Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 81 to 90 of 512.

  • 14 Aug 2024 in National Assembly: Karibuni sana na ninawatakia kila la heri. Hii ni shule nzuri iliyo na sifa kocho kocho. Waalimu ni wazuri na wanafunzi pia wako na nidhamu, na tunaifurahia. view
  • 14 Aug 2024 in National Assembly: Ahsanteni, na kila la heri. Karibuni view
  • 13 Aug 2024 in National Assembly: Bwana Spika, ninaomba tuwe makini sana hapa Bungeni. Si sawa tukisema tusifuate dini. Katiba yetu inatambua dini zote. Katika Uislamu, kujiweka kitanzi ni kati ya dhambi kubwa sana, na ninaamini kwamba hata kwenye Bibilia ni hivyo. Lakini pia Qurani inasema kwamba watu ambao hawaandikiwi madhambi ni watatu; yule ambaye hana akili mpaka wakati akili itakaporudi, mtoto mdogo na yule ambaye amelala mpaka The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor. view
  • 13 Aug 2024 in National Assembly: atakapoamka. Kwa hivyo, kama kutakuwa na njia ya kuhakikisha kweli hana akili, hapo tutasema hana dhambi. Kuna watu ambao wanatumia hizi nafasi vibaya; kwa mfano, mtu akikosana na bwanake, pengine ameoa bibi mwingine, anakunywa na kuleta sarakasi. Huyo anafaa kuadhibiwa. Sisi wengine angalau tunakubali wanne. Kwa hivyo, mambo mengine yasiingizwe katikati na mtu akatumia nafasi hiyo. Ahsante, Bwana Spika. view
  • 8 Aug 2024 in National Assembly: Mheshimiwa Spika, ukweli ni kwamba jenereta ndogo imepelekwa sasa hivi, ipo Kiunga na mafundi wanafunga. Hii iliyopelekwa ni ile imerekebishwa. Pia kwa hiyo, tunashukuru lakini ile jenereta kubwa mpya bado iko Mkowe. Twataka wafanye bidii waipeleke ile kubwa kwa sababu wamejua kuwa kuna matatizo. Ile ndogo imelemewa haiwezi peke yake ndio mkaitisha ile kubwa. view
  • 8 Aug 2024 in National Assembly: Kitu kingine ni kwamba hii stima imepotea. Niliuliza swali nafikiri tarehe ishirini na tano mwezi wa nne na nikajibiwa tarehe thelathini na moja mwezi wa sita. Wewe ulipotoa amri ya kusema jenereta ipelekwe, hilo jambo limetendeka kwa siku kumi. Kwa nini hizo siku zote tangu nilipouliza swali hawakufanya bidii watu wangu wakapata stima? Watu wamekuwa wakiteseka. Kwa hivyo, Mheshimiwa Spika nataka uwapatie watu wangu fidia kwa zile shida walizopata ndio siku ingine wasifanye makosa kama hayo. Kitu kikiharibika kirekebishwe haraka. Asante, Mheshimwa Spika. view
  • 8 Aug 2024 in National Assembly: Mheshimiwa Spika, Bwana Mwenyekiti hafai kudanganya hili Bunge. Jenereta imekuwa Mkowe kwa zaidi ya miezi miwili. Shida tu ilikuwa ni kuitoa Mokowe kuipeleka Kiunga. Sasa shida yangu ni kwamba kwa nini haikutolewa siku zote mpaka wakati Mheshimiwa Spika alisema hapa ndio mumeweza kuitoa? Sasa hizo kazi za wizara zitakuwa zinaachiwa Mheshimiwa Spika? Mpaka Mheshimiwa Spika aseme ndio ifanywe? Ilikuwa Mkowe kwa zaidi ya miezi miwili. view
  • 7 Aug 2024 in National Assembly: Ahsante, Spika wa Muda, kwa kunipatia nafasi hii kuchangia kwa mjadala wa Hoja ya ugonjwa wa kiakili ulioletwa na Mhe. Mishi Mboko. Moja kwa moja ninamuunga mkono kwa njia yoyote ile kuboresha hali ilivyo hapa nchini sasa. Ni jambo la muhimu sana. Sisi kama Wabunge, ni wakilishi wa wananchi. Jambo lolote lile ambalo litafanya mwananchi apate huduma bora, sisi hatuna budi kuliunga mkono. Kuna sababu nyingi za kusababisha haya magonjwa ya kiakili. Kuna sababu ya mihadarati, stigma, kukosa huduma pia hufanya mtu kuwa na fikra nyingi, na mambo mengine mpaka sehemu zingine tu ndio zina shida hizo. Kama kule kwetu, ... view
  • 7 Aug 2024 in National Assembly: Shida ni nyingi kule kwetu. Tuna vijiji 23. Leo sitazungumzia watu wangu tu wa Lamu Mashariki, nitazungumzia hata wale wahudumu wanaokuja kufanya kazi kule. Wanapata shida zaidi hata kushinda wale wananchi wanaishi kule. Kama polisi wakija kule, wanapata shida sana. Inafaa kutafutwe mipangilio maalumu. Hii pia itakuwa mojawapo kusaidia. Polisi akishatumwa Lamu Mashariki akilini anajua kuwa ametumwa kule kwa sababu ni adhabu. Akienda kule naskia anasema kwamba tunawapatia kazi nyingi wale OCS. Afisa huyo wa polisi akifika kule, wiki nzima hafanyi kazi, mpaka watu wakae naye wamueleze polepole ili azoee yale mazingira. Si vizuri kuweka afisa wa polisi kule kwa ... view
  • 7 Aug 2024 in National Assembly: maafisa kila baada ya miaka mitatu ili mtu asikae kule zaidi. Kuna wengine ambao wanakatalia mijini kama Nairobi, Mombasa na sehemu zingine. Wenzao wanakaa msituni bila kufanya chochote mpaka wanapotea akili. Kuna sehemu inayoitwa Kiangwe; polisi akipelekwa pale, unamhurumia sana kwa sababu yeye hajazoea. Afadhali sisi kwa sababu tunaishi kule na tumezoea yale mazingira yetu. Polisi akifika pale, anakosa maji ya kuoga kwa wiki nzima. Anaweza kukaa hata bila kuoga. Wanafurahia wakati wa mvua kwa sababu wanapata maji mengi. Mvua inaponyesha, inabidi wayakusanye maji kwa muda. Kuna wakati ambapo maji yanaisha na wanabaki na ya kunywa tu. Wakati huo hawawezi ... view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus