Mohamed Faki Mwinyihaji

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 1551 to 1560 of 1581.

  • 29 May 2018 in Senate: Mr. Deputy Speaker, Sir, the Committee is not ready to move the Bill. view
  • 29 May 2018 in Senate: Mr. Deputy Speaker, Sir, we were supposed to have a meeting this morning but it aborted due to lack of quorum. The Chairperson of the Committee is unwell. Only two Senators were in attendance. Therefore, the meeting did not take place. view
  • 29 May 2018 in Senate: Asante, Bw. Naibu Spika, kwa kunipa fursa hii ya kuunga mkono Hoya ya Sen. (Dr.) Gertrude Musuruve. Kwanza kabisa, Kiswahili ni lugha ya taifa kulingana na Katiba. Ni haki ya watoto wetu wenye ulemavu wa maskio kufunzwa kwa lugha ya Kiswahili. Hiyo ni haki yao ya Kikatiba. Sisi kama Bunge la Seneti tunapaswa kuwahakikishia kwamba haki hiyo inatimizwa. Jambo la pili ni kwamba ukosefu wa mtaala wa Kiswahili kwa wale ambao wana ulemavu wa maskio ina maana kwamba tunawanyima haki yao ya kikatiba kufunzwa kwa lugha ambayo wanaitaka. Katika sehemu nyingi katika Jamhuri ya Kenya, watu wanazungumza Kiswahili kama lugha ... view
  • 17 May 2018 in Senate: Asante, Bi Spika wa Muda, kwa kunipa fursa hii kuchangia mjadala wa kuahirishwa kwa Bunge la Seneti ili tuhudhurie Legislative Summit mjini Mombasa katika Kaunti ya Mombasa. Kama Seneta wa jiji la Mombasa, Kaunti ya Mombasa, nachukua fursa hii kwanza kuwakaribisha nyote katika mji wa Mombasa wakati wa view
  • 17 May 2018 in Senate: Not at all, Madam Temporary Speaker. view
  • 17 May 2018 in Senate: Bi Spika wa Muda, ni lazima tuweze kuzisaidia hizi bunge za kaunti ili wale Wabunge waweze kuchukua majukumu yao kikamilifu; ya kuweza kuangalia raslimali zinazokwenda kule zinafuatiliwa kikamilifu. Tumeona kwamba katika kaunti nyingi Wabunge wale wako tayari kusafiri nje ama safari zingine katika Jamhuri lakini kukaa ndani na kuweza kuuliza maswali magumu yale ambayo yatakikana kuulizwa inakuwa changamoto. The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposes only. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate view
  • 9 May 2018 in Senate: Samahani Bw. Spika. Sen. (Dr.) Langat ambaye ni Seneta wa Bomet anaweza kuongea nami ana kwa ana bila tashwishi yoyote kwamba anaweza kuripotiwa sehemu fulani kwamba amevunja sheria au mwafaka walio nao. Seneta wa Laikipia pia amezungumza kwa ufasaha kuunga mkono uwiano na akatoa mfano wa kupigana na simba ambaye anakula nyama na ukawaacha inzi ambao wanarukaruka pale. Ni jambo nzuri ambalo limekuja katika nchi yetu ya Kenya. Tuliunge mkone ili makabila yote au jamii zote katika nchi ya Kenya waunganishwe katika serikali ambayo twataka kuitumikia ili kuhakikisha kwamba yale matatizo tuliyokuwa nayo ya kura yanakwisha. Ni wazi kwamba kutokana ... view
  • 18 Apr 2018 in Senate: Asante sana, Bwana Spika kwa kunipa fursa hii kujiunga na Wakenya wengine na wakaazi wa Murang’a kuomboleza kifo cha hayati Matiba. Sisi watu wa Pwani, tulimtambua Matiba kama mwekezaji mkubwa katika biashara ya utalii katika eneo la Pwani. Vile vile, alikuwa rafiki mkubwa wa Pwani kwa sababu wakati alipokuwa akiwaania kiti cha Kenya Football Federation (KFF) kama mwenyekiti, Pwani ndio ilimuunga mkono wa kwanza ndiyo nchi nzima ikafuata badaaye. Kwa hivyo, tunamtambua hayati Matiba kama kiongozi ambaye alikuwa akiwapa kipaumbele Wakenya ambao hawakubahatika kijamii, aidha kimasomo, kibiashara na katika hali zingine za kijamii. Kifo cha Matiba pia kinatukumbusha wale wengine ... view
  • 28 Mar 2018 in Senate: Bw. Naibu Spika, nimesimama kuunga mkono Hoja ya Sen. Orengo na kuwapongeza viongozi wetu,vinara wawili; Mhe. Rais Uhuru Kenyatta na Mhe. Raila Amollo Odinga. Viongozi hawa walikuwa mahasimu wajadi lakini juzi, siku tukufu ya Ijumaa, walikuja pamoja, wakakumbatiana, wakapeana mikono na wakashusha hali mbaya ya siasa ambayo iliyokuwepo katika nchi yetu ya Kenya. Ilhali, yapo mengi ambayo bado yana takikana kufanywa kwa sababu ukabila, ufisadina mambo mengi ambayo waliyazungumzia bado yako. Ni lazima tushirikiane kama Bunge la Seneti na nchi kwa jumla kuhakikisha kwamba yametatuliwa. Jambo moja ambalo ningependa kuzungumzia ni kwamba hatuna kitu cha kutuunganisha pamoja sisi kama Wakenya ... view
  • 27 Mar 2018 in Senate: Yes, Mr. Deputy Speaker, Sir, it is fine with me. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus