Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 61 to 70 of 417.

  • 14 Nov 2024 in Senate: Mimi kama Seneta wa Kirinyaga, kwa sababu ya watu wa Kirinyaga na Kenya nzima, kwa wale wote ambao nimeongea nao na wale wanaoketi katika mabaraza kuongea shida zao na kutualika sisi kwenda kuwapa msaada, kwa ajili ya akina mama na wale ambao wamejiunga katika vikundi kule Kirinyaga ili kuchangisha pesa kusaidia waliofiwa, sitaunga mkono Mswada ulio mbele yetu. view
  • 13 Nov 2024 in Senate: Asante, Bw. Naibu Spika. Ili nifike hapa mapema nilitoka nyumbani kumi asubuhi. ndio nipate nafasi ya kujadili kuhusu mengi hususan yanayohusu Wizara ya Afya ambayo ni muhimu sana katika nchi hii. Tunaweza jenga barabara na mambo mengi lakini hatuwezi yatekeleza majukumu haya kwa wafu. Wanaotumia hizo huduma ni waliohai. Namwombea Daktari Hon. Barasa apone haraka na apate nafasi ya kuja kujibu maswali. Waswahili husema kiserema hulima kuliko jembe jipya. Yeye ni daktari, kwa hivyo ni mzoefu wa mambo yanayolingana na hospitali na basi majibu ambayo tungepata saa hii yanafaa kusuluhisha maswali yote yaliyoulizwa. La kutatanisha sana ni majibu ya Waziri ... view
  • 13 Nov 2024 in Senate: Hon. Rebecca Miano. Samahani nimepewa taarifa isiyo ya kweli na rafiki yangu hapa. Bw. Naibu Spika, Hon. Miano hakuwa mgonjwa lakini ameamua kuenda kuweka vifaru, vifaa vya ufuatiliaji katika hifadhi ya wanyama pori. Katika taratibu ya wanaombeba na uzito, anatuchukulia kwa bei rahisi kama bei ya chumvi. Ameweka vifaru kwanza halafu Bunge la Seneti linafuata. Kwa nini hangempa mwengine jukumu hilo? Nina uhakika kuwa sio yeye anaweka vifaa hivyo. Tumepoteza nafasi ya kuongea kuhusu kinachoendelea katika serikali. Waswahili husema ukikalia kuti kavu kuanguka sio ajali na--- view
  • 13 Nov 2024 in Senate: Bw. Naibu Spika, kusiwe na mazoea ya Mawaziri kukataa kuja hapa baada ya kualikwa. Waswahili pia husema kuti la mazoea humwangusha mgema. Mawaziri hawa wataanguka kwa sababu ya kuzoea kukosa kuja hapa. Asante. view
  • 12 Nov 2024 in Senate: Asante sana Bw. Spika. Kulingana na Kanuni ya Kudumu ya 159(1) ya Bunge la Seneti, naomba kuondoa katika Ratiba, The Rice Bill (Senate Bills No.19 of 2023). Sababu kuu ni ili tushauriane na wahusika wakuu wakiwemo wakulima na wote wanaohusika ili kuwasilisa huu Mswada katika Seneti kwa safari moja. Asante sana. view
  • 27 Oct 2024 in Senate: Asante, Bw. Naibu wa Spika, kwa kunipa hii nafasi. Kwanza, ninashukuru kamati iliyokaa chini na kuhakikisha wamefanikisha maelewano kati ya fedha ambazo zinaenda kaunti zetu. Kazi inayofanywa na Maseneta ni muhimu sana. Shida ambazo wanapitia kuhakikisha kwamba pesa zinazoenda kwa gatuzi zetu zimefika ni kazi ngumu, ni kazi msalagambo. Ni kazi inayohitaji Maseneta kumakinika na kutetea gatuzi zetu. Bw. Naibu Spika, jambo la ajabu ni kwamba hizi fedha zinapofika katika kaunti zetu, magavana wengi wanajifanya kama miungu na hawawezi kulizwa maswali. Ni kama Seneti tumekuwa tingatinga; kazi yetu ni kuchukuliwa kubomoa milima na tunapomaliza kutengeneza barabara na fedha kufika kaunti ... view
  • 27 Oct 2024 in Senate: Asante, Bw. Naibu Spika. Mimi kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ukulima, Uvuvi na Uchumi Samawati ni vizuri niseme ya kwamba, miradi mingi ambayo inafanyika katika gatuzi zetu ni kama magavana wengi wamesahau kuna ukulima na uvuvi. Katika nyanja ya uchumi samawati, shida iliyoko ni kwamba, ukiangalia zile bajeti zinatengenezwa na kupelekwa bunge zetu za kaunti, huwezi pata hata moja imewekwa pesa za kutosha kwenda kwa uchumi samawati. Tumetembea sehemu mbalimbali kule uvuvi unafanyika na cha kushangaza ni kwamba, wavuvi bado wanahangaika na bado kuna fedha zinafaa ziende kusaidia wale wavuvi. Bw. Naibu Spika, mkulima ni mtu wa maana na nitaregea ... view
  • 27 Oct 2024 in Senate: Mwea. Hii inagharimu wakulima shilingi 1,200 katika kila gunia. Kama mkulima atapoteza shilingi 1,200 kwa sababu ya miundo msingi ambayo inafaa itengenezwe na gatuzi ya Kirinyaga, inamaanisha kuwa ile faida yote inapatikana kwa sababu ya kupata mbolea ya ruzuku na pembejeo za bei ya rahisi inapotea. Ningependa kumwambia gavana wangu kuwa mghala muue na haki yake umpe. Tuhakikishe kwamba huduma za barabara na miundo msingi imeboreshwa ili wakulima waweze kufaidika. Sio haya tu ambayo nilikuwa nataka kusema siku ya leo. Najua kwamba kamati nyingi zimekuwa na matatizo kubwa wakati tunawaita magavana hapa kuja kujibu maswali. Mswahili husema Mrina haogopi nyuki. ... view
  • 27 Oct 2024 in Senate: Asante, Bw. Spika wa Muda. Ninaomba kwamba, Mswada kuhusu ustawishaji wa pamba, marekebisho yaliyotoka Bunga la Taifa Mswada Nambari 5 wa 23--- view
  • 27 Oct 2024 in Senate: Thank you, Mr. Temporary Speaker, Sir. I beg to move that the National Assembly amendments to the Cotton Industry Development Bill (Senate Bills No. 5 of 2023) be now considered. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus