Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 381 to 390 of 515.

  • 13 Mar 2019 in National Assembly: Thank you, Hon. Temporary Deputy Speaker. I join my colleagues in congratulating Hon. Ruweida, Woman Representative, Lamu County for bringing this important Motion to the House. view
  • 13 Mar 2019 in National Assembly: As many Members have spoken, this is one of the silent killing diseases. The effect of the disease is that many Kenyans cannot afford its cost. One must control his or her diet or nutrition if one has the disease. You will agree with me that many communities in the country cannot afford to choose what to eat. At the same time, medication for the disease is very expensive. view
  • 13 Mar 2019 in National Assembly: I urge the Government to …. view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Asante Mheshimiwa Naibu Spika wa Muda. Ningependa kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa fursa hii ya kuchangia Ripoti hii ambayo tunayo hapa Bungeni. Mimi ni Mwanakamati wa Kamati ya Hazina ya Maendeleo ya Maeneo Bunge. Vile vile, ningependa kumshukuru Mwenyekiti kwa kuileta Ripoti hii. Waheshimiwa wamezungumzia masuala ya Kamati ya Hazina ya Maendeleo ya Maeneo Bunge. Vile vile, ningependa kumpongeza Mheshimiwa Angwenyi kwa kuelezea historia fupi ya namna Hazina hiyo ilivyoanza. Ni takriban miaka 15 tangu Hazina hiyo ianzishwe. Ukweli ni kwamba Wakenya wengi wameiona faida ya Hazina hiyo tangu ianze hadi sasa inavyoendelea. Wengi waliochangia wamezungumzia changamoto nyingi ambazo ... view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Ni jambo la kusikitisha kuona pakubwa kwamba hali hii bado inaendelea katika nchi yetu. Utakubaliana na mimi ya kwamba Constituencies Development Fund (CDF) ilibadilishwa jina kuongezwa jina kwamba ni pesa za Serikali kuu kutokana na mipangilio ya Serikali ya ugatuzi. Hapo awali CDF ilikuwa na changamoto baada ya Wakenya kupitisha Katiba. Walisema ya kwamba CDF hairuhusiwi kuwepo tena kwa sababu ya ugatuzi. Katika historia fupi, baada ya hapo, masuala haya yalifika mpaka mahakamani na ikabadilishwa jina kuongezwa kwamba ni fedha za Serikali ya kitaifa. Waheshimiwa wengi ambao wamechangia leo wanalalamika kwamba hizi fedha ni kidogo kwa sababu majukumu na matakwa ... view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Vile vile, katika Bajeti ya nchi hii wakati pesa hizi zinavyogawanywa, fedha nyingi zinapelekwa katika wizara zinazohusika na elimu na usalama. Tukienda mashinani kama Waheshimiwa, tunaulizwa na wananchi masuala ya elimu na usalama. Wananchi wanatarajia pesa za NG-CDF zisimamie usalama na elimu. Nina swali kwa Serikali ya kitaifa. Kwa nini inapeana pesa nyingi kwa Wizara ya Elimu na kuna majukumu ambayo wamepeana kusimamiwa na NG-CDF katika masuala ya elimu? Maoni yangu katika jambo hili ni kuwa wakati Bajeti ya nchi hii inapopangwa, asilimia kubwa ya fedha ambazo zinaenda kwa Wizara ya Elimu ziletwe katika kuimarisha NG-CDF. Katika neno “NG-CDF”, kuna ... view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Tukiwa mashinani, walinda usalama kama machifu wanawategemea Wabunge kutekeleza mambo yao ya usalama katika zile sehemu. Serikali hii inapeana pesa kwa wizara kama hizi. Kwa hivyo, ningependelea tutenge pesa fulani kutoka kwa zile fedha ambazo zinaenda kwa wizara inayohusika na usalama na kupelekwa kwa NG-CDF ili Waheshimiwa washughulikie mambo ya usalama katika maeneo Bunge yao. view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Ninaunga mkono pakubwa pesa ya NG-CDF iongezewe. Mwenyekiti wa Kamati ya NG- CDF yuko hapa. Kama Mwanachama wa Kamati hiyo, nashauri tukae chini pamoja na Budgetand Appropriations Committee na tuangalie haya mapendekezo ambayo tumeleta ili tubadilishe haya mambo. Wabunge wengi wanalalamika kuhusu suala hili. Wabunge wengine wako na mashule 200 katika maeneo Bunge yao na hawajui vile watakavyopeana bursaries kwa sababu The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposes only. Acertified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: ya uchache wa pesa ilhali wamebandikwa majukumu kwamba kuna pesa wanapewa za Serikali katika kusimamia maeneo haya. view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Kuna changamoto ambazo tunapata kama Kamati katika suala la kuridhisha haya mambo kwa sababu Wabunge wanalalamika. Tuko mwezi wa tatu na utapata ya kwamba maeneo Bunge hayajapata kabisa ule mgao wa NG-CDF wa mwaka huu. Wengine wamepata kama Ksh10 milioni. Wabunge wenzangu wanalalamikia Kamati ya NG-CDF. Ukweli ni kwamba sisi kama Kamati, tunajitahidi vilivyo kuhakikisha kwamba Wabunge wamepata pesa kwa sababu tunaelewa hali hii. Matatizo yako katika Wizara ya Fedha katika kutoa pesa hizi. Ningewaambia Wabunge wenzangu kwamba tunajitahidi kuhakikisha tumefuatilia jambo hili kwa sababu tunajua zile changamoto Wabunge wanapitia katika maeneo Bunge yao. Wizara ya Fedha haijatilia maanani kuhakikisha ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus