Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 71 to 80 of 2266.

  • 26 Nov 2024 in Senate: Pili ni kwamba, ilikuwa ni muhimu aweze kukemea ama aseme katika Hotuba yake kwamba, hakufurahia vitendo vilivyofanywa na polisi walipotumia nguvu zaidi kuliko walivyokuwa wamefunzwa kule Kiganjo, jinsi ya kupambana na kesi kama hiyo. Hawa walikuwa vijana wadogo, waliruka ukuta na kuenda dining room, wakakula chakula kilichokuwa pale. Wengine waliingia ndani ya Bunge na kusema waliyoyasema. Lakini kuna watoto wetu ambao waliumia. Bw. Spika wa Muda, sasa watu wamesonga mbele. Wale walioumia wakati wa mgomo, natumai kwamba Rais atatafakari na atachukua hatua ya kuona ya kwamba hao vijana wa Gen-Z watapata afueni katika hospitali; na kama kulikuwa na mazishi, pesa ... view
  • 26 Nov 2024 in Senate: Inaweza kuwa sio makosa yake. Yeye anafikiria kwamba watu wana implement, lakini watu wengine wanamchelewesha katika tegemeo lake la kuwasaidia Wakenya. Hivi sasa, hizo medical covers za SHIF na SHA, zote ziko na shida ama hazifanyi kazi. Bw. Spika wa Muda, vile vile, mawaziri wake wanafaa kutimiza yale anayoyasema Rais. Lakini mara nyingi tunaona jambo la kusikitisha ambapo Rais anaelekeza kitu lakini jambo hili linakosa kutekelezwa. Wale basi, wanambwaga Rais. Kuna haja gani Rais aseme kwamba kutakuwa na Collective Bargaining Agreement (CBA) na inafaa kutiwa kidole na Waziri wa Elimu ama Waziri wa Afya; ambaye anafaa kutekeleza mishahara fulani baada ... view
  • 26 Nov 2024 in Senate: Kindly add me five. view
  • 26 Nov 2024 in Senate: I want to touch on important aspects. Jambo la kwanza ni kuwa, Rais aligusia mambo mengi mazuri. Aliongea kuhusu sukari, mahindi, kahawa, na majani chai. Kimaendeleo, zitasaidia namna gani? Kati ya mimea aliyozungumzia, kuna mimea miwili muhimu sana kutoka sehemu ninayotoka. Upande wa Kilifi kunakuzwa korosho na mananasi. Mkorosho ni mmea muhimu sana kwa maisha ya wakulima kule, pamoja na mananasi. Vitu vingi vinaweza kupatikana kwa urahisi kwa sababu ile ardhi inakuza mmea kama mkorosho. Ingekuwa vyema kama Rais angezungumzia hatua ambazo Serikali imechukuwa kutenga pesa zitakazopewa wakulima hawa wanaopanda na kuuza korosho, mananasi na maembe, kwa sababu hawa pia ... view
  • 26 Nov 2024 in Senate: Transmission Company (KETRACO) wasimamishe biashara yao pamoja na ile ya Adani kutengeneza airports zetu. Hili ni jambo ambalo litasaidia uchumi wa nchi hii kutoweza kupoteza pesa ambazo tunahijati zaidi kwa kuzikinga na ufisadi. view
  • 20 Nov 2024 in Senate: Asante, Bw. Spika. Kwanza kabisa Bi. Waziri, ninakupa heko kwa kuweka sahihi kwa mkataba wa kutaka kuendelea na kazi yako ya uwaziri hapo jana. Kama unavyojua, Kaunti ya Kilifi ambapo mimi ni Seneta, ni eneo la pwani ambalo linajulikana sana kwa mambo ya maskwota katika Kenya nzima. Ninafikiria hakuna kaunti ambayo ina maskwota wengi zaidi ya Kaunti ya Kilifi. Nikizingatia ya kwamba tunaweza kulingalisa na sasa hivi ambapo kumekuwa na wingi wa watu ambao wanataka kujenga majumba na watu ambao wamekuja kuweka raslimali zao na kutafuta vile wanaweza kujiendeleza kimaisha na kibiashara. Hilo ni jambo nzuri. Hata hivyo, tukiangalia zaidi, ... view
  • 20 Nov 2024 in Senate: Bw. Spika wa Muda, watu wanajenga majumba na wengine kuyanunua na wakija pale huwa wanakuja na hati miliki wakisema ya kwamba wao ndio wamiliki. Watu wengine wanavurushwa kwa kutumia polisi. Polisi wanatumiwa vibaya kwa kuambiwa endeni mukawaondoe watu katika makao yao. Je, ni hatua gani ambayo Wizara yako ambayo inahusika na utetezi kama huu, unaweza kutetea maskwota ama ni hatua gani Wizara yako inachukua kuona ya kwamba maskwota wanoishi kama ni Kaloleni, Rabai--- Ukiangali Eneo Bunge la Rabai, sasa hivi lote limevamiwa na waegezaji wanotaka kuja na kuweka mali zao na kila kitu. Wameichukua ardhi ile na kusongesha wenyeji waliozaliwa ... view
  • 20 Nov 2024 in Senate: Tafadhali Bw. Spika wa Muda, kwa heshima na taathima, swali hili linanihusu mimi sana. Watu wangu wametupwa na wengine wanashikwa na polisi. Kila siku mimi niko katika polisi station kuwatetea watu wangu ili waachiliwe huru. Wanashikwa kwa sababu maeneo yao yamechukuliwa na waegezaji. Ndipo ninataka Waziri, kwa sababu yuko hapa leo aeleze kinaga ubaga, je ni hatua gani ambayo Wizara yake imechukua kutetea maskwota, sio Kilifi tu bali Kenya nzima. Wanateteaje maskwota iwapo maendeleo yaje na maskwota wajue kuwa wako na haki zao. view
  • 20 Nov 2024 in Senate: Asante, Bw. Spika. Ningependelea kuona Land Control Board ya Kilifi imechunguzwa. Imejitumbukiza kwenye hali ya ufisadi. Karatasi zinatolewa mashinani na ndio sababu hawa maskota wanafurushwa. Pia polisi wanatumiwa vibaya kufurusha watu kutoka maeneo yao. Uchunguzi ufanywe katika Land Control Board ya Kilifi kama ulivyopendekeza uchunguzi ufanywe Land Control Board ya Ngong. The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate. view
  • 19 Nov 2024 in Senate: Thank you, Mr. Speaker, Sir, I beg to second. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus