Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 321 to 330 of 515.

  • 15 Nov 2022 in National Assembly: Hon. Temporary Speaker, thank you for giving me this opportunity to ask the Cabinet Secretary for Roads, Transport and Public Works the following Question: (i) Could the Cabinet Secretary outline the Government policy measures being undertaken to develop marine transport in the country, and particularly in Lamu County? (ii) What immediate plans has the Ministry put in place to provide modern marine transport facilities such as ferries, among others, to Lamu residents and tourists? (iii) What policy measures are in place to facilitate private enterprises to develop marine transport facilities in the country, and in Lamu County in particular? view
  • 12 Oct 2022 in National Assembly: Hon. Deputy Speaker, I already have the microphone. view
  • 12 Oct 2022 in National Assembly: Asante Naibu Spika kwa kunipa nafasi hii ili nami niweze kuchangia Mswada huu muhimu wa ukame kuwa janga la kitaifa. The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 12 Oct 2022 in National Assembly: Mwanzo, ningependa kuchukua nafasi hii kukupongeza kwa kupata nafasi ya kuwa Naibu wa Spika. Tunajua wewe ni mtendakazi. Tunajua kazi yako ni nzuri na tayari ishaanza kuonekana. Kusema kweli, kiangazi kinawatatiza sana watu wetu; haswa, watu wangu wa Lamu Mashariki. Kiangazi kimewaathiri watu wa Kiunga na watu wa Eneo Wodi ya Faza. Ningeomba Wabunge ama viongozi wa taifa letu wasichukulie hili janga la kiangazi kama janga la watu fulani tu maana linaathiri watu kutoka nyanja zote. Mfugaji akipata hasara kwa minajili ya ng’ombe wake kufa, hatakuwa na kitu cha kuuza ili apate faida ili imuwezeshe kupata hela za kununua mazao. ... view
  • 12 Oct 2022 in National Assembly: Nasi pia sasa tumekuwa kwa janga hilo la ukame ilhali tulikuwa tumejipanga. Kwa hivyo, nataka kuwaambia majirani zetu wa Garissa, Tana River na wale wote wanaoleta ng’ombe – hata wanaowabeba kwa malori wakiwaleta – wajue siku ile mimi napigania mabwawa na vitu vingine kupelekwa Lamu wao huwa wako mbele kupigania Lamu isipate mabwawa hayo ili wapate wao. Lakini saa hii tumeona kwamba yale mabwawa machache ya Lamu ndiyo wanayoyafuata. Kwa hivyo, Mhe. Naibu wa Spika, mimi ningeomba Serikali iweze kuangalia yale maeneo ambayo yatakuwa yakiwafaa wengine. Pesa zilitolewa yakajengwa mabwawa lakini mvua haikunyesha kule. Mvua imenyesha mahali kama Lamu, na ... view
  • 12 Oct 2022 in National Assembly: Kwa hivyo, nyinyi mnaoniangalia vizuri, tena watu wangu majirani wa Garissa, mhakikishe, maanake nyinyi ndio wa kwanza, tukipata hivyo vidimbwi vinavuta Garissa zaidi kuliko Lamu. Na hivyo ndivyo vitu vinawafaa. Saa hii watu wangu wanatatizika. Changamoto za usalama zinaongezeka kwa sababu ng’ombe na wafugaji ni wengi kwenye misitu, na katika misitu kama Boni kuna matatizo. Kwa hivyo, mnanipatia kazi ngumu mno. Kwa sasa hivi ni wakati mgumu kwa watu wa Lamu, haswa watu wa Kiunga. Kule kwenyewe kuna shida za kiusalama ilhali watu na mifugo wanakuja kwa wingi kudhoofisha usalama zaidi. Kwa hivyo, wakati mwingine mnapopanga jambo lolote kama jambo ... view
  • 18 May 2022 in National Assembly: Asante Mhe. Naibu Spika wa Muda. Naungana na wenzangu kupongeza Kamati husika kwa kuja na Ripoti hii. Kwa kweli, utakubaliana na mimi kwamba suala la afya ni nyeti na muhimu sana. Nawashukuru kwa kuwa wamelizingatia kikamilifu na kuliwekea mikakati. Mengi yamezungumzwa na wenzangu kuhusiana na suala hili. Masikitiko makubwa ni kwamba ni kweli sisi Waheshimiwa tuko na zile kadi za bima ya afya. Lakini, utapata kwamba unapopatikana na matatizo ukiwa hapa Bunge ama sehemu nyingineyo, huna budi kukimbilia hospitali kujiangalia afya. Kuna mambo mengine ambayo unapaswa kupitia hata kabla hujafika hospitali. Tukiwa hapa Bunge, Waheshimiwa huwa na kazi nyingi katika ... view
  • 18 May 2022 in National Assembly: Katika sehemu nyingi za nchi hii na kaunti zetu, utapata watu ni wagonjwa lakini hawawezi kufikia zile huduma za kujua magonjwa yao. Ndiposa utapata mtu amekaa na mara presha imepanda ila hajui alikuwa nayo; mtu amekaa, amepatikana na matatizo haya na hajui. Kwa hivyo, itakuwa vyema ikiwa Kamati itaangalia haya mambo zaidi na kuhakikisha kuwa kaunti zetu ziko na huduma za madaktari wa kutembea kama wale wanaopeana chanjo kwa watoto wadogo. Ukifanya utafiti wako, nchi hii yetu iko na watu wengi wanaoathirika na madhara ya afya ilhali hawajui. Itakuwa bora tukipata serikali yenye mipangilio ya kuenda mashinani kuangalia afya za ... view
  • 1 Dec 2021 in National Assembly: Asante, Mhe. Spika. Ningependa kuchukua fursa hii kuungana na wenzangu kumshukuru Mhe. Rais na kumpongeza pakubwa kwa Hotuba yake hapo jana katika Bunge hili. Ni dhahiri shahiri kuwa mengi yaliyozungumzwa na Mhe. Rais ni mambo ambayo yameonekana na Wakenya. Jambo moja kubwa ambalo lilishuhudiwa na Wakenya katika Bunge lililopita nikikumbuka vyema ni kuwa katika shughuli kama hii ya Hotuba ya Rais, Bunge lilikuwa na taharuki kubwa na bughudha nyingi sana kutokana na hali za kisiasa. Ukweli ni kwamba, jana kulishuhudiwa utulivu uliotokana na ushirikiano mwema kati ya Mhe. Rais Uhuru Kenyatta na wapinzani wake. Hata hivyo, ningependa kumwambia Mhe. Rais ... view
  • 1 Dec 2021 in National Assembly: Ningependa kumwambia Mhe. Uhuru Muigai Kenyatta kuwa, mbali na kuona miradi mingi ya barabara ikifanyika, katika Eneo Bunge la Lamu Mashariki, hakuna hata kilomita moja ya lami. Nimeweza kulileta jambo hili mara kadhaa katika Bunge hili na kuliwasilisha kwa wahusika wakuu. Kama viongozi kutoka Lamu, tumeshuhudia ujenzi wa LAPSSET. Ni matarajio makubwa kuwa kutokana na malengo ya ujenzi wa poti ile, Serikali hii na Rais watawapea kipao mbele vijana wetu wa Lamu katika nafasi zitakazopatikana mahali pale. Hayo ndiyo mambo ambayo yanafaa kuwa na mwongozo mwema katika Serikali hii tunayo. Tatizo kubwa ambalo liko na yafaa tulizingatie ni kuwa katika ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus