Shariff Athman Ali

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 51 to 60 of 515.

  • 20 Nov 2024 in National Assembly: Iwapo mti huu una shida, basi ni kwa vile umeletwa na binadamu. Nimejulishwa kwamba mti huu haukuwepo Kenya. Ulikuwa ni wa kwingine. Maji ni mhimu. Kukiwa na mti unaokunywa maji zaidi, basi unafaa kuondolewa. Sisi binadamu tuna vita na wanyama kwa sababu ya maji. Hayo maji ni muhimu kwa mazingira, kwetu sisi binadamu, na wanyama kwa jumla. Kuna haja ya kuharakisha hili suala. Sasa hivi kuna Waziri mtendakazi kwenye Wizara husika, Insh’Allah. Kulikuweko Waziri mwingine mtendakazi kule. Insh’Allah, wote walifanya kazi nzuri. Najua tutasaidika. Tuko pamoja naye kurekebisha. Iwapo huu mti waafaa kutolewa, bila shaka utolewe na usipandwe kabisa. Tupande ... view
  • 20 Nov 2024 in National Assembly: Mhe. Spika, niko na tatizo lingine linalotokana na swala hili. Waziri, Lamu Mashariki ina wakulima wa simsim na hawatumii madawa yeyote. Lakini kuna shida kwa sababu majirani wetu wanatumia madawa ya kuua wadudu. Kwa hivyo, simsim zao zilizopelekwa kwenye soko za nje, zilirudishwa. Kutokana na hayo, zimeharibia sifa wakulima wote wa simsim. Ninavyoongea, simsim zimejaa kwenye soko za Lamu Mashiriki. Uko na mipango gani ya kuwasaidia wakulima hao ili mazao yao ya simsim yaweze kuuzwa? Wakulima wa Lamu Mashariki wako tayari mazao yao ya simsim yapimwe maana wao hawatumii madawa za kuua wadudu. Kama vile maziwa inapokuwa nyingi kupita kiwango ... view
  • 20 Nov 2024 in National Assembly: Mhe. Naibu Spika, swali nililouliza halikujibiwa. Limepotea na ameambiwa aende kisha atarudi. Swali langu ni kuhusu simsim . Ningependa nilirejelee. Watu wangu walikuja kuniambia kwamba wako na shida. Kuna wakulima wa simsim Lamu Mashariki na wameniambia kwamba majirani wao wanatumia madawa na bidhaa zao zilirejeshwa. Hilo limefanya wao kupoteza soko. Simsim iko nyingi kule na haina soko. Je, mko na mipangilio ipi kusaidia hao wakulima wa Lamu Mashariki? Wao pia ni Wakenya. Ministry of Agriculture and Livestock Development inafanya kazi sehemu zingine, lakini Lamu Mashariki ni kama hakuna wakulima ilhali tuko nao. Tunazalisha c ashew nuts nyingi zaidi Kenya. Watu ... view
  • 20 Nov 2024 in National Assembly: On a point of order, Hon. Deputy Speaker. view
  • 20 Nov 2024 in National Assembly: Naibu Spika, niko kwa hoja ya nidhamu. Je, ni haki Waziri kusema ataenda kuuliza county government na tuna hakika wafugaji wa simsim kwetu Lamu Mashariki hawajawahi kusaidiwa na chochote na serikali hiyo? Wanajitegema wenyewe ilhali sehemu zingine wakulima wa maziwa, majani chai, kahawa, na muguka, wote wanapata fedha kutoka kwa Serikali ya kitaifa. Nilikuwa natarajia aniambie mikakati iliyopo na kama hana saa hii, aniambie atarudi Jumatano anielezee ana mikakati gani. Si vema kuniambia niende kwa serikali gatuzi niulize Gavana. Mimi si Seneta wala mwakilishi wa wadi! view
  • 20 Nov 2024 in National Assembly: Mhesh. Naibu Spika, tukizungumza kuhusu makadamia, tunafaa kuizungumzia pamoja na nuts zingine, haswa korosho ambayo katika packaging, huchaganywa na macadamia. Nataka pia Waziri anapozungumza, azichanganye vivyo hivyo. Akizungumzia makadamia, azungumzie korosho. view
  • 20 Nov 2024 in National Assembly: Mhesh. Naibu Spika, tulienda na Kamati ya Dayaspora kule USA na tukakutana na wanadayaspora wakatuambia – nataka Waziri ajue – kuwa demand ya korosho haijafikiwa hata robo. Wanahitaji korosho sana kule. Lakini kwa sababu mmea huu unatoka Pwani, haufanyiwi bidii. Kwa kuwa naona Serikali hii inazingatia mimea mingine, naomba ishughulikie sana korosho. Hii itainua Kenya kwa ujumla. Wengine wanapotoa chai na kahawa, na sisi tutoe korosho na Kenya itainuka. view
  • 13 Nov 2024 in National Assembly: Ahsante, Mhe. Spika. Ni vile sisi ni wawakilishi wa wananchi na wakituona tuko hapa leo lakini hatujauliza maswali yanayowahusu, tukirudi katika maeneo bunge yetu, tutakuwa na shida. Mwanzo, ningependa kumpongeza Waziri kwa vile yeye ni mungwana sana. Tunapoenda ofisini mwake, huwa tunapokelewa vizuri. Ninataka Waziri ajue kuwa Lamu Mashariki ndio eneo bunge pekee Kenya ambalo halina hata inchi moja ya barabara ya lami. Eneo Bunge la Lamu Mashariki lina barabara tatu. Mojawapo ni barabara ya Mtangawanda- Kizingitini ambayo mnaijua. Ninaomba mtueleze mikakati ya ujenzi wa barabara hiyo imefikia wapi angalau tuwe na barabara ya lami. Barabara ya pili ni ya ... view
  • 13 Nov 2024 in National Assembly: Mhe. Spika, Lamu Mashariki ina mazingira tofauti. Maeneo yetu sio yale wanabara mnaita landmass . Kwetu ni watermass . Tunahitaji seawalls, yaani zile kuta za bahari. Kuna kijiji kinachoitwa Bwajumwali ambacho karibu kibebwe na maji. Watoto pia wanabebwa na maji. Kijiji hicho kilijengwa kikiwa kidogo. view
  • 13 Nov 2024 in National Assembly: hakumaliza ujenzi na akakimbia. Mambo hayo pia yako katika Ministry yako. Kwa hivyo, tafadhali yaangalie. Ahsante, Mhe. Spika. view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus