19 Feb 2019 in National Assembly:
panapotokezea matatizo tuna mwongozo kamili wa kuhakikisha kwamba matizo hayaleti athari ama hayatatanishi utaratibu ambao unaendelea hivi sasa wa kisheria. Naunga mkono na naungana na wenzangu kwa kupendekeza na kuhakikisha ya kwamba haya mambo na utaratibu huu umepitishwa. Ningependa kukomea hapa. Asante.
view
13 Feb 2019 in National Assembly:
Asante, Mhe. Spika wa Muda. Kwanza ningependa kumushukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia kurudi tena hapa Bungeni kwa mwaka wa 2019 baada ya likizo ndefu.
view
13 Feb 2019 in National Assembly:
Ningependa kuungana na wenzangu kuunga mkono mapendekezo haya ya namna fedha za umma zitadhibitiwa kiumakini na kiuangalifu. Kwa kweli, hili ni suala nyeti. Tunapolizungumzia ni lazima tulifahamu kwa namna zote. Kwanza, nataka tufahamu takribani asilimia 25 za fedha zinazopatikana kutokana na mapato ya nchi zinaelekezwa kwa serikali za kaunti. Hivyo basi kuna umuhimu wa kuwa na mwongozo kuhusiana na pesa hizi wakati Serikali inazipeana kwa kaunti.
view
13 Feb 2019 in National Assembly:
Vile vile, tumeshuhudia mara nyingi sana nchi hii ikilalamika kuhusiana na masuala ya uchumi na matatizo mengineo. Naamini pakubwa haya yanasababishwa na hali ya kutodhibiti kile tunachopata kwa uangalifu. Asilimia 25 ambayo inaenda kwa kaunti sio pesa kidogo. Lakini utapata ya kwamba pesa hizi zinazoenda kwa kaunti, kaunti nyingi bado zinalalamika kuhusiana na miradi na maendeleo. Naamini pakubwa kwamba kama utaratibu huu ambao tuaujadili hapa utaweza kutumika kiusawa, nina imani kwamba matatizo kama haya hayatashuhudiwa mbeleni. Ukweli ni kwamba nchi hii ina umuhimu mkubwa wa kuhakikisha ya kwamba fedha za umma zimedhibitiwa na zimetumika kiusawa na kiuangalifu.
view
13 Feb 2019 in National Assembly:
Utakubaliana nami kwamba matatizo haya yanapatikana kwa wahusika wakuu wanaoendesha mwongozo kama huu ambao tunaujadili hapa Bungeni. Ni matumaini yangu makubwa na nina imani kwamba kama mwongozo huu utafuatwa kikamilifu na vile unavyotakikana, basi fedha za umma zitadhibitika na matarajio makubwa ya wananchi yatapatikana.
view
13 Feb 2019 in National Assembly:
Vile vile, mbali ya kwamba tunayazungumzia haya leo ama tunayajadili marekebisho haya, ni lazima tukubali matatizo yako na ni sisi tunayasababisha kupitia serikali za kaunti ama Serikali Kuu. Utapata kwamba utaratibu huu ambao tunaujadili hapa, wengine wanautumia kama sababu kwa mambo yao ya kibinafsi. Mfano ni namna serikali za kaunti zinavyotaka kutumia pesa zao. Lakini hapa katikati, hofu ni kwamba kuna baaadhi ya Wakenya ambao ni wahusika katika kutumia utaratibu huu. Wanatumia mbinu za kusikitisha badala ya kufanya mambo kiutaratibu hasa kwa kuzingatia mwongozo huu ambao tunazungumzia. Kuna miradi ambayo inahitaji kufanywa kila mwaka lakini hucheleweshwa kwa sababu ya mwongozo ...
view
13 Feb 2019 in National Assembly:
kwamba tumetembea na mwongozo huu kikamilifu. Tusilete mvutano kati ya wahusika na kaunti. Kuna wakati pengine mkandarasi amefanya kazi yake kwa utaratibu lakini inapofika wakati wa kulipwa, kwa sababu ya vigezo hivyo ambavyo tumeweka hapa, serikali ya kaunti inasema kwamba utaratibu ndio una matatizo. Hivyo basi, mkandarasi anachelewa kupewa pesa zake kwa sababu kama hiyo. Ninaamini kwamba ni mwongozo mzuri. Wakenya wanahitaji huduma bora. Mbali na hayo, ninaamini pakubwa huduma hizi zitapakitana ikiwa kutakuwa na mwongozo kamilifu na viongozi husika wataweza kumakinika na kuhakikisha wamekubali kufuata utaratibu na sharia zilizowekwa.
view
13 Feb 2019 in National Assembly:
Magavana tunawajua. Sifa za wengi wao zinajulikana. Siyo wote wenye sifa za kupendeza. Udhaifu upo ndani ya baadhi ya ndugu zetu. Kutokana na hali hii ambayo tunajadili sasa hivi, ni vyema kuhakikisha kwamba mwongozo huu umewekwa vikwazo vya kisheria namna inavyotakikana. Hivyo, tutahakikisha kwamba yeyote ambaye ni mhusika katika kaunti ni mhusika wa kuendeleza kaunti. Masuala ya fedha yatadhibitiwa kwa njia ya furaha kubwa. Serikali ya kitaifa yafaa kuhakikisha kwamba imepeana mwongozo kwa serikali za kaunti kuhusu matumizi ya fedha. Tumeshuhudia mara kadhaa matatizo katika kaunti tofauti tofauti. Mimi naona yamesababishwa na hali ambayo haikuwa hapo mbeleni ya kuweka utaratibu ...
view
5 Dec 2018 in National Assembly:
Athman (Lamu East, JP): Asante Mheshimiwa Naibu Spika wa Muda. Ningependa kumpongeza ndugu yetu ambaye ameleta Hoja hii Bungeni. Vile vile, niwapongeze Wabunge ambao wameweza kuchangia Hoja hii. La muhimu kwanza ni lazima kufahamu kama viongozi malengo na umuhimu wa Hoja hii ni nini. Tunaweza kuzungumza na kujadili lakini mwishowe ikawa umuhimu wake usipatikane kwa jamii.
view