Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 141 to 150 of 257.

  • 19 Feb 2019 in National Assembly: Asante sana, Mhe. Spika wa Muda. Ningependa kuungana na wenzangu kuunga mkono marekebisho haya ya Mswada huu kuhusu serikali za kaunti. Tunapaswa kama Wakenya kujipongeza wenyewe na kuipongeza nchi hii kwa Katiba tuliyopitisha kuhusiana na mambo mengi, mojawapo ikiwa suala la serikali za kaunti. Leo marekebisho tunayofanya hapa ni kutokana na hofu kubwa kuwa serikali za kaunti kuonekana namna zitakavyojiendeleza na namna zitakavyodumu katika kuendeleza mambo yao. Ndiposa mwongozo huu tuko nao leo waonyesha hofu iliyokuwapo ni kwamba serikali 47 za kaunti huenda zizifanye vyema ama kutokuwa na usawa. Ndiyo sababu kukawekwa mikakati kama hii ili mambo haya yatakapojitokeza ifahamike ... view
  • 19 Feb 2019 in National Assembly: panapotokezea matatizo tuna mwongozo kamili wa kuhakikisha kwamba matizo hayaleti athari ama hayatatanishi utaratibu ambao unaendelea hivi sasa wa kisheria. Naunga mkono na naungana na wenzangu kwa kupendekeza na kuhakikisha ya kwamba haya mambo na utaratibu huu umepitishwa. Ningependa kukomea hapa. Asante. view
  • 19 Feb 2019 in National Assembly: panapotokezea matatizo tuna mwongozo kamili wa kuhakikisha kwamba matizo hayaleti athari ama hayatatanishi utaratibu ambao unaendelea hivi sasa wa kisheria. Naunga mkono na naungana na wenzangu kwa kupendekeza na kuhakikisha ya kwamba haya mambo na utaratibu huu umepitishwa. Ningependa kukomea hapa. Asante. view
  • 13 Feb 2019 in National Assembly: Asante, Mhe. Spika wa Muda. Kwanza ningependa kumushukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia kurudi tena hapa Bungeni kwa mwaka wa 2019 baada ya likizo ndefu. view
  • 13 Feb 2019 in National Assembly: Ningependa kuungana na wenzangu kuunga mkono mapendekezo haya ya namna fedha za umma zitadhibitiwa kiumakini na kiuangalifu. Kwa kweli, hili ni suala nyeti. Tunapolizungumzia ni lazima tulifahamu kwa namna zote. Kwanza, nataka tufahamu takribani asilimia 25 za fedha zinazopatikana kutokana na mapato ya nchi zinaelekezwa kwa serikali za kaunti. Hivyo basi kuna umuhimu wa kuwa na mwongozo kuhusiana na pesa hizi wakati Serikali inazipeana kwa kaunti. view
  • 13 Feb 2019 in National Assembly: Vile vile, tumeshuhudia mara nyingi sana nchi hii ikilalamika kuhusiana na masuala ya uchumi na matatizo mengineo. Naamini pakubwa haya yanasababishwa na hali ya kutodhibiti kile tunachopata kwa uangalifu. Asilimia 25 ambayo inaenda kwa kaunti sio pesa kidogo. Lakini utapata ya kwamba pesa hizi zinazoenda kwa kaunti, kaunti nyingi bado zinalalamika kuhusiana na miradi na maendeleo. Naamini pakubwa kwamba kama utaratibu huu ambao tuaujadili hapa utaweza kutumika kiusawa, nina imani kwamba matatizo kama haya hayatashuhudiwa mbeleni. Ukweli ni kwamba nchi hii ina umuhimu mkubwa wa kuhakikisha ya kwamba fedha za umma zimedhibitiwa na zimetumika kiusawa na kiuangalifu. view
  • 13 Feb 2019 in National Assembly: Utakubaliana nami kwamba matatizo haya yanapatikana kwa wahusika wakuu wanaoendesha mwongozo kama huu ambao tunaujadili hapa Bungeni. Ni matumaini yangu makubwa na nina imani kwamba kama mwongozo huu utafuatwa kikamilifu na vile unavyotakikana, basi fedha za umma zitadhibitika na matarajio makubwa ya wananchi yatapatikana. view
  • 13 Feb 2019 in National Assembly: Vile vile, mbali ya kwamba tunayazungumzia haya leo ama tunayajadili marekebisho haya, ni lazima tukubali matatizo yako na ni sisi tunayasababisha kupitia serikali za kaunti ama Serikali Kuu. Utapata kwamba utaratibu huu ambao tunaujadili hapa, wengine wanautumia kama sababu kwa mambo yao ya kibinafsi. Mfano ni namna serikali za kaunti zinavyotaka kutumia pesa zao. Lakini hapa katikati, hofu ni kwamba kuna baaadhi ya Wakenya ambao ni wahusika katika kutumia utaratibu huu. Wanatumia mbinu za kusikitisha badala ya kufanya mambo kiutaratibu hasa kwa kuzingatia mwongozo huu ambao tunazungumzia. Kuna miradi ambayo inahitaji kufanywa kila mwaka lakini hucheleweshwa kwa sababu ya mwongozo ... view
  • 13 Feb 2019 in National Assembly: kwamba tumetembea na mwongozo huu kikamilifu. Tusilete mvutano kati ya wahusika na kaunti. Kuna wakati pengine mkandarasi amefanya kazi yake kwa utaratibu lakini inapofika wakati wa kulipwa, kwa sababu ya vigezo hivyo ambavyo tumeweka hapa, serikali ya kaunti inasema kwamba utaratibu ndio una matatizo. Hivyo basi, mkandarasi anachelewa kupewa pesa zake kwa sababu kama hiyo. Ninaamini kwamba ni mwongozo mzuri. Wakenya wanahitaji huduma bora. Mbali na hayo, ninaamini pakubwa huduma hizi zitapakitana ikiwa kutakuwa na mwongozo kamilifu na viongozi husika wataweza kumakinika na kuhakikisha wamekubali kufuata utaratibu na sharia zilizowekwa. view
  • 13 Feb 2019 in National Assembly: Magavana tunawajua. Sifa za wengi wao zinajulikana. Siyo wote wenye sifa za kupendeza. Udhaifu upo ndani ya baadhi ya ndugu zetu. Kutokana na hali hii ambayo tunajadili sasa hivi, ni vyema kuhakikisha kwamba mwongozo huu umewekwa vikwazo vya kisheria namna inavyotakikana. Hivyo, tutahakikisha kwamba yeyote ambaye ni mhusika katika kaunti ni mhusika wa kuendeleza kaunti. Masuala ya fedha yatadhibitiwa kwa njia ya furaha kubwa. Serikali ya kitaifa yafaa kuhakikisha kwamba imepeana mwongozo kwa serikali za kaunti kuhusu matumizi ya fedha. Tumeshuhudia mara kadhaa matatizo katika kaunti tofauti tofauti. Mimi naona yamesababishwa na hali ambayo haikuwa hapo mbeleni ya kuweka utaratibu ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus