Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 131 to 140 of 257.

  • 5 Mar 2019 in National Assembly: ya uchache wa pesa ilhali wamebandikwa majukumu kwamba kuna pesa wanapewa za Serikali katika kusimamia maeneo haya. view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Kuna changamoto ambazo tunapata kama Kamati katika suala la kuridhisha haya mambo kwa sababu Wabunge wanalalamika. Tuko mwezi wa tatu na utapata ya kwamba maeneo Bunge hayajapata kabisa ule mgao wa NG-CDF wa mwaka huu. Wengine wamepata kama Ksh10 milioni. Wabunge wenzangu wanalalamikia Kamati ya NG-CDF. Ukweli ni kwamba sisi kama Kamati, tunajitahidi vilivyo kuhakikisha kwamba Wabunge wamepata pesa kwa sababu tunaelewa hali hii. Matatizo yako katika Wizara ya Fedha katika kutoa pesa hizi. Ningewaambia Wabunge wenzangu kwamba tunajitahidi kuhakikisha tumefuatilia jambo hili kwa sababu tunajua zile changamoto Wabunge wanapitia katika maeneo Bunge yao. Wizara ya Fedha haijatilia maanani kuhakikisha ... view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Ningependa kusema ya kwamba hapo awali, mgao wa NG-CDF ulikuwa unaangazia masuala ya umaskini na wingi wa watu katika sehemu. Waheshimiwa wanalalamika kuhusu suala hili. Tutafute njia ya kuhakikisha kwamba kuna sehemu ambazo zinahitaji hizi fedha zaidi kuliko sehemu zingine. Ninaunga mkono jambo hili, lakini ifahamike pakubwa kwamba kuna miegezo mingine ambayo tunafaa kuangalia. Kwa mfano, idadi ya watu siyo suala la kuzingatiwa kikamilifu. Suala la kuzingatiwa kikamilifu ni umaskini. Unaweza kupata idadi ya watu katika sehemu ni kidogo lakini umaskini ni mkubwa sana. Kwa hivyo, tuwe waangalifu kama Waheshimiwa katika kutaka kurekebisha haya mambo tusije tukadhulumu sehemu zingine na ... view
  • 27 Feb 2019 in National Assembly: Ahsante, Mhe. Naibu Spika wa Muda. Ningependa kuungana na wenzangu katika kuwapongeza wanakamati kwa kazi yao nzuri ambayo wamefanya kuhusiana na Ripoti hii ambayo imeletwa Bungeni. Kwa kweli, wengi wamechangia kuhusiana na masuala haya, na haswa kuhusu pesa za NG-CDF – Hazina ambayo imekuwepo kuanzia mwaka wa 2003. Ni vyema Wakenya wafahamu utaratibu wa NG-CDF na mabadiliko ambayo yamefanyika katika NG-CDF. Ukweli ni kwamba fedha hizi, kuanzia mwaka wa 2003, zimeleta mabadiliko makubwa nchini Kenya. Leo kuna mengi yanayozungumziwa kuhusiana na maendeleo na mengineo lakini, ukweli ni kwamba, fedha hizi zimeonekana katika sehemu za mashinani. Fedha hizi zimeleta maendeleo makubwa ... view
  • 27 Feb 2019 in National Assembly: Tatizo ambalo bado lipo mpaka sasa ni kwamba Wakenya bado wanahitaji maendeleo. Changamoto ni nyingi. Ni lazima Serikali ifahamu kikamilifu. Miongoni mwa mbinu zilizotumika kugawanya fedha hizi katika maeneo Bunge hapo ni idadi ya watu na hali ya umaskini katika sehemu hizo. Utakubaliana nami kwamba baadaye, mbinu hiyo ilibadilishwa na kila eneo Bunge likawa linapokea kiwango sawia cha fedha kutoka NG-CDF. Hakuna eneo Bunge linalopata pesa nyingi kuliko lingine. Ukweli ni kwamba maeneo Bunge hayafanani. Kuna sehemu ambazo zimeendelea na kuna sehemu ambazo bado kuna udhaifu na umasikini mkubwa. Mbali na kusema kwamba tuangalie idadi ya watu, sidhani ni kiegezo ... view
  • 27 Feb 2019 in National Assembly: Bajeti ya Kenya inapangwa. Ni kama kusema kuwa fedha hizi zinazopelekwa katika Wizara ya Elimu, matumizi yake ni yale ambayo yamepangiwa miongoni mwa matumizi ya NG-CDF. Kwa maoni yangu, ningesema kwamba, Serikali izingatie pakubwa. Ni kama kutumia pesa kwa njia moja. Leo utapata kwamba, eneo Bunge linahitaji kujengewa madarasa. Baada ya pesa zile kupatiwa NG-CDF, zingine zinapatiwa wizara katika kuifanya kazi hiyo hiyo. Fedha hizi mwishowe hazionekani dhamani yake katika wizara hizi. Kila mmoja wa Wabunge hawa anaweza kutoa ushahidi mkubwa kuwa zile pesa tunazoziona ni zile zinazotumika kwa NG-CDF. Zile ambazo zinaenda katika wizara halafu wizara inapendekeza kuwa kujengwe ... view
  • 27 Feb 2019 in National Assembly: Ni lazima tuzingatie haya pakubwa. Nchi yetu iko na malengo na maono katika kuendeleza elimu, lakini changamoto ni nyingi. Sisi Wabunge ndio ambao tunapambana na changamoto hizi katika maeneo Bunge yetu mashinani. Serikali imepanga kwamba watoto wasome bure na madarasa yajengwe. Lakini utapata kwamba mipangilio hii Serikali imependekeza haijakamilika. Utapata kwamba katika shule moja, darasa moja lina watoto kati ya mia moja na mia mbili kwa sababu elimu ni bure. Hii ni hali ya kusikitisha. Ingekua ni vyema kwamba, kabla hawajakuja na mipangilio hii, wangefanya utafiti kikamilifu katika maeneo Bunge yote katika kaunti zote na kujua yale yanayohitajika kukamilishwa au ... view
  • 27 Feb 2019 in National Assembly: Swala la kutaka kufanya mambo na wakenya halafu baadaye kuona wanadanganywa, sioni kama yatatatua matatizo yetu. Kuna dharura kubwa ya Serikali kuzingatia. Ndio kwa sababu tunataka wanafunzi au watoto wetu wa kila sehemu waende shule. Tunataka wazazi wasaidiwe mizigo ya kulipa karo shuleni. Ningependa kuambia Bunge hili kwamba, hadi tunavyozungumza hivi sasa, mipangilio hii haijaweza kuwa na mwongozo kikamilifu kwa sababu matatizo mengi hayajaweza kusuluhika. Ningependekeza kama wenzangu walivyotoa maoni kuhusu fedha za NG-CDF. Nina imani kwamba utafiti huu umefanyika na umeonekana kuleta mabadiliko makubwa. Fedha hizo ziongezwe katika kuendesha maswala haya ya maendeleo katika maeneo Bunge yote ya Kenya ... view
  • 27 Feb 2019 in National Assembly: Ningependa kuunga mkono Ripoti hii ambayo imeletwa Bungeni. view
  • 19 Feb 2019 in National Assembly: Asante sana, Mhe. Spika wa Muda. Ningependa kuungana na wenzangu kuunga mkono marekebisho haya ya Mswada huu kuhusu serikali za kaunti. Tunapaswa kama Wakenya kujipongeza wenyewe na kuipongeza nchi hii kwa Katiba tuliyopitisha kuhusiana na mambo mengi, mojawapo ikiwa suala la serikali za kaunti. Leo marekebisho tunayofanya hapa ni kutokana na hofu kubwa kuwa serikali za kaunti kuonekana namna zitakavyojiendeleza na namna zitakavyodumu katika kuendeleza mambo yao. Ndiposa mwongozo huu tuko nao leo waonyesha hofu iliyokuwapo ni kwamba serikali 47 za kaunti huenda zizifanye vyema ama kutokuwa na usawa. Ndiyo sababu kukawekwa mikakati kama hii ili mambo haya yatakapojitokeza ifahamike ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus