27 Oct 2024 in Senate:
yalikuwa ni majadiliano kulingana na vile ambavyo hatukuwa tumeelewana katika ugavi wa pesa zinazoenda kwenye serikali zetu za mashinani. Majabali wetu waliokuwa katika hii Kamati wakiongozwa na Sen. Ali Roba, walikuwa Sen. Sifuna, Sen. Murgor, Sen. Faki, Sen. Veronica Maina, Sen. Onyonka, Sen. Wamatinga, Sen. (Prof.) Tom Ojienda Odhiambo, SC, Sen. Mungatana, na Sen. Oketch Gicheru. Tuliwapeleka majabali hawa ambao walifanya bidii walivyoweza kujadiliana na kupitisha pesa zile. Kulingana na matokeo ya awali tulikuwa tumesema tupeleke Shilingi 400 bilioni kwenye serikali za kaunti 47 zote. Wagawanye taratibu ili kila kaunti ifaidike na zile pesa. Lakini kwa sababu ya sintofahamu tofauti ...
view
27 Oct 2024 in Senate:
kuhudumia mtu aliyepata ajali ama mtu anayetaka kulazwa katika vile vyumba ambavyo vinaitwa Intensive Care Unit (ICU) au chumba cha wagongwa mahututi; chumba ambacho mtu anaweza kupata madawa na hatimaye akatoka katika ile hali yake ya kimahututi na akaja akiwa mzima tena na akarudi kwa jamii yake akiwa na afya njema. Tunasema hiyo ndiyo sababu tunasisitiza sana kwamba pesa nyingi zipelekwe kwa hospitali ili wakenya wawe na afya nzuri, nchi itakuwa na maendeleo zaidi. Bw. Spika wa Muda, vile vile kuna hali za mawasiliano. Pesa hizi si za kutumia vile mtu anavyotaka, ila tuone hali za mawasiliano. Barabara zile za ...
view
27 Oct 2024 in Senate:
Tunaona simanzi zinatandaa katika familia tofauti tofauti kwa sababu ukiulizwa unasema mimi sina pesa za kulipa mishahara. Lakini sasa hakutakuwa na sababu ya wafanyikazi wetu wanaofanya kazi katika serikali za mashinani kukosa mishahara yao. Nasema kwamba kipaumbele iwe ni wafanyikazi wenu wanaofanya kazi katika kaunti zote 47 katika Kenya. Hivi sasa pesa ziko. Walipeni mishahara yao. Bw. Spika wa Muda, nataka kumalizia kwa kusema hii Ripoti yetu tuliiandika na kukubaliana nayo. Hii ni kwa sababu ni ripoti ambayo imepeana mwelekeo na imeeleza ni sababu gani tumeweza kukubaliana kuchukua hizi Shilingi 387 bilioni. Tukakubali zile zingine kama shilingi 13 bilioni zipotee ...
view
17 Oct 2024 in Senate:
Bw. Spika, naunga mkono Hoja hii ili tuwe na nafasi ya kumsikiliza Naibu wa Rais siku ya Jumamosi. Tunaelewa kwamba hii ni kesi muhimu sana na macho yote nchini yanaangalia Seneti. Napeana pole zangu kupitia Senior Counsel, Mhe. Paul Muite, kwa sababu client wake ni mgonjwa. Ugonjwa ni jambo la Mwenyezi Mungu. Hatuwezi kusema kwamba mtu hawezi kuwa mgonjwa. Mtu yeyote anaweza kuwa mgonjwa. Kwa hivyo, ningependa afikishe pole za Seneti. Tunamtakia kila la heri. Mwenyezi Mungu ampe nafuu ili tupatane hapa. Bw. Spika, tuko katika njia panda; ni mgonjwa. Je, tuendelee ama tusiendelee? Tumpe nafasi. Kama binadamu, hii ni ...
view
17 Oct 2024 in Senate:
Asante, Mhe. Spika. Naunga mkono Hoja hii inayohusu kumng’atua mamlakani Naibu wa Rais. Katika Kanuni zetu za Kudumu, Kipengele 145, kinaongea jinsi Rais ama Naibu Rais anavyoweza kuondolewa mamlakani. Kwanza, mashtaka yote yalioko mbele yetu kuhusu ukosefu wa nidhamu au nidhamu kwa Wakenya, inasikitisha kusikia Naibu Rais akisema kwamba Kenya ni kampuni na kwamba iko na hisa na kama hukuwapigia kura kama walivyotaka, utangojea sana kupata maendeleo. Mtu akiwa Naibu Rais anakuwa kiungo muhimu cha kuunganisha taifa. Ukiwa Naibu Rais uliyechaguliwa, maendeleo ni lazima yafike mashinani kote nchini kwa waliokupigia kura na hata wale ambao hawakukupigia kura. Wewe ni kama ...
view
17 Oct 2024 in Senate:
kutoka Mombasa hadi Malindi iligeuzwa katikati na ikaenda kwa hoteli inayoitwa Vipingo Beach Resort Limited. Huo ni mradi ambao ungefaidisha zaidi watu wa Kilifi hususan wakulima, wafanyibiashara na wananchi lakini yeye akaigeuza ikaenda kwake. Nilipata fursa ya kuenda huko. Barabara hiyo imehepa mikanju na miembe ikienda kwenye hiyo hoteli. Hivyo sio namna barabara zinavyotengenezwa. Huo ni ukiukaji wa nidhamu. Mhe. Spika, sisi sote tunaamini kwamba kuna Mungu na ukimkosea atakuadhibu wakati fulani. Wale waliokosewa sasa hivi, kuna malipo yanayoendelea. Ni jambo la kusikitisha kuona kwamba ukifa mali yako haitaenda kwa watoto wako bali kwa ndugu yako na bibi yake na ...
view
15 Oct 2024 in Senate:
Asante, Bw. Spika. Kwanza, ninamsifu dada yetu, Fatuma Dullo, Seneta wa Isiolo, kwa kuleta malalamishi kama haya mbele ya Bunge la Seneti. Ni jambo la kusikitisha sana kuona gavana aliyeitwa kwa Bunge la Seneti aje ama gavana ameitwa na Kamati ya Seneti ajitokeze na akose kuitika. Ni jambo pia la kusikitisha kwamba, yeye kama kiongozi wa gatuzi la Isiolo, ni lazima azingatie sheria na ajue kwamba, Bunge la Seneti ndio linalomshugulikia na kumtafutia pesa ili atumie na kufanya maendeleo ndani ya Isiolo. Ule uamuzi, Bw. Spika, umeutoa hivi sasa kwamba yeye aitwe tena mbele ya Kamati, kupitia kwa Jenerali Mkuu ...
view
15 Oct 2024 in Senate:
gatuzi la watu wa Isiolo na akiitwa na Isiolo au Kamati ya Seneti, ni lazima afike hapo. Asipofanya hivyo, hatua itachukuliwa.
view
14 Oct 2024 in Senate:
Asante, Bw. Spika. Kwa sasa, watu wa Kaunti ya Kericho wanajua ya kwamba kesi yao sasa hivi iko kwa Seneti. Hoja iliyo mbele yetu ni ya kusimamisha kusikilizwa kwa kesi dhidi ya gavana ama kuimaliza wakati huu. Tumekuwa na mifano tofauti tofauti mbele ya Seneti. Kulikuwa na Kesi ya Mhe. Mike Sonko aliyekuwa Gavana wa Jimbo la Nairobi City. Jambo kama hili lilitendeka lakini Seneti iliamua kusikiliza kesi yote kwa ujumla ndiposa iamue. Ninataka tuchukue uamuzi huo huo ambao ulichukuliwa wakati ule na Bunge hili. Bunge hili na Maseneta wengine sio waliokuwako lakini wale ambao wako sasa hivi wanaweza kufanya ...
view
14 Oct 2024 in Senate:
kando kidogo ili tuweze kuichukua pamoja na hizi zingine kama tulivyofanya katika mfano wa kesi ya Mhe. Sonko.
view