Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 41 to 50 of 2266.

  • 26 Feb 2025 in Senate: ambao wanaishi sehemu mbali mbali. Kwa mfano, unavyoelewa, Kilifi ni kaunti moja kubwa katika Kenya, na wapo wanaotumia hii ridhaa ambayo iko Bamba na wale watu wa Bamba sasa imekua haifanyi kazi. Ikiwa ni hivyo, Wizara yako imechukua hatua gani kuona ya kwamba wale ambao hawapati services kama hizi wanaweza kuzipata wakiwa huko Bamba, Kilifi County. view
  • 26 Feb 2025 in Senate: Bw. Spika wa Muda, Waziri anaweza kuwa hajui lakini kulingana na Kanuni zetu za Kudumu katika Bunge la Senate, ukianza kuongea unatumia lugha moja. Kwa vile umeanza kuongea Kiswahili, ingekua bora zaidi uendelee kuongea Kiswahili mpaka umalize, si ukifika katikati unawacha panda njia unafuata panda njia ingine. Hiyo hairuhusiwi katika kanuni zetu na ingekua hivyo hivyo--- view
  • 26 Feb 2025 in Senate: Asante Sen. Mandago. view
  • 26 Feb 2025 in Senate: Kulingana na Kanuni zetu za Kudumu, wewe peke yako ndiye unaweza kuniuliza, je, ninahitaji kuambiwa kitu chochote na ndugu yangu Sen. Mandago, kama nilikuwa sijasema kisawa sawa? Kwa hivo, alivyosema yeye si haki kumjibu Seneta hata kama yeye ni Mwenyekiti wangu katika kamati ya Afya. Hana ruhusa na hawezi kuvunja sheria za Kanuni za Kudumu za hili Bunge la Senate. Kwa hivyo, Bw. Spika wa Muda, Waziri ni lazima azingatie ya kwamba yuko katika Jumba hili na akiwa katika Jumba hili la Seneti, kama Kanuni zinasema ni Kiswahili ama kizungu akianza, amalize akijua pia yeye yuko chini ya hizo Kanuni ... view
  • 25 Feb 2025 in Senate: Bw. Spika, ningependa kuunga mkono taarifa hii kuhusu mambo ya ngano. Wakulima wa ngano lazima waangaliwe pia ili mazao yao yanunuliwe katika masoko ya nje. Ni jambo la kusikitisha na madharau kwa wakulima wa ngano kutoonyeshwa kuwa ngano pia ni muhimu. Wakulima wengi hawajui watafanya nini na ngano waliovuna, mmojawao akiwa Sen. Wakili Sigei. Tulipokuwa tukizungumza naye, aliniambia kuwa amevuna ngano nyingi lakini hana mahali pa kuipeleka. Ni kama atapeana bure ama akae nayo na hatimaye iharibike. Taarifa hii ambayo imeletwa na Seneta wa Narok ni muhimu. Wakulima hao wanafaa kuangaziwa ili kuendeleza shughuli zao. Haina haja kuagiza ngano kutoka ... view
  • 25 Feb 2025 in Senate: kutetewa na Wizara. Suala hili linafaa kuangaliwa na Kamati ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ambayo inafaa kuchunguza vizuri na kutupatia mwelekeo. view
  • 25 Feb 2025 in Senate: Asante, Bw. Spika. Jambo la kwanza ni kuwatakia kila la heri wajane walioachwa nyuma, watoto pamoja na vitukuu wake. Tunayo imani ya kwamba Mwenyezi Mungu atailaza roho ya marehemu mahali pema walipolala wema. Ninamfahamu Bw. Leonard Mambo Mbotela kwa miaka mingi. Alikuwa ni mtu muungwana na hata hilo jambo la kusema “Je, huu ni ungwana” ni kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa na tabia zake ambazo ni za heshima na za ungwana. Alikuwa sio mtu wa kutaka fujo. Saa zote alijaribu ku - encourage jamii ili iweze kutenda vyema katika maisha yao. Kijiji cha Frere Town kule Kisauni ambako wazee wake ... view
  • 25 Feb 2025 in Senate: Asante, Bw. Spika wa Muda. Jambo la kwanza yule ambaye alikuwa amefanya makosa na ikabainika wazi ya kwamba kweli Seneta alikuwa amefanya makosa, aliweza kuomba msamaha wakati alipatikana kuwa na hiyo hatia. Kwa kawaida unaona ule ugumu wa mtu akiwa amekosea na akiwa hajui, na akiwa amekosea na akiwa anajua. Wengi huwa pengine wanaweza kukataa kuomba msamaha ama wengine wakaweza kuomba msamaha. Sasa hivi tayari ndugu yetu Omtatah alikuwa hapa na amesema ijapokuwa akijivua yeye nguo yake anaweza kuomba msamaha, lakini kwa vile ambavyo ameona ajigawanye mara mbili, akasema yeye pia amesema pole sana na anaomba msamaha na hii Seneti ... view
  • 25 Feb 2025 in Senate: Nilisema kujitenga mwili wake na vile alivyotamka--- view
  • 25 Feb 2025 in Senate: Pole, Bw. Spika wa Muda. Pengine ulimi uliteleza ndio nikaskia sauti ya Sifuna akicheka. The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus