Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 381 to 390 of 512.

  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Asante Mheshimiwa Naibu Spika wa Muda. Ningependa kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa fursa hii ya kuchangia Ripoti hii ambayo tunayo hapa Bungeni. Mimi ni Mwanakamati wa Kamati ya Hazina ya Maendeleo ya Maeneo Bunge. Vile vile, ningependa kumshukuru Mwenyekiti kwa kuileta Ripoti hii. Waheshimiwa wamezungumzia masuala ya Kamati ya Hazina ya Maendeleo ya Maeneo Bunge. Vile vile, ningependa kumpongeza Mheshimiwa Angwenyi kwa kuelezea historia fupi ya namna Hazina hiyo ilivyoanza. Ni takriban miaka 15 tangu Hazina hiyo ianzishwe. Ukweli ni kwamba Wakenya wengi wameiona faida ya Hazina hiyo tangu ianze hadi sasa inavyoendelea. Wengi waliochangia wamezungumzia changamoto nyingi ambazo ... view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Ni jambo la kusikitisha kuona pakubwa kwamba hali hii bado inaendelea katika nchi yetu. Utakubaliana na mimi ya kwamba Constituencies Development Fund (CDF) ilibadilishwa jina kuongezwa jina kwamba ni pesa za Serikali kuu kutokana na mipangilio ya Serikali ya ugatuzi. Hapo awali CDF ilikuwa na changamoto baada ya Wakenya kupitisha Katiba. Walisema ya kwamba CDF hairuhusiwi kuwepo tena kwa sababu ya ugatuzi. Katika historia fupi, baada ya hapo, masuala haya yalifika mpaka mahakamani na ikabadilishwa jina kuongezwa kwamba ni fedha za Serikali ya kitaifa. Waheshimiwa wengi ambao wamechangia leo wanalalamika kwamba hizi fedha ni kidogo kwa sababu majukumu na matakwa ... view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Vile vile, katika Bajeti ya nchi hii wakati pesa hizi zinavyogawanywa, fedha nyingi zinapelekwa katika wizara zinazohusika na elimu na usalama. Tukienda mashinani kama Waheshimiwa, tunaulizwa na wananchi masuala ya elimu na usalama. Wananchi wanatarajia pesa za NG-CDF zisimamie usalama na elimu. Nina swali kwa Serikali ya kitaifa. Kwa nini inapeana pesa nyingi kwa Wizara ya Elimu na kuna majukumu ambayo wamepeana kusimamiwa na NG-CDF katika masuala ya elimu? Maoni yangu katika jambo hili ni kuwa wakati Bajeti ya nchi hii inapopangwa, asilimia kubwa ya fedha ambazo zinaenda kwa Wizara ya Elimu ziletwe katika kuimarisha NG-CDF. Katika neno “NG-CDF”, kuna ... view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Tukiwa mashinani, walinda usalama kama machifu wanawategemea Wabunge kutekeleza mambo yao ya usalama katika zile sehemu. Serikali hii inapeana pesa kwa wizara kama hizi. Kwa hivyo, ningependelea tutenge pesa fulani kutoka kwa zile fedha ambazo zinaenda kwa wizara inayohusika na usalama na kupelekwa kwa NG-CDF ili Waheshimiwa washughulikie mambo ya usalama katika maeneo Bunge yao. view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Ninaunga mkono pakubwa pesa ya NG-CDF iongezewe. Mwenyekiti wa Kamati ya NG- CDF yuko hapa. Kama Mwanachama wa Kamati hiyo, nashauri tukae chini pamoja na Budgetand Appropriations Committee na tuangalie haya mapendekezo ambayo tumeleta ili tubadilishe haya mambo. Wabunge wengi wanalalamika kuhusu suala hili. Wabunge wengine wako na mashule 200 katika maeneo Bunge yao na hawajui vile watakavyopeana bursaries kwa sababu The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposes only. Acertified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: ya uchache wa pesa ilhali wamebandikwa majukumu kwamba kuna pesa wanapewa za Serikali katika kusimamia maeneo haya. view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Kuna changamoto ambazo tunapata kama Kamati katika suala la kuridhisha haya mambo kwa sababu Wabunge wanalalamika. Tuko mwezi wa tatu na utapata ya kwamba maeneo Bunge hayajapata kabisa ule mgao wa NG-CDF wa mwaka huu. Wengine wamepata kama Ksh10 milioni. Wabunge wenzangu wanalalamikia Kamati ya NG-CDF. Ukweli ni kwamba sisi kama Kamati, tunajitahidi vilivyo kuhakikisha kwamba Wabunge wamepata pesa kwa sababu tunaelewa hali hii. Matatizo yako katika Wizara ya Fedha katika kutoa pesa hizi. Ningewaambia Wabunge wenzangu kwamba tunajitahidi kuhakikisha tumefuatilia jambo hili kwa sababu tunajua zile changamoto Wabunge wanapitia katika maeneo Bunge yao. Wizara ya Fedha haijatilia maanani kuhakikisha ... view
  • 5 Mar 2019 in National Assembly: Ningependa kusema ya kwamba hapo awali, mgao wa NG-CDF ulikuwa unaangazia masuala ya umaskini na wingi wa watu katika sehemu. Waheshimiwa wanalalamika kuhusu suala hili. Tutafute njia ya kuhakikisha kwamba kuna sehemu ambazo zinahitaji hizi fedha zaidi kuliko sehemu zingine. Ninaunga mkono jambo hili, lakini ifahamike pakubwa kwamba kuna miegezo mingine ambayo tunafaa kuangalia. Kwa mfano, idadi ya watu siyo suala la kuzingatiwa kikamilifu. Suala la kuzingatiwa kikamilifu ni umaskini. Unaweza kupata idadi ya watu katika sehemu ni kidogo lakini umaskini ni mkubwa sana. Kwa hivyo, tuwe waangalifu kama Waheshimiwa katika kutaka kurekebisha haya mambo tusije tukadhulumu sehemu zingine na ... view
  • 27 Feb 2019 in National Assembly: Ahsante, Mhe. Naibu Spika wa Muda. Ningependa kuungana na wenzangu katika kuwapongeza wanakamati kwa kazi yao nzuri ambayo wamefanya kuhusiana na Ripoti hii ambayo imeletwa Bungeni. Kwa kweli, wengi wamechangia kuhusiana na masuala haya, na haswa kuhusu pesa za NG-CDF – Hazina ambayo imekuwepo kuanzia mwaka wa 2003. Ni vyema Wakenya wafahamu utaratibu wa NG-CDF na mabadiliko ambayo yamefanyika katika NG-CDF. Ukweli ni kwamba fedha hizi, kuanzia mwaka wa 2003, zimeleta mabadiliko makubwa nchini Kenya. Leo kuna mengi yanayozungumziwa kuhusiana na maendeleo na mengineo lakini, ukweli ni kwamba, fedha hizi zimeonekana katika sehemu za mashinani. Fedha hizi zimeleta maendeleo makubwa ... view
  • 27 Feb 2019 in National Assembly: Tatizo ambalo bado lipo mpaka sasa ni kwamba Wakenya bado wanahitaji maendeleo. Changamoto ni nyingi. Ni lazima Serikali ifahamu kikamilifu. Miongoni mwa mbinu zilizotumika kugawanya fedha hizi katika maeneo Bunge hapo ni idadi ya watu na hali ya umaskini katika sehemu hizo. Utakubaliana nami kwamba baadaye, mbinu hiyo ilibadilishwa na kila eneo Bunge likawa linapokea kiwango sawia cha fedha kutoka NG-CDF. Hakuna eneo Bunge linalopata pesa nyingi kuliko lingine. Ukweli ni kwamba maeneo Bunge hayafanani. Kuna sehemu ambazo zimeendelea na kuna sehemu ambazo bado kuna udhaifu na umasikini mkubwa. Mbali na kusema kwamba tuangalie idadi ya watu, sidhani ni kiegezo ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus