Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 1611 to 1620 of 2266.

  • 17 Jul 2019 in Senate: Leo amenoa kwa sababu amekuita “mzungumzishi”. Katika Bunge la Tanzania, Bwana Spika anaitwa Bwana Spika. Hajapewa jina lingine na Mheshimiwa Mbunge huwa anaitwa Mheshimiwa Mbunge wa eneo fulani. Hakuna jina kama “mzungumzishi” ama cheo cha “mzungumzishi”. Je, ni haki dadangu kuendelea kutumia jina “mzungumzishi”? Tunaomba aliondoe jina hilo jina atumie jina Bwana Spika. view
  • 17 Jul 2019 in Senate: Bw. Spika, asante. Kuna tafakari mbili hapa za Google. Google ile ya Sen. Malalah inasema wewe ni chatter Ile Google nyingine inasema ya kwamba wewe ni “mzungumzishi”. Hata hivyo, tunasema ya kwamba Google hizi zote mbili hazifai kwa sababu sio Kamusi ya Kiswahili. Google moja imetoa kwa maktaba na nyingine ya Sen. Malalah ninafikiria pengine ame-Google pande hiyo--- Maktaba imetoka upande za Pwani; hii ya Sen. Malalah ambapo Spika anaitwa chatter hatujui ni ya upande gani. Katika maoni yangu, hiyo amri uliyotoa kwanza--- view
  • 17 Jul 2019 in Senate: Bw. Spika, mimi ninaongea hapa katika Bunge na ningependa unitegee masikio kwa sababu ukishatoa amri iwe ni sawa au si sawa, ni lazima amri yako itimie ndani ya Bunge hili. Hatusemi kwamba yale Seneta dada yangu alivyokuwa anasema au Sen. Malalah wana makosa. Lakini tunasema kwamba kwa sababu umetoa amri, hiyo amri yako itimie halafu kama kuna marekebisho ya aina yoyote, yaletwe kesho; sio leo baada ya Bw. Spika kutoa amri ya Bunge hili. view
  • 16 Jul 2019 in Senate: Asante, Bw. Naibu Spika. Langu ni kukuunga mkono katika kuwakaribisha wanafunzi kutoka Kaunti ya ndugu yangu, Sen. Mwangi, ambaye ni Seneta mtendakazi. Vile vile, ningependa kuwaambia vijana kwamba Maseneta wote waliopo hapa walikuwa vijana kama wao. Walienda shule, wakafanya bidii na hatimaye wamejipata hapa kwa sababu ya kuchaguliwa na wananchi. Pia nyinyi pia mnaweza kuwa Maseneta kama sisi baada ya sisi kustaafu na muendelee kujenga taifa letu. Nawatakia kila la kheri wanafunzi kutoka Kaunti ya Nyandarua. Nafurahi pia kuona kwamba ndugu yangu amefurahishwa sana kwa kuja kwenu. view
  • 10 Jul 2019 in Senate: Madam Temporary Speaker, I beg to second. view
  • 20 Jun 2019 in Senate: Asante sana, Bi. Spika wa Muda kwa kunipa fursa hii. Nawashukuru waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Uganda kwa sababu hao ndio majirani wetu wa karibu sana. view
  • 20 Jun 2019 in Senate: Nawapa wabunge wa Uganda kongole kwa kuja hapa kujifunza. Ingawa Maseneta wengine wanasema kwamba Wabunge hawa hawaelewi Kiswahili, naamini kwamba wengi wao wanaelewa Kiswahili. Nina imani kwamba watajifunza mambo mengi sana hata lugha ya Kiswahili. Ningependa kuwashawishi kwamba Kenya ina mahali kwingi ambapo wanaweza kutembea jioni jioni. Kiongozi wa wengi wa Seneti, Sen. Murkomen, anajua sana sehemu ninazozungumzia, kwa hivyo anaweza kuwatembeza jioni. view
  • 20 Jun 2019 in Senate: Bi. Spika wa Muda, nawashawishi Wabunge wa Bunge la Uganda wachukuwe nafasi hiyo ili waone Kenya inaweza offer kitu gani. view
  • 20 Jun 2019 in Senate: Asante sana, Bi. Spika wa Muda. view
  • 19 Jun 2019 in Senate: Ahsante Bw. Spika. Hilo jambo ni la kusikitisha. Ninatoa pole kwa familia ya wale waliopoteza maisha yao. Ni aibu ya kwamba kitendo kama hiki kinatendeka kila siku. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus