16 Oct 2019 in National Assembly:
Hon. Speaker, pursuant to the provisions of Standing Order No.42(A)(5), I wish to ask the Cabinet Secretary for Transport, Infrastructure, Housing and Urban Development: (a) When will the Ndau and Kizingitini seawalls, which have been under construction for the last 15 years, be completed? (b) What measures has the Ministry put in place to ensure that the said construction is completed?
view
3 Oct 2019 in National Assembly:
Asante, Mhe. Naibu Spika wa Muda. Ninataka nianze kwa kuwapongeza wanakamati kwa kazi waliofanya, lakini ninataka kusimama kwa msimamo wa kupinga Ripoti hii. Waswahili husema “mficha uchi hazai”. Ndugu zetu wamepewa kazi hii, sababu kubwa ni mateso ambayo Wakenya wamekuwa wakipitia katika nchi hiyo. Nikiwauliza Waheshimiwa, ni kwa nini hawakupelekwa nchi nyingine ilhali kuna Wakenya wanaofanya kazi katika nchi nyingine pia? Kwa nini wakapelekwa Saudi Arabia kuchunguza mambo fulani, hususan yale yanayojiri; Wakenya wanavyokufa kwa njia zisizoeleweka? Ni masikitiko makubwa sana kuona kwamba nchi yetu yaendeshwa bila utaratibu. Leo hii tunaambiwa kuna Wakenya wanaenda kule kwa njia ambazo hazieleweki. Lakini ...
view
3 Oct 2019 in National Assembly:
Mhe. Naibu Spika wa Muda, kama nilivyosema, ni masikitiko makubwa kwa sababu nilitarajia Kamati hii ichukue majina ya Wakenya wote waliorudishwa nchini wakiwa wameathirika kwa kudhulumia na kuteswa, halafu waende kule wakafanye uchunguzi kuhusu waathiriwa hao.
view
3 Oct 2019 in National Assembly:
Mwisho, ninaamini kuwa kweli watu wengi wanapenda kuenda Saudi Arabia kufanya kazi kwa sababu ya hali ya kiuchumi nchini mwetu.
view
2 Oct 2019 in National Assembly:
Thank you, Hon. Temporary Deputy Speaker. Due to the time remaining and it looks like many Members are interested in speaking to this Motion, is it in order for the time to be limited to three minutes, instead of five per Member?
view
2 Oct 2019 in National Assembly:
Asante Naibu Spika wa Muda. Kwanza kabisa, ningependa kuungana na wenzangu kutoa rambirambi zangu za pole kwa familia waliopoteza wapendwa wao.Vile vile, ningependa kumpongeza Mhe. Mishi kwa kuileta Hoja hii Bungeni. Naibu Spika wa Muda, Waheshimiwa wengi wamezungumza kwa masikitiko makubwa na kwa kuzingatia yaliyojiri kutokana na kisa hiki cha hivi majuzi cha kupoteza ndugu zetu Wakenya katika mkasa wa feri. Vile vile, ni masikitiko makuu kwa Wakenya. Ni majonzi makubwa kwamba, hata baada ya tukio hili, mpaka sasa, hakuna juhudi zozote ambazo zimefanywa kusawazisha hii mahali. Kwa kweli, ni masikitiko makubwa, na ni aibu kwa nchi hii kwa jumla. ...
view
25 Sep 2019 in National Assembly:
Asante sana, Mhe. Naibu Spika wa Muda. Kwanza, ningependa kumpongeza Mheshimiwa kwa kuleta Hoja hii. Tunakubaliana sote kuwa ni Hoja muhimu sana na tunahitaji kuijadili kwa namna yake. Ukweli ni kwamba, mzazi yeyote anayepeleka mtoto shuleni huwa na malengo kwamba mtoto yule amalize shule na baadaye, awe kijana mwenye mwongozo katika ulimwengu wa leo. Lakini kwa masikitiko makubwa, suala hili limeonekana halina mwongozo na utaratibu. Sitaki niilaumu Serikali lakini nataka kuipa changamoto. Hii ni kwa sababu vijana wengi wanaomaliza shule wanapotea katika njia ambazo hazijulikani. Vijana wengi hawana kazi kwa sababu ya tatizo hilo. Kwa maana hiyo, kuna umuhimu mkubwa ...
view
25 Sep 2019 in National Assembly:
Inasikitisha kuona kwamba wengi wa vijana wetu hawana mwongozo katika hali hii. Hawana kazi wala ujuzi na hawajasomea taaluma nyingine. Sio kwa sababu vijana hawataki kufanya hivyo, ni kwa sababu ya utaratibu na mpangilio wa Serikali yetu. Hiyo ndiyo inafanya vijana wakose imani katika jambo hili. Nikizungumzia Eneo Bunge la Lamu, hivi sasa, watu wengi wanafahamu kwamba tuko na Lamu Port-South Sudan-Ethiopia-Transport Corridor Project (LAPSSET). Lakini kwa masikitiko makubwa, jambo ambalo Serikali haijafanya ni kuhakikisha kwamba mradi huu umewasaidia vijana. Zile nafasi 1,000 ambazo ziliahidiwa na Serikali kwa vijana katika LAPSSET, hadi sasa, hazijawekwa bayana. Jambo hili halijafanyika. Kutokana na ...
view
18 Sep 2019 in National Assembly:
Asante. Ningependa kuchukua fursa hii kuunga mkono Mswada huu na vilevile kumpongeza pakubwa Mbunge aliyeuleta hapa kwa sababu suala la ajira ni suala nyeti. Aliyeuleta Mswada huu amelenga masuala ya akina mama wanaofanya kazi, haswa wakati wanapojifungua na namna watakavyopata nafasi ya kupumzika watakapokuwa wakiwalea watoto wao.
view
18 Sep 2019 in National Assembly:
Ukweli ni kwamba Waheshimiwa wengi wanaposimama kuchangia Mswada huu wanazungumzia neno “ajira” kwa ujumla katika nchi hii. Ukweli ni kwamba ile hali ya ajira katika nchi hii ni hali ambayo inahitaji kupewa kipaumbele tunapojadili kuhusu suala hili.
view