Mohamed Faki Mwinyihaji

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 1791 to 1800 of 2095.

  • 12 Sep 2019 in Senate: Asante, Bi. Spika wa Muda, kwa kunipa fursa hii kuunga mkono Arifa ya Sen. (Dr.) Musuruve. Ningependa kumpongeza Sen. (Dr.) Musuruve kwa kutetea haki za wale ambao hawakubahatika katika jamii, hususan wale ambao ni walemavu. Wengi wetu hatukuwa tunajua kuwa kuna mwezi maalum ambao unahadhimisha siku ya viziwi. Lakini kwa uwezo wake ametuelimisha na sisi pia tutaendelea kuwaelimisha wengine ambao walikuwa hawajui swala kama hili. Tukiangalia hata sisi katika Bunge la Seneti na Bunge la Kitaifa, hakuna mkalimani wa lugha ya ishara ambaye anatafsiri mazungumzo ambayo yanaendelea katika Bunge kwa wale ambao hawasikii katika jamii. Kwa hivyo, kama Bunge la ... view
  • 11 Sep 2019 in Senate: On a point of order, Madam Temporary Speaker. I am sorry to take you back, but this is the second time I am pressing the intervention button and have not been seen by the Speaker to speak on this issue. I do not wish to say much, but it has been a trend in this House that some of us are not seen, to be given a chance to speak. At the end of the day, we are not here to speak for ourselves. We are speaking on behalf of the electorate that elected us into this House. We should ... view
  • 11 Sep 2019 in Senate: Asante Bi. Spika wa Muda, kwa kunipa fursa ya kuchangia azimio la upanzi wa miti ambalo limeletwa Seneti na Sen. Kibiru, Seneta wa gatuzi la Kirinyanga. Ninampongeza Sen. Kibiru kwa fikira zake na kuleta azimio kama hili. Kwa sasa, kuna umuhimu mkubwa wa kupanda miti, kuboresha na kurudisha mazingira kwa sababu ya changamoto la ongezeko la joto ulimwenguni, kwa jina lingine global warming . Juzi kulitokea kibunga katika nchi ya Bahamas iliyoko kusini mwa Amerika. Sababu kubwa ilisemakana kwamba ni tatizo la ongezeko la joto ulimwenguni. Kwa hivyo, upanzi wa miti utasaidia pakubwa kupambana na tatizo la ongezeko la joto ... view
  • 11 Sep 2019 in Senate: Miradi nyingi inayofanywa katika Jamhuri yetu ya Kenya, iwe ni ya barabara au ujenzi wa majumba, yote inahitilafiana na mazingira yalivyo wakati inapoanza. Vile vile, hakuna juhudi yoyote ambayo inafanywa kwa sasa kisheria kuhakikisha kwamba yale mazingira yanaregeshwa kama vile yalivyokuwa kabla ya mradi kuanza. Azimio hili litasaidia pakubwa kulazimisha wanakandarasi kuhakikisha kwamba wameyarejesha mazingira kama vile walivyoyapata kabla ya kuanza mradi ule. view
  • 11 Sep 2019 in Senate: Bi. Spika wa Muda, vile vile, azimio hili litasaidia pia kupunguza ukosefu wa kazi kwa vijana na akina mama kwa sababu wataweza kupata fursa ya kutengeneza vipandio vya miche na vile vile, kupewa kazi ya kupanda miti katika ile miradi ambayo itafanywa na wanakandarasi katika maeneo tofauti tofauti. view
  • 11 Sep 2019 in Senate: Tumeona katika miji kama vile Mombasa kuwa hakuna misitu mikubwa isipokuwa ile ya mikoko yaani Mangrove forests . Hii pia imeingiliwa na kukatwa kiholela kwa sababu ya changamoto ya sehemu ya kuishi na miti ambayo inatumika kama kuni na katika ujenzi wa nyumba. view
  • 11 Sep 2019 in Senate: Kwa sasa kuna mradi wa Bandari ya Mombasa wa kujenga Container Terminal view
  • 11 Sep 2019 in Senate: . Ule mradi utakapokamilika sehemu kubwa itakuwa kama jangwa. Hata hivyo, The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate. view
  • 11 Sep 2019 in Senate: ikiwa watalazimishwa kupanda mikoko katika sehemu ile, itaboresha mazingira yale na kusaidia pakubwa kusafisha hewa ambayo inatumika katika mji wa Mombasa na viunga vyake, ili wananchi wapate hewa safi. view
  • 11 Sep 2019 in Senate: Mradi huu umekuja katika wakati mwafaka. Itakuwa bora ikiwa wale ambao watahusishwa nakutekeleza watahakikisha kwamba wanakandarasi wote wanalazimishwa kupanda miti ili mazingira yetu yawe bora. Katika kila sehemu ya nchi, kwa sasa kuna mradi ambao unafanyika na Serikali. Itabidi tutoe masharti ya kwamba ni lazima mwanakandarasi apande miti anapomaliza kufanya mradi. Hii inamaanisha kwamba katika kila sehemu ya nchi yetu tutaongeza eneo ambalo lina misitu na miti mizuri ambayo tumeipoteza itarejea katika jamii yetu. Litakuwa ni funzo kwa vijana wetu ambao tunatarajia kwamba watarithi yale mazingira. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus