Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 71 to 80 of 417.

  • 27 Oct 2024 in Senate: Asante, Bw. Spika, Mswada wa pamba ambao uko mbele yetu ulimaliziwa katika Bunge la Seneti na ukaenda Bunge la Taifa ili uweze kuzingatiwa baada ya kufanya misururu ya mikutano na uhamasishaji wa umma katika sehemu tofauti na Kamati ya Ukulima, Uvuvi na Uchumi Samawati ya Seneti kuleta ripoti katika Seneti. Ilipoenda kule, kuna marekebisho ambayo Bunge laTaifa limeomba yafanywe na ukarudishwa tena kwa Kamati ya Ukulima, Uvuvi na Uchumi Samawati. Tulikaa chini na tukavalia njuga swala hilo na tukaangalia mambo yote ambayo yanafaa kuangaliwa, na tukakubaliana kwamba, marekebisho yote yaliyotoka Bunge la Taifa yanafaa kuzingatiwa. Kwa hivyo, hakuna Seneta aliyekuja ... view
  • 27 Oct 2024 in Senate: nchi, Bonda la Ufa, maeneo ya Kati, Ukambani na uende mpaka Lamu katika eneo la Pwani, pamba kwa sababu inastahimili ukame, inaweza kukuzwa katika sehemu nyingi. Ni kitega uchumi kizuri na kama tutawekesha na kuhakikisha kwamba kuna mtaji wa kukuza pamba, pembejeo zinapatikana na mbegu zinaitwa za BT, ambazo kilo moja ni zaidi ya Shilingi 7,000 lakini ni pamba nzuri sana ikipewa wakulima. Tulionelea ikiwa wakulima watapewa nafasi na pembejeo, watanufaika pakubwa na pamba. Bw. Spika wa Muda, pamba ni mmea ambao una maana sana kwa sababu, ukitoa ile pembe kwa kimombo inaitwa lint, itatengeneza nguo. Ukitoa mbegu ya ndani ... view
  • 27 Oct 2024 in Senate: Samahani, Bw. Spika wa Muda. Nitahakikisha nitafuatilia maagizo hayo. Nilikuwa namalizia kwa kusema ya kwamba, mmea wa pamba ni mojawapo ya mimea ambayo inasawasisha jamiii nyingi nchini. Wakati kuna watu ambao wanasamehewa mikopo, kuna watu wanaopewa mitaji, iwe kwamba kila Mkenya ana mmea unaompatia pesa za kujikimu. Ukiangalia takwimu ya mahali ambapo pamba inapandwa, pamba ni mmea unaoweza kustahimili ukame. Sehemu nyingi nchini zinaweza kukuzwa pamba. Pia, katika Kamati ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kuna miswada ambayo tutawasilisha kuhusu jamii za wafugaji ili kuhakikisha kwamba wananufaika na kilimo biashara. Mswada huu utakapotiwa sahihi na Rais wa Jamuhuri ya Kenya utakuwa ... view
  • 27 Oct 2024 in Senate: Wakati Rais alisema kuwa Mswada wa Sukari uko hapa uzingatiwe, tulichoma mafuta usiku kucha na mchana kutwa. Mimi kama Mwenyekiti mwenza Mheshimiwa Emanuel Wangwe tukakaa chini na kuhakikisha kuwa tumemaliza kushughulikia Mswada huo. Tunapoongea, kuna matumaini katika wakulima wa miwa, kahawa na majani chai. Kwani kama Seneta wa Bomet umeleta Mswada kujaribu kulainisha mambo ya kilimo cha chai. Matumaini ya wakulima wa ndengu yako wapi? Matumaini ya wakulima wa pamba yako wapi? Kutakuwa na matumaini kama tutakuja na kuhakikisha kwamba Miswada kama hii inapita bila siasa ambazo hazina maana. Nikimalizia, Waswahili husema wavuvi wa pweza hukutana mwambani. Sisi kama Maseneta ... view
  • 27 Oct 2024 in Senate: Samahani, Bw. Spika wa Muda. Nitamuita Seneta wa Kitui, Sen. Wambua, kuunga mkono Mswada huu. view
  • 27 Oct 2024 in Senate: Asante, Bw. Spika wa Muda. Naomba unipe dakika tatu ili nishukuru wale Maseneta ambao wameunga mabadiliko ambayo yameletwa katika Mswada huu wa pamba. Pili, ni kuwa pamba ni mmea muhimu sana kwa sababu inakuwa malighafi ya chakula cha wanyama na mafuta. Sen. M. Kajwang' ambaye pia ni mmoja wa walio The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate. view
  • 27 Oct 2024 in Senate: katika Kamati ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi tulipata kuzuru Kaunti ya Kitui na kupata ya kwamba mafuta yanayotolewa katika mbegu za pamba yanatumika kutengeneza nguvu za umeme ya kutumia kwa generator zao na pia yanatumika kwenye gari zao. Sen. M. Kajwang' ndiye mwenyekiti wa Kamati inayohusika na mabadiliko ya tabia nchini. Kwa hivyo, hilo ni jambo nzuri sana tukiweza kuipata. Pamba sio nguo pekee ila ni malighafi ya vitu vingine vingi. Bw. Spika wa Muda, kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Seneti No.66(3), naomba swali la Mswada huu liahirishwe hadi siku nyingi. Asante. view
  • 17 Oct 2024 in Senate: Asante sana, Bw. Spika. Kwanza ningetaka kumuombea afueni haraka Naibu wa Rais. Ningependa kusema hivi, fisi anapotaka kula mwanawe, husema kwamba ananuka kama mbuzi. Ni dhahiri shairi kuwa, mashtaka iliyo mbele yetu leo ni fisi anayetaka kumla mwanawe. Wakati Sen. Thang’wa alikuwa anaongeo hapa, leo ulimwambia uombe msamaha. Alikuwa amemwambia Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Jinai kwamba anapojibu, ajibu na wanao. Mashtaka ambayo imekuwa na kampuni zote zilizokuwa hapa, mingi zilikuwa za watoto wake Rigathi Gachagua. Ama kweli, chambilecho, mkuki kwa nguruwe, kwa binadamu mchungu. Kwa sababu hakuwezi kuwa na ubaguzi wa wanawe Naibu Rais, lakini kusiwe wale wengine ... view
  • 17 Oct 2024 in Senate: Mimi nimetoka Kirinyaga na ninajua mashtaka yote 11 ambayo yako hapa. Kuna jambo moja ambalo mpaka ufanye kama utadhihirisha hayo mashtaka na ni ushiriki wa umma ambao tuko na ushahidi mbele yetu. Katika ushirika wa umma ambao tuko nao mbele yetu, isipokuwa picha za maofisi za National Government – Constituency Development Fund (NG –CDF) na takwimu ambazo zimetoka katika Bunge la Kitaifa. Hii ni kwamba wale wote ambao walikuwa wametia sahihi kumuondoa Naibu wa Rais ndio walio ongoza katika ushiriki wa umma. Bw. Spika, ningeuliza itakuwaaje na itawezekanaje mtu ambaye ametia sahihi kumuondoa Naibu wa Rais anaongoza katika ushiriki wa ... view
  • 17 Oct 2024 in Senate: kuzingatia ushahidi na kuangalia kila jambo na maombi ambayo tuko nayo katika Seneti kuwa wenye haki na uaminifu. Asante sana. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus