1 Aug 2023 in Senate:
The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard Services,Senate.
view
1 Aug 2023 in Senate:
Vile vile, kazi ya kutafuta Deoxyribonucleic Acid (DNA) pia ina changamoto kwa sababu hatuna vifaa vya kupima DNA hapa. Mpaka, ziwasilishwe Afrika Kusini ambako pia inachukuwa muda kuweza kuwatambua wale waliofariki na jamaa zao tofauti tofauti. Wengi ambao walienda kule Shakahola walibadili majina yao. Kama unaitwa Mohamed Faki, kule unajiita jina lingine ambalo hata kama umeweza kupatikana, jina lako na stakabadhi zako zinaonyesha majina tofauti na yale ambayo ulikuwa unajulikana nayo. Kwa hivyo, imekuwa ni vigumu kabisa kuweza kuwatambua watu wale na kuwaunganisha na familia zao ili waweze kuzikwa. Bw. Spika wa Muda, muda uliyokuwa umepeanwa ni miezi mitatu lakini ...
view
1 Aug 2023 in Senate:
The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard Services,Senate.
view
1 Aug 2023 in Senate:
Bw. Spika wa Muda, ni swala ambalo linaibuka na pia ningependa Mwenyekiti, aliangalie swala hilo wakati tutakapo ongezewa muda kwa sababu ni tatizo ambalo litahujumu sheria zetu za kuhusu haki za kibinadamu. Nikimalizia, leo tukiwa katika chakula za mchana, tulikuwa na Seneta wa Kaunti ya Bungoma. Yeye pia alinieleza kwamba majuzi, kuna watu kama hao wamepatikana Nakuru. Walikuwa wanaelekea sehemu za Ethiopia kuenda kwa maswala kama haya ya Shakahola. Ni mambo ambayo bado yako, dini kama hizi bado ziko na fikra kama hizi bado ziko. Kwa hivyo, inafaa tuweze kumaliza swala hili na tuliangalie vizuri ili kuwe na msingi wa ...
view
25 Jul 2023 in Senate:
Bw. Spika, nimesimama kuambatana na Kifungu cha 52 (1), cha Kanuni za Kudumu za Seneti kutoa Kauli kuhusu siku ya Kimataifa ya Lugha ya Kiswahili iliyoadhimishwa mnamo Tarehe 7 Julai, 2023. Bw. Spika, Kiswahili ni Lugha ambayo inatumiwa na kuzungumzwa na zaidi ya watu milioni 200 katika Bara la Afrika. Hii ndiyo lugha inayokuwa na kusambaa kwa kasi zaidi ulimwenguni, ikizingatiwa kuwa mataifa ya Uchina na Japan yameanza kufunza lugha hii nchini mwao. Afrika Kusini pia ni taifa ambalo lugha hii imeanza kufunzwa. Moja ya maazimio ya Umoja wa Afrika ni kwamba siku moja lugha yetu hii ndiyo itakayo kuwa ...
view
25 Jul 2023 in Senate:
Nchini Kenya, sherehe hizi ziliadhimishwa na jamii ya Waswahili katika eneo la Mama Ngina Water Front, Kaunti ya Mombasa. Maeneo haya ni baadhi ya turathi za Waswahili na mahali hapa tangu zamani palijulikana kama Mzimle. Bw. Spika, wakati maadhimisho haya yakifanyika, inapaswa tuzingatie hatua tulizopiga katika kuendeleza lugha ya Kiswahili. Hapa Seneti tumeweza kufasiri Kanuni zetu za Kudumu kwa lugha ya Kiswahili lakini bado zipo hatua nyingi zinazofaa kupigwa ili tuwe na matumizi ya Kiswahili katika Seneti. Kwa mfano, bado hatuweza kufasiri Miswada ya Sheria, Ardhihali na ripoti za kamati kwa lugha ya Kiswahili. Hatua hii itasaidia pakubwa kuwapa ufahamu ...
view
25 Jul 2023 in Senate:
Niko na nyingine ya feri.
view
25 Jul 2023 in Senate:
Bw. Spika, nimesimama chini ya kifungu cha 52(1) cha Kanuni za Kudumu za Seneti kutoa Kauli kuhusu swala la kitaifa kuhusiana na kuzorota huduma za feri katika kivuko cha Likoni. Mheshimiwa Spika, kivuko cha Likoni kinaunganisha sehemu ya Pwani kusini na kisiwa cha Mombasa. Vile vile, kinaunganisha Kenya na Tanzania kupitia barabara ya Malindi-LungaLunga-Horohoro-Tanga-Bagamoyo. Barabara hii ni ya kimataifa. Kina umuhimu mkubwa kwa maisha ya wanabiashara, sio kwa kaunti za Mombasa na Kwale pekee, bali pia kwa Afrika Mashariki na Afrika kwa jumla. Hivi karibuni, huduma katika kivuko hicho zimedorora sana. Kumekuwa na msongamano mkubwa wa magari na watu wanaotumia ...
view
25 Jul 2023 in Senate:
Mheshimiwa Spika, hili daraja la miguu lilianzishwa 2020 na liligharimu Serikali karibu Kshs1.4 bilioni. Daraja ni jipya na halina sababu ya kurekebishwa kwa muda mrefu kama vile ilivyopangwa. Itakumbukwa kwamba, daraja la kuvukia kwa miguu kwa wasafiri wanaotembea kutoka Likoni hadi kisiwani lilizinduliwa wakati wa janga la Corona, ili kuondoa msongamano na kurahisisha usafiri. Kwa hivyo, kabla ya kulifunga daraja hili, ni muhimu kwa Halmashauri ya Bandari kuweka mikakati mbadala kupunguza msongamano katika kivuko cha Likoni. Kuna wawekezaji wanaomiliki vyombo vya usafiri baharini na ambao wako tayari kutoa huduma hizo katika kivuko cha Likoni, lakini Halmashauri ya Bandari imekataa kuwapa ...
view
18 Jul 2023 in Senate:
Bi. Spika wa Muda, nimemusikiza mweshimiwa Wafula kwa makini. Lakini Kenya hii inajulikana watu ambao walikula pesa ya mahindi na anayejulikana ni mmoja pekee yake hapa na hatuna haja ya kumtaja na kuna ushahidi. Asante.
view