maswala ya usafirishaji wa mizigo ni njia moja ambayo itasaidia Wakenya kuweza kujikomboa, hususan watu wa Mombasa na wengine ili kuweza kupata biashara katika kaunti zetu. Ukiangalia mkondo wa barabara kutoka Mombasa mpaka Malaba, kuna biashara nyingi ambazo zinafanyika katika barabara hiyo. Biashara zile ninawezakufilisika iwapo hatutaweza kuwa na usafirishaji wa mizigo kwa njia nyingine mbali na njia ya reli. Nikimalizia, bado tuna changamoto nyingi ambazo nchi inatakikana kuzikabili na kuziepuka. Changamoto hizi tunaweza kuzikabili tu wakati nchi yetu itakuwa na amani. Tutakuwa tunavuta Kamba katika sehemu moja. Hususan ... view
  • 10 Nov 2021 in Senate: Asante, Bw. Spika, kwa kunipa fursa hii kumaliza mchango wangu kwa ripoti hii. Niliposimama jana, nilikuwa nimeeleza kuwa baadhi ya wale ambao walichukuliwa na hadi leo hawajapatikana ni kijana anayejulikana kwa jina la Mubarak Husni. Alichukuliwa tarehe 25/3/2018. Niliweza kuleta Taarifa hapa katika Bunge la Senati na hadi leo, habari za kijana huyu, pahali alipo, ama kama yuko hai au ashafariki hazijulikani. Haki Afrika ambayo ni kundi la haki za kibinaadamu ambayo inafanya kazi Mombasa kimeweza kutoa ripoti yake. Mpaka sasa, mwaka huu wa 2021 peke yake, kufikia tarehe 30/10/2021, watu 42 wameweza kuchukuliwa bila ya sababu yeyote. Kati ya ... view
  • 10 Nov 2021 in Senate: Bw. Spika, wakati wa nyuma, haki zilipokuwa zimedhulumiwa wakati wa Serikali ya awamu ya pili ya hayati Daniel Arap Moi, mambo haya yalipo angaliwa wakati wa Serikali ya Mheshimiwa Kibaki, watu wengi ambao walifanya mambo kama haya walipelekwa Mahakamani. Rais msataafu hayati Moi pia alipelekwa mahakamani kuhusiana na haki kama hizi. Kwa hivyo, ninawaonya wale ambao hivi sasa wanaendelea kudhulumu na kuhujumu haki za binadamu. Sheria itashikana na wao wakati mmoja. Hakuna swala ambalo linaweza kupita bila kuwa na sheria itakayofuatilia kuhakikisha kwamba wale ambao wameweza kupotezwa, na kuuliwa kiholela wamelipwa ridhaa ili familia ziamini kwamba haki imeweza kutendeka. Bw. ... view
  • 10 Nov 2021 in Senate: (ATPU), Director wa I ntelligence, hakuna kitu kitakulinda wewe wakati utakapostaafu ama utakapotoka katika kazi hiyo. Sheria itapambana na wewe na siku moja itakushika na kukupeleka jela kama vile ambavyo unawatesa na kudhulumu haki za Wakenya ambao washikwa bila sheria yoyote. Bw. Spika, kwa kumaliia ninasema kwamba mapendekezo yote ambayo yametolewa, ni kweli yanaweza kufanya kazi. Lakini, pia tungependa kuwe na mwongozo kuwa wale wote ambao familia au wapendwa wao wamechukuliwa kiholela, wapate fursa ya kuelezea maswala kama haya. Hii ni kwa sababu, hivi sasa, wengi wanaogopa. Mtu anaambiwa mtoto wake amechukuliwa kwa sababu ni Alshaabab . Kwa hivyo, hawezi ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus