Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 1601 to 1610 of 2266.

  • 23 Jul 2019 in Senate: Asante, Bw. Naibu Spika. Hapo awali, ulitueleza kwamba kuna watoto kutoka Kajiado County ambao mpaka sasa wako pale juu. Nina kuunga mkono kwa kuwakaribisha kwa dhati. Ninawapa kongole walimu na watoto ambao wako katika madarasa ya chini kwa kuja katika Bunge la Seneti ili wasikie, watafakari na waoene Maseneta pamoja na Spika na vile tunafanya mambo yetu. Wao ni viongozi wa siku za usoni. Ninawapa changamoto ya kwamba hakuna lisilowezekana katika ndoto zao. Kama wanataka kuwa Maseneta siku moja, hiyo ndoto inawezekana. Kwa hivyo, wafanye bidii. Nimeketi katikati ya Maseneta wanaotoka katika kaunti za uchungaji. Shule hii ni moja wa ... view
  • 23 Jul 2019 in Senate: Nimesema, wafugaji. view
  • 23 Jul 2019 in Senate: Asante, Bw. Naibu Spika. Kuna tofauti ya watumishi wa Mungu na wafugaji au wachungaji. Nikizingatia mambo ya--- view
  • 23 Jul 2019 in Senate: Bw. Naibu Spika, amesema kwamba nimetumia neno ‘wachungaji’ ambalo hata ndani ya Bibilia linamaanisha mtu anayetafuta kondoo aliyepotea na kumleta nyumbani. Nimesema kwamba hawa ndugu zangu wanaishi katika sehemu ambapo wanafuga mifugo kama vile ndugu yangu Sen. (Dr.) Ali anafuga ngamia, hawa wanafuga ng'ombe ambao wanatupatia maziwa na bidhaa zingine. Ndio maana nilisema nimeketi katikati ya dadangu na kakangu ambao ni Maseneta wa nguvu kutoka maeneo ya Kajiado na Narok. The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate. view
  • 23 Jul 2019 in Senate: Bw. Naibu Spika, hawa hawakupata nafasi hii kwa urahisi. Walifanya bidii wakiwa watoto kama nyinyi katika sehemu za ufugaji. Kwa hivyo, nyinyi mnaweza kuwa kama wao. view
  • 18 Jul 2019 in Senate: Asante sana, Bi Spika wa Muda. Najiunga na Hoja hii ambayo imeungwa mkono na wenzangu wote. Bubu ni mtu asiye na uwezo wa kuzungumza. Wakati unatesa bubu, itafika wakati bubu ataanza kububuja maneno ili aanze kuongea, unafaa kukimbia mbali sana. Tulikuwa tumenyamaza kwa muda mrefu sana, lakini sasa tunawaambia ndugu zetu kwamba hatunyamazi tena. Maseneta 52 walioandamana leo ni walinzi wa serikali za kaunti. Tulienda kortini leo kudai haki ya serikali za kaunti. Nia yetu ni kuona kwamba serikali za kaunti zimepata fedha zao na wanaweza kutekeleza wajibu wao kwa wananchi. Bi. Spika wa Muda, naunga mkono kwa dhati Hoja ... view
  • 17 Jul 2019 in Senate: On a point of order, Mr. Speaker, Sir. view
  • 17 Jul 2019 in Senate: Bw. Spika, sisi sote hatufahamu lugha ya Kiswahili kwa ufasaha. Wewe ni mtu amabaye umekua ukiona maneno hayo yakitendeka hapa na umekua na roho ya kuweza kuwasikiliza. Mimi ningeomba, Sen. Were ni dada yangu, ana upungufu kidogo wa kuweza kujieleza kwa lugha hii. Kwa hivyo, mpatie nafasi aweze kujieleza katika lugha anayoifahamu sana. view
  • 17 Jul 2019 in Senate: Asante, Bw. Spika. Ningependa kuunga mkono taarifa hii. Tunaona ya kwamba watoto wakiwa wamekubaliwa kuingia shule za upili, hasa shule ambazo ni za hadhi ya juu, siku ya kwanza, wiki ya kwanza, mwezi wa kwanza au muhula wa kwanza, wanateswa na wenzao wa vidatu vingine. Wanaweza kuwafanya wenzao kuwa kama watumwa. Wakati mzazi anapopeleka mtoto wake shule, nia yake ni kwamba mtoto huyo aweze kujifunza na kupata masomo ambayo yatamfaidi siku zake za usoni. Lakini hii dhuluma inayoendelea katika shule zetu hakubaliki kamwe. Juzi tulisoma kwenye gazeti, jua ya Nairobi School ambapo wanafunzi wa kidatu cha kwanza walifanyiwa dhuluma kubwa ... view
  • 17 Jul 2019 in Senate: Ahsante sana, Bw. Spika. Nampa kongole ndugu yangu, Sen. Orengo, kwa huo ufafanuzi. Katika hoja yangu ya nidhamu, nilikuwa nataka kusema mambo hayo hayo. Ninatoka katika eneo moja na Sen. (Dr.) Zani na ninamheshimu sana. Yeye ni msomi. Katika wale madaktari wanaotoka kule kwetu, yeye yuko katika ulingo wa hali ya juu sana--- view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus