Mohamed Faki Mwinyihaji

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 571 to 580 of 2123.

  • 29 Aug 2023 in Senate: Asante, Bw. Spika, kwa kunipa fursa kuchangia Hoja hii ya mjadala wa kitaifa. Najiunga na wenzangu kuwapongeza viongozi wa nchi na wa Azimio, Mheshimiwa ‘Baba’ Raila Amolo Odinga, kwa kuweza kuwa na makubaliano kuhusiana na maswala haya. Wakati kulitangazwa kwamba kutakuwa na mjadala wa kitaifa, nchi ilipumua, biashara zikafunguka na amani ikarudi katika nchi yetu ya Kenya. Kwa hivyo, ni masikitiko kwamba wenzetu hapa wanaweza kuzungumza kwamba ilikuwa haifai kwa viongozi hawa kuwa na mjadala. Tukiangalia hata uhuru uliopatikana katika nchi hii, baadhi ya ndugu zetu walikufa lakini baada ya mazungumzo, kukapatikana mwafaka kule Lancaster na uhuru katika nchi yetu ... view
  • 29 Aug 2023 in Senate: Tuliona jana katika vyombo vya habari akitishia kupeleka watu mbinguni. Yeye sio Yesu wala mtume. Sisi sote ni wananchi na binadamu wa Kenya. Iwapo kuna mambo yoyote ambayo yanatakiwa kuzungumzwa, yazungumzwe kwa njia ya mijadala view
  • 29 Aug 2023 in Senate: Bw. Spika, mimi sijatoka nje ya Hoja. Ni jambo ambalo lilikuwa la adhiri na kila mtu aliona. view
  • 29 Aug 2023 in Senate: Bw. Spika ndio ninasema ya kwamba mimi niko ndani ya Hoja ya leo--- view
  • 29 Aug 2023 in Senate: Bw. Spika, niko ndani ya Hoja na nitaendelea kubaki hapo. Mwisho, ninasema ya kuwa hakuna soko lisilo na wendawazimu. Majadiliano yataendelea. Wale ambao wanasema ya kwamba hakuna, mwisho wataona ya kwamba yamekuwa na kikomo chake. Waswahili husema, “Haiwi, haiwi, mwisho huwa.” Pia walisema wakati mwingine, “Amani haiji ila kwa ncha ya upanga. Kwa hivyo, ninaunga mkono Hoja hii. Tuko tayari kufanya lolote ambalo linatakikana kama viongozi katika Bunge hili kuhakikisha ya kwamba--- view
  • 9 Aug 2023 in Senate: Bw. Naibu Spika, taarifa aliyoisoma dada yetu Sen. Okenyuri ni muhimu sana, kwa sababu inazungumzia maswala ya utalii. Ni masikitiko kwamba ameizungumzia katika Kanuni ya Kudumu ya 52(1) ambayo haitupi fursa hususan wale ambao wametoka kwenye maeneo ya kitalii, si kama maeneo ya Nandi ambayo hayana utalii, ili waweze kuchangia taarifa kama hii. Namshauri dadangu kwamba siku nyingine akiwa na Kauli nzuri kama hii, aweze kuileta kwa kanuni ambayo itatupa nafasi ya kuchangia. view
  • 9 Aug 2023 in Senate: Bw. Naibu Spika, wakati mwingine akileta Kauli nzuri kama hii inafaa ashauriwe na ofisi ya Katibu, ili Kauli kama hizi zisisomwe bila kuchangiwa na Maseneta wengine. Jana Sen. Okenyuri alisoma taarifa muhimu sana, lakini hatukupata--- view
  • 9 Aug 2023 in Senate: Bw. Naibu Spika, Nampongeza --- view
  • 9 Aug 2023 in Senate: Bw. Naibu Spika, Nampongeza dada yetu Sen. Okenyuri kwa kuzungumzia swala hili la utalii. Utalii ni moja ya zile--- view
  • 9 Aug 2023 in Senate: Hapa Seneti najulikana kama Sen. Mwinyihaji Faki Mohammed. Khatib ni jina la uwakili. Madam Temporary Speaker, I thank you for giving me this opportunity to comment on the two Statements. The first one is the Statement by Sen. Kavindu Muthama on the Ad Hoc Committee on compensation of the bomb blast victims. I commend Sen. Kavindu Muthama and her Committee for the splendid work they have done in the one month they have been in existence. The work they have done is commendable. I hope that by the end of their term, the victims of the bomb blast will have ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus