17 Nov 2022 in Senate:
counties. Now, they should be given the equipment on a need basis, so that each county chooses which equipment they want for their hospitals.
view
17 Nov 2022 in Senate:
The donor funds covered by this Bill are very essential. Contracts have been negotiated and signed but the funds are not being released because we have not passed this law to enable the Government to release the funds. This discourages the donors who have done a lot to facilitate the availability of those funds to county governments. They have been impeded by the failure to pass this law. This is a separate Fund. Therefore, there is need to prepare a different Bill to operationalize the Equalization Fund.
view
17 Nov 2022 in Senate:
Mr. Deputy Speaker, Sir, as you are aware, the Fund is provided for under Article 204 of the Constitution. It is a distinct Fund. Therefore, we cannot lump it with the County Governments Additional Allocations Bill, 2022. This is because the utilization of these Funds is not based on any conditions. There are no conditions imposed as a result of utilization of the Equalization Fund. The Fund also creates a 3 per cent Monitoring Fund, which is also not provided under the Equalization Fund. Therefore, there is likely to be a conflict if it is included in the County Governments ...
view
16 Nov 2022 in Senate:
Bw. Spika, asante kwa kunipa fursa hii kuchangia maombi ya Taarifa kutoka kwa Sen. Osotsi. Kama tunavyojua, nchi yetu ilikumbwa na janga la Korona na vile vile, baada ya hapo kukawa na wasiwasi kutokana na uchaguzi uliofanyika mnamo 9th Agosti, 2022. Yote hayo yaliadhiri uchumi, hususan utalii kwa sababu utalii unapendelea mazingira ambayo yako na utulivu na usalama. Bw. Spika, sasa kwa vile uchaguzi umekwisha na uchumi umeanza kufukuka, Wakenya wengi, mashirika na wafanyikazi wa serikali wamepata fursa ya kwenda kwenye mikutano, ili kuweza kujadili miradi na maswala mengine ya kuendesha Serikali. Hili jambo la kuzuia mikutano kufanyika katika hoteli ...
view
16 Nov 2022 in Senate:
The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate.
view
16 Nov 2022 in Senate:
sababu ya wasiwasi. Sasa hivi, Serikali imepiga marufuku mikutano kufanyika katika mahoteli kama hayo. Bw. Spika, iwapo agizo hili litatekelezwa, itaamaanisha ya kwamba wale wawekezaji wa biashara za hoteli, watakosa kupata faida yoyote, mwaka huu wa 2022. Agizo hili litaadhiri uchumi kwa sababu mapato yanayotokana na utalii yataweza kupungua na hata yale malengo ya Serikali ya kukusanya pesa walizotarajia mwezi wa sita, bajeti iliposomwa, hayataweza kutimizwa. Ningependa swala hili liangaliwe kwa haraka, kwa sababu tayari tunafikia mwisho wa mwaka na wangependelea angalau wapate faida kidogo, ili waweze kuregesha raslimali zao mwaka huu wa 2022. Asante, Bw. Spika.
view
16 Nov 2022 in Senate:
Asante Spika wa Muda, kwa kunipa fursa ya kuchangia Hoja iliyoletwa na Sen. Mungatama, MGH, Seneta wa Kaunti ya Tana River. Masuala ambayo ameyazungumzia Sen. Mungatana, MGH ni mazito sana ikizingatiwa kwamba maji ni uhai na tumekuwa na maafa ya mara kwa mara katika eneo la Mto Tana, ikiwemo ukame ambao sasa unaendelea pakubwa. Vilevile, kuna mafuriko ambayo yanatokea mara kwa mara. Bw. Spika wa Muda, Mto Tana ni sehemu ambayo iko na nafasi kubwa ya kuinua uchumi wa Kaunti yake na hata nchi nzima kwa jumla. Hii ni kwa sababu mahali ambapo Mto Tana unaingia katika Bahari ya Hindi, ...
view
16 Nov 2022 in Senate:
The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate.
view
16 Nov 2022 in Senate:
Ninaunga mkono maoni ya Mhe. Ali Roba, kwamba kufanywe tena uchunguzi upya kuhusiana na mradi huu. Tuangalie hatari gani imeletwa kwa mazingira na wananchi wote, baada ya kuidhinishwa kwa mradi huu kuanzia sehemu ya juu kule ambako maji yanakwenda, mpaka sehemu ya chini ambayo ni mtoni, ambako maji yale yalikuwa yanafika kusaidia wananchi ambao wako katika sehemu zile. Bw. Spika wa Muda, mradi wa Galana-Kulalu ungesaidia pakubwa maswala haya. Mradi wa Bura ambao pia uko katika Kaunti ya Tana River, pia ungesaidia. Hii miradi yote imesalia kuwa kitendawili. Hadi sasa, miradi hii haijaleta latija ambayo iliyotakiwa. Kwa mfano, kilimo cha ...
view
15 Nov 2022 in Senate:
Asante Bw. Spika kwa kunipa fursa hii kuunga mkono Ripoti ambayo imeletwa Bungeni ya uteuzi wa wagombea wa ubunge wa EALA. Kwa hakika wote ambao wameteuliwa wanatajiriba. Ni vizuri tuchague watu ambao watakuwa na uwezo wa kusongesha mbele Bunge hili la Afrika Mashariki. Bw. Spika, tukiangalia katika zile taasisi za East Africa Cooperation, Mahakama ya East Africa imefanya maamuzi ambayo yamesaidia maswala ya haki za binadamu katika maeneo yetu kwa sehemu kubwa kuliko yale ambayo yamefanywa na Bunge hili. Hayo yote yametokana na maswala kwamba wale wanaoenda kutuwakilisha ni watu ambao wanaenda kutafuta kazi. Si watu wanaoenda kuangalia yale maswala ...
view