Mohamed Faki Mwinyihaji

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 1371 to 1380 of 2123.

  • 11 May 2021 in Senate: tunabaguliwa wazi. Hata zile nafasi za kuteuliwa, kwa mfano katika Bunge, sisi kama watu wa Pwani hatuzipati. Jambo la pili ni kuwa hili swala la inclusivity lisiwe kwamba tunapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa; yaani, tupitishe halafu baadaye tunawachwa mataani kama tulivyo achwa muda uliopita. Jambo la tatu ni ofisi ya Ombudsman katika taasisi ya mahakama. Taasisi ya mahakama inatakikana iwe huru bila kuingiliwa na taasisi yote ama upande wowote katika maswala haya. Kuwepo kwa Ombudsman kwa hakika italeta mtafaruku katika taasisi ya mahakama, kwa sababu wakati Jaji atakapokuwa anaandika hukumu yake atakuwa anaangalia kwenye bega lake na kujiuliza, “Je, ... view
  • 11 May 2021 in Senate: The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate. view
  • 11 May 2021 in Senate: Bw. Spika, swala la maeneo Bunge limeleta utata kwa sababu halijatolewa kwa usawa. Tunaona kuwa maeneo mengi ambayo yanahitaji maeneo zaidi yamenyimwa. Ijapokua Mombasa inaongezewa viti vitatu vya Bunge, hiyo haitoshi kabisa. Mombasa imekuwa maradufu kwa muda wa miaka kumi na tunahitaji viti zaidi ya vitatu ambavyo tunaweza kupata hivi sasa. Pia tutakuwa tunakiuka Katiba kwa sababu swala la mipaka ya maeneo ya bunge hushughulikiwa na tume ya IEBC. Tume hii husimamia maswala ya ugavi wa maeneo bunge kwa kuzingatia wingi wa watu, mambo ya kiuchumi na usawa wa kuwakilishwa. Hii ni kwa sababu kuna maeneo mengi makubwa ambayo ni ... view
  • 11 May 2021 in Senate: Madam Deputy Speaker, Mombasa votes yes. view
  • 11 May 2021 in Senate: Mr. Speaker, Sir, on behalf of the people of Mombasa and Kenyans in general, I vote ‘yes’. view
  • 6 May 2021 in Senate: Asante Bw. Spika. Yangu yatakuwa mafupi sana. Tumefanya baadhi ya impeachment kutumia Kamati na nyingine tukafanya kupitia Bunge nzima la Seneti. Bunge nzima la Seneti linatoa uwazi zaidi kuliko kujifungia katika Kamati. Tuliona katika impeachment ya Taita Taveta na Kirinyaga, Kamati ilitoa uamuzi wake. Kwa hivyo, haina uwazi. Ninapendekeza impeachment ifanywe kupitia Bunge lote Seneti kwa sababu tutaonekana wazi na kila mtu. Makosa yatasomwa paruwanja. Kinyume na wale wanaosema kwamba gavana apewi nafasi nzuri ya kujitea--- view
  • 6 May 2021 in Senate: Bw. Spika, ninaomba unilinde kutokana na jirani wangu, Sen. Wako. view
  • 6 May 2021 in Senate: Bw. Spika, huwa tunampa heshima yote Sen. Wako anapozungumza. view
  • 6 May 2021 in Senate: Bw. Spika, zote ziko wazi kwa wananchi. Lakini, ikiwa tumekaa Bungeni maelezo yale yatakuwa yanapeperushwa moja kwa moja kupitia runinga hadi Wajir ambako watu hawataweza kuja hadi Nairobi kusikiza kesi ambayo iko dhidi ya gavana wao. Justice must not only be done, but seen to be done . Kwa hivyo, haki itatendeka wakati Bunge lote la Seneti litakapo kaa kuchunguza madai ambayo yameletwe mbele ya Bunge hili kuhusiana na gavana yeyote yule. Kanuni zetu zinafaa zibadilishwe. Gavana akipatikana na hatia, anatakikana aje kujitetea lakini madai yasipothibitishwa, Bunge halitapata fursa ya kujadili ripoti ile. Kwa hivyo, Bunge itakuwa kama conveyor belt ... view
  • 13 Apr 2021 in Senate: Asante, Bw. Spika, kwa kunipa fursa hii nijiunge na Maseneta wezangu kumpa kongole Sen. Haji Abdulkadir Mohamed ambaye alichaguliwa bila kupingwa kama Seneta wa Kaunti ya Garissa. Viatu anavyovaa ni vikubwa sana. Sisi Maseneta wenzake tuna jukumu la kumsaidia ili kuona kwamba anatekeleza jukumu lake kama Seneta wa Kaunti ya Garissa na pia kama mtumishi katika nchi yetu. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus