Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 81 to 90 of 515.

  • 24 Sep 2024 in National Assembly: Hivi sasa, katika chuo cha Waislamu cha Mafunzo ya Ualimu, na kile cha Mafunzo ya Ualimu cha Shanzu, tunasomesha zaidi ya wanafunzi 100 kupitia usaidiza wa hazina ya NG-CDF. Hao wanaosoma wataenda wapi? Leo hii niko na msukumo mkubwa. Mkwe wake Nordin, ambaye ni Mwenyekti wa Board, amewafukuza wanafunzi hao kutoka chuoni kama njia moja ya kuniadhibu mimi kwa sababu sijakubali Ishakani na Dar-es-Salaam Point ziende Ijara. Hivi sasa, wanafunzi wamefukuzwa kutoka chuoni kwa sababu hatujalipa hiyo pesa. Hazina ya NG-CDF ikiondolewa, tutaenda wapi? view
  • 17 Sep 2024 in National Assembly: Asante, Mhe. Spika. Nami ninatoa rambirambi zangu, za familia yangu na watu wa Lamu kwa jumla, kwa Mheshimiwa aliyefariki. Ningependa pia kuchukua nafasi hii kutoa rambirambi zangu kwa familia ya Naibu wa Gavana wa Lamu aliyefariki. Mungu aiweke roho yake pahali pema. Alikuwa mtu mzuri mwenye ukakamavu na maskini amewacha familia ndogo. Mwenyezi Mungu aisaidie familia yake na ajaze pengo alilowacha. Kwa Gavana wetu wa Lamu na wakaazi wa Lamu, mwenyezi Mungu atupe subira na badali. Mungu amwezeshe Gavana kufanya uamuzi wa busara. Ninatoa pole kwa watu wa Mpeketoni, familia na watu wote wa Lamu kwa niaba ya familia yangu ... view
  • 14 Aug 2024 in National Assembly: Ahsante Mhe. Spika kwa kunipatia nafasi nami niwakaribishe Cambridge Link School Bungeni. Ningependa kurekebisha jambo Mhe. Spika ametaja kidogo. Kwa vile ninatoka sehemu za Lamu, imechukuliwa kuwa hii shule nayo inatoka pale. Ilhali, inatoka sehemu za Nyali, Mombasa. Ninawakaribisha sana. Niliwatafutia nafasi ili wakuje Bungeni. Waliona nimewaleta wanafunzi wa Lamu wengi, na wao pia wakataka kufika mahali hapa. Mtoto wa dadangu, Jamil, anasoma katika hii shule, na akawa anataka kufika mahali hapa. Na hivyo ndivyo waalimu walijiandaa kwa hii safari. Karibuni sana. Ninawahisi msome kwa bidii maana nyinyi ndio viongozi wa kesho. Katikati yenu, tuko na marais, magavana, wabunge na ... view
  • 14 Aug 2024 in National Assembly: Karibuni sana na ninawatakia kila la heri. Hii ni shule nzuri iliyo na sifa kocho kocho. Waalimu ni wazuri na wanafunzi pia wako na nidhamu, na tunaifurahia. view
  • 14 Aug 2024 in National Assembly: Ahsanteni, na kila la heri. Karibuni view
  • 13 Aug 2024 in National Assembly: Bwana Spika, ninaomba tuwe makini sana hapa Bungeni. Si sawa tukisema tusifuate dini. Katiba yetu inatambua dini zote. Katika Uislamu, kujiweka kitanzi ni kati ya dhambi kubwa sana, na ninaamini kwamba hata kwenye Bibilia ni hivyo. Lakini pia Qurani inasema kwamba watu ambao hawaandikiwi madhambi ni watatu; yule ambaye hana akili mpaka wakati akili itakaporudi, mtoto mdogo na yule ambaye amelala mpaka The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 13 Aug 2024 in National Assembly: atakapoamka. Kwa hivyo, kama kutakuwa na njia ya kuhakikisha kweli hana akili, hapo tutasema hana dhambi. Kuna watu ambao wanatumia hizi nafasi vibaya; kwa mfano, mtu akikosana na bwanake, pengine ameoa bibi mwingine, anakunywa na kuleta sarakasi. Huyo anafaa kuadhibiwa. Sisi wengine angalau tunakubali wanne. Kwa hivyo, mambo mengine yasiingizwe katikati na mtu akatumia nafasi hiyo. Ahsante, Bwana Spika. view
  • 8 Aug 2024 in National Assembly: Mheshimiwa Spika, ukweli ni kwamba jenereta ndogo imepelekwa sasa hivi, ipo Kiunga na mafundi wanafunga. Hii iliyopelekwa ni ile imerekebishwa. Pia kwa hiyo, tunashukuru lakini ile jenereta kubwa mpya bado iko Mkowe. Twataka wafanye bidii waipeleke ile kubwa kwa sababu wamejua kuwa kuna matatizo. Ile ndogo imelemewa haiwezi peke yake ndio mkaitisha ile kubwa. view
  • 8 Aug 2024 in National Assembly: Kitu kingine ni kwamba hii stima imepotea. Niliuliza swali nafikiri tarehe ishirini na tano mwezi wa nne na nikajibiwa tarehe thelathini na moja mwezi wa sita. Wewe ulipotoa amri ya kusema jenereta ipelekwe, hilo jambo limetendeka kwa siku kumi. Kwa nini hizo siku zote tangu nilipouliza swali hawakufanya bidii watu wangu wakapata stima? Watu wamekuwa wakiteseka. Kwa hivyo, Mheshimiwa Spika nataka uwapatie watu wangu fidia kwa zile shida walizopata ndio siku ingine wasifanye makosa kama hayo. Kitu kikiharibika kirekebishwe haraka. Asante, Mheshimwa Spika. view
  • 8 Aug 2024 in National Assembly: Mheshimiwa Spika, Bwana Mwenyekiti hafai kudanganya hili Bunge. Jenereta imekuwa Mkowe kwa zaidi ya miezi miwili. Shida tu ilikuwa ni kuitoa Mokowe kuipeleka Kiunga. Sasa shida yangu ni kwamba kwa nini haikutolewa siku zote mpaka wakati Mheshimiwa Spika alisema hapa ndio mumeweza kuitoa? Sasa hizo kazi za wizara zitakuwa zinaachiwa Mheshimiwa Spika? Mpaka Mheshimiwa Spika aseme ndio ifanywe? Ilikuwa Mkowe kwa zaidi ya miezi miwili. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus