Mohamed Faki Mwinyihaji

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 41 to 50 of 2123.

  • 1 Apr 2025 in Senate: Kama alivyozungumza Sen. Cherarkey, Kamati ya Devolution and Intergovernmental Relations itabidi iwaite mahasimu wote pamoja na Gavana wa Kaunti hiyo wiki hii ili watoe mwongozo kuhusu suala hili. Ni aibu kwamba Kaunti ya Nyamira imeshindwa kutatua masuala kama haya madogo. Nakumbuka mwaka wa 2018 tulikuwa na shida katika Kaunti ya Mombasa. Kulikuwa na watu wanaandamana kila siku kulitisha Bunge la Kaunti ya Mombasa wakisema fagia Bunge! Fagia Bunge! Tulipouliza hapa, baada ya wiki moja, gavana, na spika waliletwa hapa na matatizo haya yakamalizwa siku moja. Kwa hivyo sio masuala ya kungojea. Haya ni masuala Kamati husika inafaa kuyavalia njuga na ... view
  • 1 Apr 2025 in Senate: Asante, Bi. Spika wa Muda, kwa kunipa fursa hii. view
  • 1 Apr 2025 in Senate: The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate. view
  • 1 Apr 2025 in Senate: Asante, Mhe. Spika, kwa kunipa fursa hii ili niweze kuchangia marekebisho ya Mswada wa Sheria Endelezi yaani, Statutory Instruments (Amendment) Bill, 2024. Sheria hii inapania kuadhibu wale ambao wamepewa jukumu la kutunga sheria hizi endelezi, iwapo watakosa kuzitunga sheria hizo kwa muda ule ambao umewekwa na sheria ama muda wa miezi 12 baada ya sheria hiyo kupitishwa na Bunge, na kuwekwa sahihi na Rais, ili kutumika katika nchi yetu. Kwa sasa, kuna sheria nyingi ambazo zilipitishwa na Bunge ambazo mpaka sasa hazijaweza kutumika kikamilifu, kwa sababu sheria endelezi ambazo zilipaswa kutungwa hazijatungwa. Utungaji wa kanuni hizi endelezi, mara nyingi huwa ... view
  • 1 Apr 2025 in Senate: The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate. view
  • 1 Apr 2025 in Senate: kwamba hazikiuki Katiba na hazikiuki ile sheria kuu ambayo imempa nafasi Waziri ama jopo linalotunga sheria hizo, kuweza kuhakikisha kwamba wametunga sheria hiyo na yale mambo ambayo yanatakikana kabla ya sheria hii kupitishwa, yote yamewekwa katika sheria. Kwa hivyo, lazima yapitiwe ndio sheria hizi ziweze kutumika. Vile vile, sisi kama Bunge, tuna muda maalum ambao lazima tuutumie ili tuweze kupitisha sheria hiyo. Ikiwa hatukuweza kupitisha kwa muda ule, sheria ile inaweza kutumika bila kupitishwa na Bunge. Kwa hivyo, suala la kuwapa muda ama kutoa vigezo vikali ambavyo lazima Waziri afanye, na iwapo hatafanya, ataadhibiwa ni jambo ambalo linatilia nguvu uwezo ... view
  • 1 Apr 2025 in Senate: The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate. view
  • 1 Apr 2025 in Senate: Kwa hivyo, ilikuwa ni wizara husika waweze kuleta marekebisho haya ili waongezewe muda ndiyo waweze kuongezea sheria hizo muda. Ukiangalia katika kaunti zetu, zile sheria za ujenzi wa nyumba, nyingi zao ni zile ambazo zilikuwa zinatumika wakati kulikuwa na manispaa na mabaraza za miji. Hawajaweza kutunga kanuni mpya za kuweza kusimamia mambo ya ujenzi. Ukiangalia, majumba mengi yamejengwa upya katika miji mikuu, hata affordable housing ama zinazojengwa na serikali, lazima zipitie zile sheria za nyumba za ujenzi katika kaunti zetu. Ipo haja na ninafikiri, hili nitalizungumzia katika kamati yetu, kuangalia sheria zote za ujenzi katika kaunti zetu kama zimeweza kuambatana ... view
  • 20 Mar 2025 in Senate: Thank you, Hon. Speaker, Sir. I rise pursuant to Standing Order No.53(1), to seek a Statement from the Standing Committee on Education regarding the operations of Bandari Maritime Academy in Mombasa County. The Bandari Maritime Academy in Mombasa County is a regional center of excellence for maritime skills development in the blue economy. However, in recent times, the institution has faced several challenges, including delayed salary payments for the lecturers, irregular fee payment structures and the absence of a clear framework for placing students in industrial attachment. These challenges, if not resolved, impact the Academy's operations and daily status as ... view
  • 19 Mar 2025 in Senate: Asante, Bw. Spika kwa kunipa fursa hii kuchangia kwenye Kauli iliyoletwa Bungeni na Sen. Abass, Seneta wa Wajir. Amezungumzia masuala ya ugonjwa wa Kala-azar . Ugonjwa huu umeingia katika Kaunti za kaskazini. Wiki iliyopita tulizungumzia Kaunti ya Marsabit, hivi sasa tunazungumzia Kaunti ya Wajir. Zamani, afya haikuwa imegatuliwa. Ilikuwa ni shida kupata wataalamu wa kupambana na majanga kama haya kwa muda mfupi. Kaunti zetu hazijafanya mipango yoyote kuhusiana na magonjwa kama haya. Inakuaje ugonjwa unaingia, wananchi wanafariki, sio mmoja bali wawili watatu. Ripoti ya magazeti ilisema kuwa watu kadhaa wamepoteza maisha yao kwa sababu ya ugonjwa huu. Ni ugonjwa ambao ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus