Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 301 to 310 of 512.

  • 15 Mar 2023 in National Assembly: Mhe. Spika wa Muda, Umrah ana tajriba ya mambo ya mazingira. Hayo ndiyo mambo yake. Ana shirika linaloitwa Safari Doctor, shirika ambalo limekuwa Lamu na limetusaidia sana mpaka likapewa tuzo na United Nations (UN) katika mambo haya. Leo, nashangaa ninapoambiwa kwamba Umrah hana tajriba. Umrah ndiye mtu anayeweza kututetea tupate fedha kutoka kwa donors ili zitusaidie kwa mambo ya mazingira. Rekodi zinaonyesha Umrah alishindana na nchi nyingine kwa mambo haya, akashinda kama Mkenya, na akapewa tuzo ya UN. Inasikitisha sana. Au ni kwa sababu yeye ni Mbajuni? Hizi shida ambazo tunapata ni nyingi. Mambo haya yamefanywa kana kwamba hawakuwa wanataka ... view
  • 15 Mar 2023 in National Assembly: Hivi juzi tu, wamefanya mambo ya forest rangers . Sisi watu wa Lamu East tukapewa view
  • 15 Mar 2023 in National Assembly: watano na watu wengine wamepewa arobaini. Ni mambo haya yanatumika kukandamiza Mbajuni. Kwani sisi hatuna haki? Huyu Umrah ni mmoja tu! Tumepitisha watu wangapi hapa? Mbajuni mmoja ndio mmeona lazima mumkandamize? Si haki! Kamati haiko sawa. Haifai inavyofanya. Nionyesheni document moja ya Umrah ambayo haiko sawa. Mwanzo, alipokwenda Ethics and Anti-Corruption Commission (EACC) aliambiwa hizi view
  • 15 Mar 2023 in National Assembly: ndio zinafaa; apeleke hili na lile. Hii ndio maana alitoa mfano kuwa ukienda kuomba passport, utaambiwa uandike reason . Ukiandika sababu ni kuwa unaenda Tanzania, kisha uende huko na uitwe uende taifa lingine, utatumia passport hiyo hiyo. Kama alipitishwa na IEBC, kwa nini hawezi kupitishwa na Bunge na mwaka haujaisha? Documents zote ambazo sisi tulipeana kama wagombea viti bado hazija expire . Wana sababu zao hawa! Hawamtaki tu Umrah. Ninawaambia wanafanya makosa. Waangalie shirika la Safari Doctor na waulize view
  • 15 Mar 2023 in National Assembly: ya Umrah. Nawaambia, Umrah ndiye expert kwa mambo haya. Umrah amevuta pesa nyingi kutoka serikali za nje kuleta huku Kenya, mpaka akapewa tuzo ya UN. Itakuwaje apewe tuzo ya UN kisha hapa sisi tunamkataa? Hiyo ni dhuluma kwa Wabajuni, na haifai. Si sawa. Sisi pia ni Wakenya na tunalipa tax . Mtu mmoja wa Kibajuni katika hawa appointees ndio nyinyi hamumtaki? Imewaingia jichoni. It is not fair! view
  • 14 Mar 2023 in National Assembly: Asante Bwana Spika, kwa kunipa nafasi ya kutoa rambirambi zangu kwa niaba yangu, watu wangu wa Lamu East, na familia yangu, kwa familia ya Grace Onyango. Kwa kweli, Bi. Grace alikuwa mfano mwema. Mwanzo, ningependa kumpongeza Mbunge wa kiume ambaye ni rafiki wa wanawake. Inaonyesha kuwa kuna wanaume ambao ni marafiki wa wanawake. Lakini kuna wale ambao ni maadui wa wanawake ilhali hawawezi kukaa bila wanawake. Wakija hapa, wanaanza kutupiga. Hawawezi kukaa bila wanawake lakini wanapinga affirmative action . Tunavyo hivi viti 47 mkononi. Wanaume, msijisumbue kuvitoa. Hatuwezi kuwachilia kile tunacho ili tutafute kingine. Tumeona umuhimu wa affirmative action seats ... view
  • 7 Mar 2023 in National Assembly: Asante, Mhe. Spika, kwa kunipatia nafasi ya kuchangia ombi lililotumwa kuhusu watu kupotea kiholela. Sisi, katika Lamu Kaunti, tumeathirika sana. Tukitaja watu wetu waliopotea na hatujui wako wapi mpaka sasa, orodha ni ndefu. Tulifikiria ni masuala ya Al Shabaab kwa vile tuko mpakani lakini la kusikitisha na kuchanganya watu zaidi ni kuwa hivi karibuni tuliambiwa mauaji ya Lamu Kaunti hayahusiani na Al Shabaab bali ni mambo ya mashamba. Watu ninaowasimamia sasa wanatatizika. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 7 Mar 2023 in National Assembly: Hawajui wanaowaua ni nani? Kwa nini watu wetu wakimbie na wateswe kwa sababu ya AlShabaab na kumbe kuna kiongozi anayejua wanavyouawa? Nimefurahia hili ombi. Hata mimi itabidi niifanye iwe kauli au dua ili Serikali ituambie ni nani anawaua watu Lamu. Hilo ni jambo ambalo limetatiza watu sana. Siku nyingi tumekuwa tukifikiri ni Al Shabaab kumbe siyo wao bali ni mambo ya ardhi. Aliyoyasema Kiongozi wa Wengi Bungeni, inamaanisha anawajua wanaowaua watu huko Lamu Kaunti. Na itakuwa vizuri kuwataja kwa sababu imetutatiza sana. Kule, tunategemea utalii. Watalii sasa hawakuji maana kuna askari wengi na msafara wa magari mengi. Wakikuja kama watalii ... view
  • 7 Mar 2023 in National Assembly: Ahsante, Mhe. Naibu Spika. Swali hili limengojewa sana, mpaka wenyewe wamekuja hapa. Dadangu ambaye ni rafiki yangu, Thweba, amekuja kuona vile nitauliza Swali hili kwa sababu wao wanaathiriwa sana. view
  • 7 Mar 2023 in National Assembly: Hon. Deputy Speaker, I rise to ask the Cabinet Secretary for Information, Communication and the Digital Economy the following Question: (a) Could the Cabinet Secretary explain why the people of Siu, Shanga and Mkokoni in Lamu East Constituency are suffering from digital exclusion by not being connected to the mobile phone network? (b) Could the Cabinet Secretary further explain why the entire Lamu East Constituency is still served by 2G Network when the rest of the country is on 4G Network and is soon transitioning to 5G Network? (c) What plans does the Ministry have to ensure that Siu, Shanga ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus