Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 441 to 450 of 515.

  • 11 Oct 2017 in National Assembly: zingeelekezwa katika masuala haya ya ukulima, zipewe wakulima, nafikiri kila mahala ama sehemu katika nchi hii, watu wangeweza kufanya ukulima. view
  • 11 Oct 2017 in National Assembly: Mimi ningependa kuwaambia ndugu zangu Waheshimiwa kwamba mambo kama haya ni muhimu tuyajadili kwa namna inayotakikana. Tunafaa tujadili ni vipi mkulima atalipwa pesa wakati ameleta bidhaa yake. Ni vipi tutaweza kulizungumzia suala la miwa peke yake kwa sababu uchumi wetu ni ukulima na matatizo yako kila mahali. Leo, Bunge hili litapitisha suala hili la wakulima wa miwa wasaidike kwa namna hii, lakini je, kesho tutarudia tena tuanze kuzungumza na wengine? Naomba ile kamati ambayo itaundwa iweze kuzingatia zile nyanja husika na kuweza kulisuluhisha suala hili la kuhakikisha kwamba nchi hii haiko tena katika ile taswira ya kuonekana kwamba watu wako ... view
  • 11 Oct 2017 in National Assembly: Ni muhimu sana Serikali izingatie wakulima na ihakikishe kwamba imeweza kusaidia viwanda vyote na wakulima wote. Nina imani kubwa litakapofanyika hivyo, basi tutasahau masuala ya matatizo ya vyakula na kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi hii. Leo, kilo moja ya sukari ni mia tatu ama mia nne. Kuna watu wameacha kunywa chai kwa sababu hawawezi kununua sukari. Leo tunajadili vipi mkulima atalipwa pesa yake wakati ameleta bidhaa. Tunamjadili vipi yule anainunua hii sukari ili bei ipungue? Njia ya kuweza kumsaidia yule mwenye kununua bidhaa hii ni kuhakikisha ya kwamba wakulima wamesaidika na tumeweka mambo ya ukulima kisawasawa. Bidhaa zile zinapofika ... view
  • 11 Oct 2017 in National Assembly: Ahsante na naunga mkono Hoja hii, Mhe. Spika wa Muda. view
  • 16 Mar 2017 in National Assembly: On a point of order, Hon. Temporary Deputy Speaker. view
  • 16 Mar 2017 in National Assembly: Thank you, Hon. Temporary Deputy Speaker. I think we are discussing a very important Motion today and yet we are only four members in this Chamber. I do not think we can proceed with this important Motion for our country while we are only four Members. The decision that will be made from this Motion will affect this country and it is wrong for only four members to make it. I do not think we have quorum under Standing Order No.35 to proceed with this Motion. Thank you. view
  • 7 Jun 2016 in National Assembly: Asante, Mhe. Naibu Spika wa Muda. Kwa kweli, Hoja hii ni ya kushangaza. Kuzungumza kuhusu Bunge hili kupitisha mkopo wa Kshs27.3 bilioni ni jambo la kushangaza. Huu mradi ambao unafanyika Mombasa ni mradi ambao tukiwa watu wa Pwani na Wakenya, tungependa uwe kwa sababu ya kuinua uchumi wa nchi hii na uchumi wa Pwani. La kushangaza ni kwamba jambo hili limeletwa Bungeni ilhali mradi huu unaendelea. Ninashindwa pesa hizi zilikuwa zimepangiwa kulipwa namna gani ilhali huu ni mradi ambao tayari umeanza. Isitoshe, linalonishangaza ni kwamba mbali na kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kuinua uchumi wetu, ni vipi tutaweza kusaidia sehemu ... view
  • 7 Jun 2016 in National Assembly: Kwa kweli, hatuwezi kukataa maendeleo yasifanyike, na tukiwa kama viongonzi tuna kila haki kuhakikisha kwamba tumesaidia nchi hii katika swala nzima la uchumi wetu. Lakini, mambo mengine kama haya yanahitaji maswala mengi kutoka kwetu sisi viongozi. Kwa mfano, tunasema kwamba tutachukua takribani miaka 34 kulipa deni hili na ilhali tuna uhakika KPA ni shirika moja katika nchi hii linaloingiza pesa nyingi sana. La ajabu ni kwamba leo Serikali inajiongezea madeni kama haya, na nina imani kwamba mzigo huu utakuwa wa wananchi. Hili linatendeka ilhali ushuru unaotozwa mizigo katika bandari ni wa juu. Baadaye wanaoleta bidhaa ama kufanya biashara katika nchi ... view
  • 7 Jun 2016 in National Assembly: Kama viongozi tunahitaji kujadiliana pakubwa kabla hatujajiweka katika madeni kama haya ambayo mwisho wake kama ninavyosema, yatakuwa mzigo wa mwanachi wa Kenya wa kawaida. Mimi ningependa kusema kwamba kuna miradi mingi ambayo inahitaji kufanyika na ni bora zaidi. Kama hizi pesa zitatumika, zitafungua milango nchini na kuinua uchumi. view
  • 7 Jun 2016 in National Assembly: Kama nilivyosema, tunahitaji maendeleo na uchumi uinuke katika nchi hii lakini ninaona Hoja hii ina maswala mengi ambayo tunahitaji kufahamu kupitia kwa Serikali ama kupitia wahusika. Hatuoni haja kama viongozi kupitisha pesa hizi halafu ziwe mzigo kwa wananchi ama kupitisha pesa hizi ilhali kuna sehemu zingine kama nilivyosema kama Lamu zinazohitaji pesa hizi ili miradi ambayo imekwama kama hii iendelee. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus