Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 141 to 150 of 515.

  • 28 Feb 2024 in National Assembly: Watu wangu wa Msitu wa Boni, Kiunga, Faza Ward na Mtangawanda ambao hawajui watu wakubwa serikalini hawapati nafasi hizi. Kwa hivyo, huu Mswada ukipitishwa, itakuwa haki. Kama mwalimu wa kule Kiunga anastaafu akifikisha miaka 60, wale wa huku wanaojua watu wakubwa Serikalini wastaafu wakifikisha miaka 60 pia. Lakini, sio kwa kuwa anajua mtu, basi yeye ndio anaongezewa miaka. Ninaunga mkono sana Mswada huu. Wakenya wote wastaafu wakifikisha miaka 60. view
  • 28 Feb 2024 in National Assembly: Pia, ninaunga mkono vile Mhe. alivyosema hapa kwamba matayarisho yafanywe mapema kwa sababu inachukuliwa kama kigezo ili mwingine aendelee kufanya kazi na kusema hakuna mwingine anawezakufanya taaluma yake. Ni vizuri vile ilivyosemwa kwamba kabla yule mwenye taaluma ile hajaondoka, mwingine atayarishwe achukue hiyo nafasi yake. Isiwe kiegezo cha kukosesha wengine kazi kwa kumpendelea mtu mwingine. Pia, ninaunga mkono pale anaposema wale makatibu washikilizi wasifanye zaidi ya miezi sita. Kusema kweli, tunapoteza sana kwa sababu wakikaa pale, utaona katibu amekuja kazini hata hana morali kwa sababu hajui kesho kutakuwa vipi. Katibu ajue akienda sana ni miezi sita. Aandikwe au atolewe. Kwa ... view
  • 28 Feb 2024 in National Assembly: hivyo watu wasishtuke wakidhani kuwa ni kwa watu wote Kenya. Kuna wale wengine hawapitii huku. Wao wataendelea na zile sheria zao. view
  • 28 Feb 2024 in National Assembly: Ahsante, Mhe. Naibu Spika. view
  • 14 Feb 2024 in National Assembly: Ahsante sana, Mhe. Spika wa Muda kwa kunipatia nafasi hii ili nichangie. Kwanza, ningependa kumpongeza Mbunge Mwakilishi wa Wanawake wa Kaunti ya Nairobi, Mhe. Esther Passaris, kwa kuleta Hoja hii. Pia, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwa katika Eneo Bunge langu la Lamu Mashariki, hakujawahi kutokea mauaji kama haya ya kinyama. Wanaume wetu ni wastaarabu; hawaui wanawake. Nachukua nafasi hii kuwapongeza wanaume wote wa Lamu Mashariki. Ni kweli Lamu The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor view
  • 14 Feb 2024 in National Assembly: Mashariki inakumbwa na shida nyingi sana, lakini, alhamdulilahi, tunashukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwa kwetu hatujashuhudia mauaji ya wanawake. Hivi leo tunalia na Wakenya wengine. Si sawa wanawake kuuawa. Pia si sawa sisi kulaumu tu Serikali. Kwa maoni yangu, tunazo sheria nyingi kuhusu jambo hili, lakini hazitumiki. Jambo ambalo nataka kutilia mkazo sana ni namba ile ya dharura ya 1195. Wakenya wengi hawajui kuwa kuna namba ya dharura inayoshughulikia maswala haya. Namba hii hutumika masaa 24, na pia inapigwa bila malipo. Unapopatikana na tatizo lolote kama la ubakaji, ukipiga namba hii, unapata nusra na watu wa kukusaidia hata kama ni kwa ... view
  • 7 Dec 2023 in National Assembly: Asante, Mhe. Spika wa Muda, kwa kunipatia nafasi ili nichangie Hoja hii. view
  • 7 Dec 2023 in National Assembly: Asante, Mhe. Spika wa Muda, kwa kunipatia nafasi ili nichangie Hoja hii. view
  • 7 Dec 2023 in National Assembly: Suala la ugaidi lina utata sana. Halina dini wala kabila. Nimetoka Lamu, ambayo imekuwa katika vyombo vya habari mara nyingi kwa sababu ya mambo ya ugaidi. Wengine wamekuwa kwa vyombo vya habari kwa sababu ya utaalamu fulani, lakini sisi saa zote tukitajwa kwa habari ni kwa sababu ya mambo ya ugaidi. Eneo Bunge langu linaathirika sana na mambo ya ugaidi. Suala hili likizungumzwa, tunazungumza kutoka ndani mwa roho zetu kwa sababu ni mambo ambayo tunajua yanatuathiri. Kuna mtu mmoja ambaye ameuawa leo. Ninatoa pole zangu, kisha niendelee kuchangia Hoja hii. view
  • 7 Dec 2023 in National Assembly: Suala la ugaidi lina utata sana. Halina dini wala kabila. Nimetoka Lamu, ambayo imekuwa katika vyombo vya habari mara nyingi kwa sababu ya mambo ya ugaidi. Wengine wamekuwa kwa vyombo vya habari kwa sababu ya utaalamu fulani, lakini sisi saa zote tukitajwa kwa habari ni kwa sababu ya mambo ya ugaidi. Eneo Bunge langu linaathirika sana na mambo ya ugaidi. Suala hili likizungumzwa, tunazungumza kutoka ndani mwa roho zetu kwa sababu ni mambo ambayo tunajua yanatuathiri. Kuna mtu mmoja ambaye ameuawa leo. Ninatoa pole zangu, kisha niendelee kuchangia Hoja hii. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus