24 Nov 2021 in National Assembly:
Ahsante, Mhe. Naibu Spika wa Muda. Nami naungana na wenzangu kuchangia marekebisho haya huku nikimpongeza Mhe. Barasa kwa kuleta haya Bungeni. Nataka kwanza tujiulize ikiwa haya tunayojadili hapa Bungeni leo ni ya sheria ambayo tayari iko katika nchi hii ama haiko. Ukweli ni kwamba hii ni sheria tayari ipo lakini imemlazimu Mhe. Barasa kuiregesha Bungeni kwa sababu ya marekebisho. Nataka tujiulize kwa nini imelazimu irudi Bungeni kwa sababu ya marekebisho. Hali halisi ni kwamba sheria hii inawagandamiza na kuwadhulumu Wakenya sana. Wengi wameenda mbele za haki bila kupata hizi haki zao. Unapokuwa mfanyikazi na kila mwisho wa mwezi unakatiwa pesa ...
view
24 Nov 2021 in National Assembly:
nyumbani, wafaa kuambiwa pesa zako ziko benki uende ukachukue. Ndiyo ujue utazifanyia nini. Sioni sababu hata moja ya pesa hizi kukaa katika sehemu ambazo zipo kwa muda wote huo, kama miaka mitano au sita au saba, baada ya mtu kustaafu. Baada ya hizo siku zote, pesa hizo zinazalisha riba katika benki. Lakini mtu yule hapewi! Wanaochukua riba ni watu wenngine Serikalini. Ndiposa utapata matatizo makubwa katika idara hizi. Kuna masuala mengi. Wengi wanapatikana na makossa ya ulaghai na ufisadi katika idara hizi kwa sababu wamezuia haki za watu wakidhania labda ni haki zao. Kwa hivyo, la usawa katika kurekebisha haya ...
view
3 Aug 2021 in National Assembly:
Asante Mhe. Naibu Spika wa Muda kwa kupata fursa hii kuchangia Mswada huu wa waqf. Wengi wamezungumzia suala hili la waqf . Ningependa kueleza kwamba ni vyema kwanza tufahamu maana ya waqf ndiposa tupate yale maelezo kamili, ingawaje Mhe. Duale ametueleza. Waqf imekuweko katika nchi hii na imekuwa ikitambulika na nchi hii. Ni muongozo umekuwa ukitembea ama ukiendelezwa na Waislamu. Hivi sasa Mswada huu umefika hapa bungeni kwa marekebisho zaidi. Hii ni dalili kuonyesha kwamba umechukua mkondo wa sheria ya nchi hii inavyotakikana. Lakini, ni vyema vilevile tufahamu ya kwamba utaratibu na muongozo ambao unatakikana hususan katika suala hili, tukiwa ...
view
3 Aug 2021 in National Assembly:
kwa namna isivyo. Mheshimiwa Mishi ametoa mfano kuwa kuna raslimali ambazo ziko Mombasa zinazotumiwa kwa njia isiyo ya haki. Kwa hivyo, kutokana na hali hii, tume hii ya waqf haiwezikufanya lolote isipokuwa kupitia Bunge hili na kuweza kuweka makaribisho haya kwa usaidizi wa Wabunge ili kuweza kurekebisha na kuendesha utaratibu huu kwa namna yake. Kama nilivyosema, tunao wengi ambao wako tayari kuyafanya haya – kuweka fedha zao na raslimali zao kwenye waqf ili zisaidie jamii. Lakini, inafaa kuwe na muongozo. Hakukuwa na utaratibu au sheria ya kisawasawa. Ndiposa watu wengi walikosa imani ya kufanya jambo kama hili. Ninaamini pakubwa kwamba ...
view
16 Jun 2021 in National Assembly:
Ahsante Mhe. Naibu Spika wa Muda. Ningependa kuchukua fursa hii, kuungana na wenzangu kuunga mkono huu Mswada ambao uko mbele yetu kuhusiana na ugavi wa pesa ambazo zinaenda kwa serikali gatuzi.
view
16 Jun 2021 in National Assembly:
Kwa kweli, Wakenya mwaka 2010 walisimama kidete kuhakikisha kuwa wamepitisha Katiba ambayo itakuwa na serikali gatuzi. Kutokana na hiyo, matarajio ya Wakenya yalikuwa ni mengi sana, miongoni mwao ni kuona kwamba, huduma zimeweza kuwafikia kule mashinani na The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor.
view
16 Jun 2021 in National Assembly:
kuhakikisha kwamba usawa umepatikana na wakaweze kufurahia zile huduma ambazo zilikuwa ziwafikie katika sehemu 47 zilizogawanywa nchini.
view
16 Jun 2021 in National Assembly:
Vile vile, ni jambo muhimu sana na ni jambo linalohitaji kuzingatiwa, kwamba, zile fedha ambazo zinaenda katika serikali gatuzi, ni fedha ambazo zinahitaji kuwahudumia wananchi. Lakini kwa masikitiko makubwa, tumeweza kushuhudia kwa takriban hivi sasa awamu ya pili kuanzia serikali hizi zianze shughuli zake, kwamba kumekuwa na matatizo mengi sana, husasan katika zile hali za uongozi ambao unapatikana katika sehemu hizo. Mbali na maadhimiyo ya Wakenya kutaka serikali za kaunti ziwe zinafanya kazi katika sehemu 47 zilizopo, yale yanayoshuhudiwa hivi sasa yamekuwa ni matatizo mengi sana. Ukweli ni kwamba Wakenya wanahitaji huduma lakini zile shida na mateso yanayoonekana hivi sasa ...
view
16 Jun 2021 in National Assembly:
ile na anayestahili kupewa kazi ambayo anaweza kuifanya katika sehemu ile haimaanishi kwamba awe ni mtu wako kisiasa. La msingi ni ikiwa anastahili kupata kazi ile, basi ni sawa wale wahusika waweze kuchukua fursa hii kufanya usawa katika kuendeleza mambo kama haya. Kwa hayo machache, ningependa kuhimiza Serikali ya kitaifa kuhakikisha kwamba matatizo haya hayapatikani kwa sababu yanapotokea, shida nyingi ambazo utaziona zinajitokeza katika kaunti, lawama inakuwa nyingi na ule uchumi unaaza kuleta shida katika sehemu zile kwa sababu zile fedha zinapokuwa hazijafika katika sehemu hiyo, ni wengi ambao wanapata matatizo na wanapata shida sana kutokana na hali hiyo. Kwa ...
view
6 May 2021 in National Assembly:
Ahsante, Mhe. Spika. Nataka nichukue fursa hii kuungana na wenzangu ambao wametangulia kuzungumza kwa kupinga na kukataa marekebisho haya. Vile vile, nataka niseme kwamba nchi hii inawashukuru pakubwa Mhe. Raila Odinga na Mhe. Uhuru Kenyatta kwa kunyamazisha fujo iliyokuweko nchini. Miongoni mwa fujo hizo tulikuwa sisi viongozi. Leo hii nchi inashuhudia kwamba hakuna tena makelele na matusi. Tunalolijadili mbele yetu ni suala la uchumi na mazingira ama miundo msingi katika nchi yetu ya Kenya. Tunayajadili haya yote yaliyoko mbele yetu kama Wabunge tuliopewa fursa. Ni mambo mazuri tunapoyaona na kuyasoma lakini yote yanahitaji kutekelezwa baada ya kupitishwa na Bunge. The ...
view