12 Apr 2023 in Senate:
The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate.
view
12 Apr 2023 in Senate:
Bunge la Seneti likapeleka Kamati kwenda kuchunguza na ikapatikana kwamba ni kweli waliwakusanya wale randa randa wa mjini wote na wakaenda wakawatupa msituni. Ni mambo ambayo yamefanyika. Ni lazima tuwakemee sisi kama Maseneta katika nchi yetu ya Kenya.
view
12 Apr 2023 in Senate:
Kwa kumalizia, ninampongeza Sen. Mungatana kwa kuleta Mswada huu ambao utasaidia pakubwa kuziamsha kaunti zetu ambazo haziangalii sana maswala ya haki. Wanaangalia mambo madogo madogo ambayo kwa muda mrefu, hayapeleki mbele haki za wananchi katika kaunti zile.
view
11 Apr 2023 in Senate:
Asante, Bwana Spika, kwa kunipa fursa hii kuunga mkono Ardhilhali iliyoletwa katika Bunge hili na Seneta wa Kaunti ya Nandi, Sen. Cherarkey. Masaibu yaliyokumba familia ya mwendazake Mhe. Seroney ni ya kusikitisha katika nchi yetu ya Kenya kwa sasa. Hii ni nchi ambayo ina sheria na mwongozo, lakini hatuwaangalii viongozi ambao wamepita katika kuhudumia nchi yetu kwa siku za nyuma. Ningependa kuwakumbusha katika Bunge hili na lililopita tuliupitisha Mswada wa kulipa kiinua mgongo madiwani waliokuwa wamehudumia katika baraza za miji na manispaa ya zamani kabla ya kuja katika ugatuzi lakini hadi sasa imekuwa hadithi ya nenda rudi. Tutaweka pesa mwaka ...
view
15 Mar 2023 in Senate:
Thank you, Mr. Speaker, Sir. I wanted to inform the House and Sen. Omogeni that the Senate was the subject of an editorial this morning by The Daily Nation Newspaper. Therefore, if you think that some of us think that this matter is trivial, look at the editorial of The Daily Nation Newspaper today. I thank you.
view
15 Mar 2023 in Senate:
Bw. Spika, asante kwa kunipa fursa hii. Kuna msemo wa Kiswahili unaosema, ‘Nyani haoni umbile.’ Yaani, nyani haoni umbo lake. Ningetumia lugha nyingine lakini sio ya kistaarabu.
view
15 Mar 2023 in Senate:
Bw. Spika, tumesikia kauli zilizotolewa na Maseneta kadha wa kadha, akiwemo, Sen. Orwoba, ambaye anatoka hivi sasa.
view
15 Mar 2023 in Senate:
Itakumbukwa kwamba wiki tatu zilizopita, Sen. Orwoba, alikuwa hapa Bungeni akiwa ameingia katika hada zake. Sisi kama Maseneta tulimheshimu na tukamvumilia katika ile hali aliyokuwa nayo. Leo ni masikitiko kwamba, Sen. Orwoba anaweza kusimama katika Bunge hili na kukemea haki ya Maseneta wa upinzani, wakidai haki zao. Bw. Spika, mambo mengi yamezungumzwa. Nimeskia pia Kiongozi wa Walio Wengi akisema kwamba, tunaharibu wakati wa Bunge. Lakini, haki ni haki. Haiwezekani kwamba haki zetu sisi zikataliwe katika Bunge tuliochaguliwa kuwakilisha watu wetu. Ikiwa sisi kama Seneta, haki zetu zinakataliwa, je, itakuwa vipi kwa wale ambao tunaowaakilisha? Bw. Spika, ruling imeletwa mbele yako. ...
view
15 Mar 2023 in Senate:
Bw. Spika, ninashangaa na wakili Sen. Cherarkey ambaye nimemfunza hapa bungeni. Anatuaibisha.
view
15 Mar 2023 in Senate:
The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposes only. Acertified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate.
view