Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo

Parties & Coalitions

All parliamentary appearances

Entries 1721 to 1730 of 2266.

  • 16 Oct 2018 in Senate: shetani atafanya kazi yake anayoijua katika akili ya yule kijana ama yule dada. Kwa hivyo, kipengele kama hiki ni muhimu na ninaiunga mkono ili tuweze kufanya mageuzi ndiposa ipatikane katika sheria zetu za kupambana na mambo ya ugaidi. Jambo lingine ningependa kuzungumzia ni vijana kupigwa risasi na kuuawa katika mkoa wa Pwani; Mombasa, Kilifi na Kwale. Sio wengine wanaofanya jambo kama hili ila ni polisi. Jambo hili linafanywa na watu ambao wanasilaha. Mara nyingi ukienda kuuliza baada ya siku mbili au tatu kuhusu mtu ambaye amepigwa risasi, utaambiwa ya kwamba ‘hatujui ni nani alimuua’. Visa kama hivi vinafanya watu wawe ... view
  • 16 Oct 2018 in Senate: Magenge kama haya yanafaa kuangaziwa ili tumalize ugaidi. Wakati Serikali inatafuta bunduki zilizopotea, wanafaa kupeana amnesty kwa walio na bunduki bandia wazirejeshe ili wasamehewe. Watu wengi wanajiunga na vikundi vya ugaidi. Wengi wako hapa Kenya na wengine wako Somalia. Ndio maana wanajeshi wa Kenya Defence Forces (KDF) wako kule Somalia kwa sababu sote hapa tunataka amani ambayo haiwezi kuwepo bila sisi kuwa na majeshi yetu Somalia. Hata hivyo, hiyo sio suluhu pekee. Tunafaa kuzingatia kuwa kuna watoto wetu kule na ikiwa wataondoka--- Kwa mfano, kuna mmoja aliyekuwa akilia kuwa hana miguu na mikono kutokana na pengine kulipuliwa kwa bomu au ... view
  • 16 Oct 2018 in Senate: Tuko hapa sote kama Wakenya. Ikiwa nchi hii itaharibika, Wakenya wa tabaka zote wataharibikiwa. Hatuwezi kusema kuwa ugaidi unafanywa na Waislamu ama Wakristo. Vile vile, hatuwezi kusema kuwa unafanywa na watu ambao hawana dini. Ugaidi unahusu kila mtu; awe Mkristo au Mwislamu. Tumeona vijana wetu wa dini za Kikristo na Kiislamu na vile vile wasiokuwa na dini wakijiunga na ugaidi. Tumeshuhudia vijana wetu wa tabaka mbalimbali za Kenya wakijiunga na makundi ya kigaidi niliyotaja hapo awali. Kwa hivyo, Serikali inafaa kuhakikisha kuwa Kifungu hiki cha 12 kinawekwa mwafaka. Baada yao kupewa The electronic version of the Senate Hansard Report is ... view
  • 16 Oct 2018 in Senate: mafunzo, Serikali inafaa kutangaza kujumuika kwao na Wakenya na wasichukuliwe kama wagonjwa wa ukoma ya kwamba hawawezi kupata kazi. Hiyo inawafanya kubaki kama mayatima. Ikiwa siwezi kupata kazi, basi nitarudi kule nilikotoka. Kwa hivyo, sisi kama Wakenya lazima tuzingatie mambo haya. Serikali nayo inafaa kujikakamua vilivyo ili kutekeleza wajibu wake kwa Wakenya. view
  • 16 Oct 2018 in Senate: Bi. Spika wa Muda, naunga mkono Mswada huu. view
  • 16 Oct 2018 in Senate: Asante sana, Bi. Spika wa Muda, kwa kunipa nafasi hii. Ningependa kumuunga mkono Sen. Pareno katika Mswada huu ambao ameuleta kuhusu jinsi ya kuwasilisha malalamiko ya wananchi katika Bunge. The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor, Senate. view
  • 16 Oct 2018 in Senate: Bi Spika wa Muda, tulikuwa hapa mwaka wa 2013 katika Bunge la Kumi na Moja. Wakati huo hatukuwa na sheria ambapo wananchi wangepewa nafasi ya kutoa malalamiko yao katika Bunge. Nina furaha kuwa sheria zetu zinawezesha watu wetu katika kaunti zetu au mtu binafsi kuleta malalamiko yake mbele ya Seneti hii na kusikilizwa. Jambo hili lilikuwa limeleta joto nyingi kwa MCAs wetu katika Serikali za Ugatuzi kutosikizana. Na tulikuwa na hiyo shida katika Bunge la Kumi na Moja. Lakini hivi sasa nimeona ya kwamba mmezingatia huu Mswada ambao umeletwa na dada Sen. Pareno. Nimeona ya kwamba hii sheria ambayo itatusaidia ... view
  • 16 Oct 2018 in Senate: la kaunti, ombi hilo litakubaliwa. Kipengele kama hiki kinazuia utumiaji vibaya wa mamlaka katika serikali za kaunti. Tumegundua kwamba wakati mwingi, sheria zinatumiwa vibaya, haswa katika serikali za kaunti. Sheria hii itaweza kuweka mwelekeo ama mwangaza kisawasawa kisheria ili kila mtu ambaye ana jukumu kama katibu asitumie sheria hii kukataza malalamiko ambayo yamewasilishwa na mwananchi kwa bunge la kaunti ama serikali ya kaunti kwa misingi kwamba haikuzingatia muundo wa kuwasilisha ombi hilo kwa bunge. Tunataka kupitisha sheria hii ili itumike vivyo hivyo. Pia, maagizo ya vile watu wanaweza kuja pamoja na kuongea juu ya malalamiko yao, sheria hii itakuwa nzuri ... view
  • 16 Oct 2018 in Senate: ambazo zitakuwa zinaenda katika bunge za kaunti. view
  • 2 Oct 2018 in Senate: Asante, Mhe. Naibu Spika kwa kunipa fursa hii kueleza maoni yangu juu ya Mswada huu. Kwanza, nampa heko ndugu yetu, Sen. Cherargei kwa kuleta Mswada huu mbele ya Bunge la Seneti. Imemchukua muda mwingi wa kutafakari na kuona umuhimu sisi kuwa na sheria hii. Kama mwanasheria nasema ya kwamba kusimamisha mfanyikazi wa Serikali tukianzia Rais, Naibu wake, Makatibu wa Kudumu, Baraza la Mawaziri, gavana anayetawala kaunti aliyochaguliwa na wale wanaochaguliwa na gavana kufanya kazi na yeye kama vile County Executive Committee (CECs) view

Comments

(For newest comments first please choose 'Newest' from the 'Discussion' tab below.)
comments powered by Disqus