Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 71 to 80 of 512.

  • 26 Sep 2024 in National Assembly: Mhe. Spika, haya mambo yanayoongelewa hapa si ya kweli. Dadangu Mhe. Muthoni amekuja hapa Bungeni kwa sababu hatujahusishwa. Hakuna kiongozi yeyote aliyeitwa, wala hakuna aliyepinga. Asiseme eti political leaders . Mimi sijawahi kuitwa, wala Mhe. Muthama au Mhe. Muthoni. Hao viongozi wengine ni akina nani, ilhali Kaunti ya Lamu iko na Constituency mbili na Women Representative mmoja peke yake? Hatujawahi kuitwa. Huo ni uongo. Jambo la pili ni kuwa kuna kigezo hapo… view
  • 26 Sep 2024 in National Assembly: Mhe. Spika, sasa niseme nini badala yake? Kwa sababu sio ukweli huo. view
  • 26 Sep 2024 in National Assembly: Well guided, Hon. Speaker. Jambo jingine linalotumika Lamu ni kwamba ukiuliza kama pengine kuna uzembe mahali, wanasema ni view
  • 26 Sep 2024 in National Assembly: . Hakuna utovu wa usalama Lamu. Tunaishi na kuenda popote tunapotaka. Hapo Hindi, watu ni wengi na miradi pia ni mingi, kama vile LAPSSET. Utovu wa usalama unatokea wapi sasa? Wamekosa kusema ukweli, na badala yake kutumia kigezo cha utovu wa usalama. Ardhi, sijui kama ni hii ya Swahili Scheme, kwa sababu imeleta utata. Kila gavana akiingia analeta sheria zake, na mambo yasipoenda, anasonga hapo hapo; lakini sio kwamba ni Memberof Parliament au political leaders . Ningeomba huyo Waziri aje ajibu au nilitengeneze swali hili kivingine. Niambieni ni vipi nitafanya. Kwa sasa ni kama tu kumgombeza Mwenyekiti bure, naye hajui ... view
  • 25 Sep 2024 in National Assembly: Ahsante. Waziri, mwanzo, ningependa kukupongeza na kukushukuru wakati ulikuwa Waziri wa Barabara, Usafiri na Kazi za Umma. Ulijua Lamu Mashariki haina barabara na ukafanya mipango mizuri. Ahsante. Saa hii pia, ningependa ufikirie kuhusu Lamu Mashariki katika upande wa michezo. Hakika kwa miaka kadhaa au tangu uhuru upatikane, hakuna kitu kimefanywa katika Eneo Bunge la Lamu Mashariki katika upande wa michezo. Nimesikia mipango yote ambayo umezungumzia. Kaunti ya Lamu haina uwanja wa Serikali ya Kitaifa wala ya kaunti. Katika mipangilio yote, sisi tunaachwa nyuma. Nakuomba kwa hisani yako kama unaweza kutaja kitu kimoja ambacho kimefanywa Lamu Mashariki na hii Wizara. Niambie ... view
  • 24 Sep 2024 in National Assembly: Ahsante, Mhe. Naibu Spika kwa kunipa nafasi hii nami nipate kuzungumza kuhusu NG-CDF. Katika maeneo bunge mengi, pesa za NG-CDF ndizo pesa pekee tunazotarajia kufanyia maendeleo. Eneo Bunge la Lamu Mashariki na maeneo bunge mengine mengi yamebaguliwa kwenye mipango ya maendeleo. Kwa mfano, tukiangalia rekodi, tutaona kwamba kwenye Bajeti ya mwaka uliopita, Eneo Bunge la Lamu Mashariki lilipewa Ksh4 milioni, ilhali kuna eneo bunge lingine ambalo lilipewa Ksh450 milioni. Pesa za NG-CDF ndizo pesa pekee ambazo hazihusishwi na ubabe kwa sababu kila eneo bunge linapata mgao wake na linajipangia miradi yake kulingana na jinsi sheria inavyosema. Katika Serikali kuu, pesa ... view
  • 24 Sep 2024 in National Assembly: tunaelekezwa wapi. Ninavyozungumza, Rais ametusaidia. Kule kwetu, viwango vya elimu viko chini sana, na madhara kwetu yameonekana. Vijana wameonekana wakienda wanavyokwenda ikabidi tuwasomeshe. Tukapewa nafasi ya kuajiri walimu lakini miongoni mwa walioajiriwa, ni waalimu wawili peke yake kutoka katika Lamu Mashariki. Hazina ya NG-CDF ilikuwa inatuokoa… view
  • 24 Sep 2024 in National Assembly: Hivi sasa, katika chuo cha Waislamu cha Mafunzo ya Ualimu, na kile cha Mafunzo ya Ualimu cha Shanzu, tunasomesha zaidi ya wanafunzi 100 kupitia usaidiza wa hazina ya NG-CDF. Hao wanaosoma wataenda wapi? Leo hii niko na msukumo mkubwa. Mkwe wake Nordin, ambaye ni Mwenyekti wa Board, amewafukuza wanafunzi hao kutoka chuoni kama njia moja ya kuniadhibu mimi kwa sababu sijakubali Ishakani na Dar-es-Salaam Point ziende Ijara. Hivi sasa, wanafunzi wamefukuzwa kutoka chuoni kwa sababu hatujalipa hiyo pesa. Hazina ya NG-CDF ikiondolewa, tutaenda wapi? view
  • 17 Sep 2024 in National Assembly: Asante, Mhe. Spika. Nami ninatoa rambirambi zangu, za familia yangu na watu wa Lamu kwa jumla, kwa Mheshimiwa aliyefariki. Ningependa pia kuchukua nafasi hii kutoa rambirambi zangu kwa familia ya Naibu wa Gavana wa Lamu aliyefariki. Mungu aiweke roho yake pahali pema. Alikuwa mtu mzuri mwenye ukakamavu na maskini amewacha familia ndogo. Mwenyezi Mungu aisaidie familia yake na ajaze pengo alilowacha. Kwa Gavana wetu wa Lamu na wakaazi wa Lamu, mwenyezi Mungu atupe subira na badali. Mungu amwezeshe Gavana kufanya uamuzi wa busara. Ninatoa pole kwa watu wa Mpeketoni, familia na watu wote wa Lamu kwa niaba ya familia yangu ... view
  • 14 Aug 2024 in National Assembly: Ahsante Mhe. Spika kwa kunipatia nafasi nami niwakaribishe Cambridge Link School Bungeni. Ningependa kurekebisha jambo Mhe. Spika ametaja kidogo. Kwa vile ninatoka sehemu za Lamu, imechukuliwa kuwa hii shule nayo inatoka pale. Ilhali, inatoka sehemu za Nyali, Mombasa. Ninawakaribisha sana. Niliwatafutia nafasi ili wakuje Bungeni. Waliona nimewaleta wanafunzi wa Lamu wengi, na wao pia wakataka kufika mahali hapa. Mtoto wa dadangu, Jamil, anasoma katika hii shule, na akawa anataka kufika mahali hapa. Na hivyo ndivyo waalimu walijiandaa kwa hii safari. Karibuni sana. Ninawahisi msome kwa bidii maana nyinyi ndio viongozi wa kesho. Katikati yenu, tuko na marais, magavana, wabunge na ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus