3 May 2023 in Senate:
Hii ni Serikali iliyochaguliwa kwa imani kwamba itaondoa mauwaji ya kimbari na kuleta usalama kwa mwananchi. Leo ni masikitiko kwamba ndugu yangu Sen. Chute kutoka Mandera aliyechaguliwa kwa chama cha United Democratic Alliance (UDA), analia kwamba watu wake wanapata shida na wanakufa wakati Serikali inasumbua viongozi wa upinzani.
view
3 May 2023 in Senate:
The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate.
view
3 May 2023 in Senate:
Marsabit, samahani. Lakini Marsabit na Mandera kwote usalama ni duni. Huwezi tembea kama tunavyotembea Mombasa wakati wowote, masaa 24 bila shida yeyote. Hizi ni sehemu ambazo zilipiga kura kwa Serikali ya UDA---
view
27 Apr 2023 in Senate:
Asante, Mheshimiwa Spika, kwa kunipa fursa hii kuwakaribisha wawakilishi Bunge la Kaunti za Kilifi na Kiambu.
view
27 Apr 2023 in Senate:
The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate.
view
27 Apr 2023 in Senate:
Mheshimiwa Spika, wiki iliyokwisha, tulikuwa katika Kaunti ya Kilifi nilipomzindikiza Sen. Mdazayo, kuhutubia Bunge lile. Makaribisho waliotupatia wawakilishi Bunge wa County ya Assembly ya Kilifi yalikuwa murwa sana. Leo nimewakaribisha katika Kamati ya Delegated Legislation ambao ndio wamezuru. Kusema ukweli, ni Wabunge na maafisa ambao wako tayari kusoma kutoka Bunge letu. Mheshimiwa Spika, ni masikitiko kwamba, kwa sasa, Kaunti ya Kilifi imegubikwa na msiba mkubwa kutokana vitendo vinanvyoendelea vya kanisa mbili ambazo zinahubiri sehemu hiyo. Tunawaombea Mungu wakaazi wa Kaunti ya Kilifi. Mungu awape subira na nguvu ya kupambana na vitendo vya makanisa kama hayo ambayo kwa hakika ni aibu ...
view
27 Apr 2023 in Senate:
Asante Mheshimiwa Spika. Nimesimama kwa mujibu wa Kanuni ya Kudumu ya 53(1), kuomba Kauli kutoka kwa Kamati ya Kudumu ya Barabara, Uchukuzi na Makao, kuhusu kusimama kwa ujenzi wa barabara ya mzunguko wa Barclays Mombasa hadi makutano ya Jomvu, barabara ya Magongo hadi makutano ya Jomvu na barabara ya makutano ya Jomvu hadi Standard Gauge Railway (SGR), katika Kaunti ya Mombasa. Katika taarifa hiyo, Kamati iangazie yafuatayo-
view
27 Apr 2023 in Senate:
(1) Iarifu Seneti lini wakandarasi wa ujenzi wa barabara hizo tatu watarudi kuendelea na mradi wa ujenzi wa barabara hizo, ikikumbukwa kwamba, muda mahsusi uliotangazwa kuchukua ujenzi huo umekamilika.
view
27 Apr 2023 in Senate:
(2) Iwapo Kenya National Highways Authority (KENHA) inatambua kwamba kutokamilika kwa barabara hizo, imekuwa kero kwa wahudumu wa usafiri na wananchi kwa jumla katika maeneo hayo. (3) Ibaini ni hatua gani Kenya National Highways Authority (KENHA) itachukua dhidi ya wanakandarasi hao, walioondoka kwenye maeneo ya kazi bila kukamilisha mradi huo, ikizingatiwa kwamba hasara kubwa zinazokadiriwa na kampuni za uchukuzi, kwa kuharibika kwa magari yao kutokana na ubovu wa barabara hiyo. Mheshimiwa Spika, jumamosi iliyopita, wasafiri wengi waliokuwa wanakwenda
view
27 Apr 2023 in Senate:
walichelewa kwa sababu barabara ya kutoka Barclays mpaka Jomvu, maeneo ya Kibarani ilifurika, kusababisha magari kutoweza kupita. Wengi waliokuwa wanasafari kuelekea SGR na Airport walitatizwa na mvua kubwa iliyosababisha maji mengi kwenye barabara hiyo. Asante, Mheshimiwa Spika
view