12 Feb 2025 in Senate:
Asante, Bw. Spika wa Muda. Kwanza nampa kongole Seneta wa Nairobi, ndugu yangu Edwin Sifuna, kwa kuleta Taarifa hii ambayo ni muhimu sana kwa watu walio mashinani kote nchini. Jambo la kwanza, ninaiunga hoja hii mkono kwa dhati kwa sababu, wale wanaofanya kazi kule vijijini ni watu muhimu sana na inatakikana waangaliwe na kaunti zao. Ni jambo la aibu kuona hapa Nairobi, ambapo ni jiji kubwa hapa nchini, lina watu wanaojitolea kufanya kazi katika jamii lakini hawangaliwe sawa sawa. Lakini tunasikia kwamba hawaangaliwi, leo watu wanaenda na miguu kavu, hata hawana slippers ama zile viatu ndugu zetu wa Kikamba huwa ...
view
12 Feb 2025 in Senate:
na walikuwa wanazalisha au wakunga. Bw. Spika wa Muda, siyo kila mama alikuwa anaweza kwenda hospitali kuzaa. Wakunga walikuwa wanalipwa na manispaa zao. Kwa hivyo, tunataka jukumu kama hilo pia litekelezwe kiukamilifu zaidi katika serikali zetu za gatuzi. Ninaunga mkono Taarifa hii ya Katibu wetu wa Chama Cha ODM ndugu yetu, Sen. Sifuna. Asante sana.
view
12 Feb 2025 in Senate:
Thank you, Mr. Temporary Speaker, Sir. I second.
view
12 Feb 2025 in Senate:
The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate.
view
12 Feb 2025 in Senate:
Similarly, Hon. Members this being a Procedural Motion and in the absence of Members keen on contributing to it, I make a determination pursuant to Standing Order No.84(2) that this is a matter that does not affect counties and, therefore, proceed to put the question.
view
12 Feb 2025 in Senate:
Mr. Temporary Speaker, Sir, I beg to second.
view
12 Feb 2025 in Senate:
Mr. Temporary Speaker, Sir, I beg to second.
view
12 Feb 2025 in Senate:
Asante Bw. Spika wa Muda. Ilikuwa ni mtihani mkubwa sana kufikia hapa ambapo tumefikia kwa sababu kuchagua maseneta na kuwaweka katika kamati hizi zilizoko ndani ya Seneti sio kazi rahisi. Kwa upande wa maseneta walio wachache tumejaribu iwezekanavyo kuona ya kwamba kila tuliyemchagua ni seneta mkakamavu katika kitengo ambacho tumempatia. Mimi ninaunga mkono na kusema kwamba Maseneta hawa wote ambao wamewekwa katika Taarifa hii ya leo wana ujuzi, taaluma, akili na uwezo wa kutekeleza wajibu wa majukumu ambayo tumewapatia. Vile tumewachagua hawa Maseneta ambao watakuwa katika kamati hizi sio kazi rahisi. Mara nyingi tunaona kamati nyingi kwa mfano ule wakati ...
view
12 Feb 2025 in Senate:
Asante Mstahiki Spika wa Muda. Naanza kwa kuunga mkono wale wote waliochaguliwa hapa katika hizi Kamati zote tatu. Kamati hizi ni nguzo ya Seneti kwasababu ni Kamati ambazo ziko na majukumu ya hali ya juu hususan mambo ya utekelezaji wa pesa na matumizi na pia kuchunguza kama hizo pesa tunazopeleka mashinani zinatumika vyema. Kwa hivyo, tukiwa tunajidai na hizi Kamati, ni kwamba tuko na imani ya kwamba zitatekeleza wajibu wake. Hao waliochaguliwa hapa wote katika hizi Kamati ni wakakamavu. Niko na imani ya kwamba watatimiza vile inavyotakikana kufanywa hasa matumizi ya pesa katika kaunti. Asante. Ninaunga mkono.
view
11 Feb 2025 in Senate:
Asante, Bw. Naibu Spika. Kwanza ninakubaliana na majina yaliyoko hapa, ya Maseneta ambao wataketi katika kamati inayoongoza Bunge katika itifaki zake. Waliochaguliwa hapa ni Maseneta walio na ukakamavu wa mambo ya Seneti. Tuna imani ya kwamba hawa waliochaguliwa wataweza kutimiza ile hadhi ambayo wamepewa. Nikiendelea kuunga mkono majina haya saba, ningependa kutangazia ndungu zangu ya kwamba ni jambo ya kusikitisha ninaposimama na kutangaza kifo kilichotokea cha babake Spika wetu wa Seneti, Hon. Amason Kingi. Kifo hicho kilitokea jana wakati madaktari walipokuwa wakiendelea kumpatia matibabu mzee wetu. Ijapokuwa sisi tulimpenda, Mwenyezi Mungu alimpenda zaidi. The electronic version of the Senate Hansard ...
view